Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo makanisa-ya-katika-China. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo makanisa-ya-katika-China. Onyesha machapisho yote

4/03/2018

Sura ya 55. Usieleze Kile Mungu Alicho Nacho na Kile Alicho


Mwenyezi Mungu alisema, Kazi na matamshi ya Mungu ya miaka michache iliyopita yote yamerekodiwa kimsingi katika kitabu, Neno Laonekana katika Mwili. Baadhi ya maneno katika kitabu hiki ni ya kinabii na yanatabiri vile enzi za baadaye zitakavyokuwa. Unabii kwa kweli ni mfumo wa jumla, na zaidi ya nusu ya kitabu kinajadili kuingia kwa mwanadamu kwa maisha, kinaweka wazi utu, na kinazungumzia kuhusu kumwelewa Mungu na tabia Yake. Na kuhusu enzi gani, enzi ngapi na ufalme wa aina gani mwanadamu ataingia baadaye, je, hakuna mipango makini, hakuna marejeleo maalum na zaidi hakuna vipindi vya muda? Yaani, enzi za baadaye hazikuhusu. Sasa hivi sio wakati na tuko mbali sana nayo.

1/19/2018

Umeme wa Mashariki | Njia… (1)

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki, injili
uhalisia,ushindi,Kanisa

  Umeme wa Mashariki | Njia… (1)

  Katika maisha yake, hakuna mtu anayejua ni aina gani ya vipingamizi ataenda kukutana navyo, wala hajui ni aina gani ya kusafishwa ambayo atapata mara kwa mara. Kwa wengine ni katika kazi yao, kwa wengine ni katika matazamio yao ya siku za baadaye, kwa wengine ni katika familia yao ya asili, na kwa wengine ni katika ndoa yao. Lakini kilicho tofauti nayo ni kwamba leo sisi, kundi hili la watu, tunateseka kwa ajili ya neno la Mungu. Yaani, kama mtu anayemtumikia Mungu, amekutana na vipingamizi katika njia ya kuamini katika Yeye, na hii ni njia ambayo waumini wote hufuata na ni njia iliyo chini ya miguu yetu yote.Ni kutoka katika kipengele hiki ndipo tunaanza rasmi mwendo wetu wa kuamini katika Mungu, kuanza maisha yetu kama binadamu, na kuingia katika njia sahihi ya maisha.