Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Biblia-na-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Biblia-na-Mungu. Onyesha machapisho yote

9/13/2019

“Kupita Katika Mtego” – Je, Kuamini katika Biblia Kunaweza Kuwakilisha Kumwamini Mungu? | Filamu za Injili (Movie Clip 3/7)



“Kupita Katika Mtego” – Je, Kuamini katika Biblia Kunaweza Kuwakilisha Kumwamini Mungu? | Filamu za Injili (Movie Clip 3/7)


Wachungaji na wazee wa ulimwengu wa dini hushikilia maneno ya Paulo katika Biblia yanayosema "Maandiko yote yametolewa kwa msukumo wa Mungu," wakiamini kwamba Biblia ni maneno ya Mungu kabisa na kufanya yote wanayoweza kuiinua Biblia na kuishuhudia, na kuifanya Biblia na Mungu kuwa visawe. Wanaamini kwamba Biblia inamwakilisha Bwana na kwamba imani katika Bwana ni imani katika Biblia. Je, Biblia nzima kweli imetolewa kwa msukumo wa Mungu? Je, Bwana, Mungu, yuko ndani ya Biblia? Je, ni kazi ya Mungu ambayo imetoa Biblia, au Biblia ambayo imetoa kazi ya Mungu? Je, Biblia inaweza kweli kumwakilisha Bwana? Video hii fupi itakuonyesha njia sahihi.

Zaidi: Maneno ya Roho Mtakatifu | "Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?"

8/18/2019

Swahili Gospel Full Movie "Fichua Siri Kuhusu Biblia" | Kufichua Hadithi ya Kweli ya Biblia


Swahili Gospel Full Movie "Fichua Siri Kuhusu Biblia" | Kufichua Hadithi ya Kweli ya Biblia


Feng Jiahui na wazazi wake waliamini katika Bwana tangu alipokuwa mdogo. Alipokuwa na umri wa miaka 18 aliingia katika shule ya seminari, na katika miaka yake ya 30 akawa mhubiri katika kanisa la nyumba huko Shanxi, Uchina. Kwa miaka mingi, Feng Jiahui alidumisha imani madhubuti ya kuwa Biblia ilitiwa msukumo na Mungu, na kwamba lazima tuamini katika Mungu kwa mujibu wa Biblia. Aliamini kuwa hakukuwa na maneno yaliyonenwa na Mungu nje ya Biblia, na kwamba kuondoka kutoka kwa Biblia kutakuwa uzushi.

8/12/2019

“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Tunaweza Kupata Uzima kwa Kuamini Katika Biblia? | Swahili Gospel Movie Clip 6/6



“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Tunaweza Kupata Uzima kwa Kuamini Katika Biblia? | Swahili Gospel Movie Clip 6/6


Mara kwa mara wachungaji na wazee huwafundisha watu kuwa hawawezi kuitwa waumini wakiondoka kwenye Biblia, na kwamba kwa kushikilia Biblia pekee ndiyo wanaweza kupata uzima na kuingia katika ufalme wa mbinguni. Kwa hivyo, je, kweli hatuwezi kupata uzima tukiondoka kwenye Biblia? Je, ni Biblia ambayo inaweza kutupa uzima, au ni Mungu ambaye anaweza kutupa uzima? Bwana Yesu alisema, "Tafuta katika maandiko; kwa kuwa ndani yake mnadhani kuwa mna uzima wa milele: na hayo ndiyo yananishuhudia. Nanyi hamtakuja Kwangu, kwamba mpate uhai" (Yohana 5:38-40).  

8/07/2019

“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Ni Vipi Kuna Makosa Ndani ya Biblia? | Clip 5/6



“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Ni Vipi Kuna Makosa Ndani ya Biblia? | Swahili Gospel Movie Clip 5/6

Watu wengi wanaamini kwamba Biblia yote imetiwa msukumo na Mungu, kwamba imetoka kabisa kwa Roho Mtakatifu, na kwamba hakuna hata neno moja lililo na kosa. Je, mtazamo wa aina hii unawiana na ukweli? Biblia iliandikwa na waandishi zaidi ya 40, yaliyomo yaliandikwa na kupangwa na mwanadamu, na haikufunuliwa moja kwa moja na Roho Mtakatifu. Ilikuwa vigumu kuepuka kuingiza mawazo na makosa ya mwanadamu wakati ambapo ilikuwa ikiandikwa na kupangwa na mwanadamu.


8/06/2019

“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Je, Biblia Nzima Imetiwa Msukumo na Mungu Kweli? | Swahili Gospel Movie Clip 4/6



“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Je, Biblia Nzima Imetiwa Msukumo na Mungu Kweli? | Swahili Gospel Movie Clip 4/6


Watu wengi katika ulimwengu wa dini wanaamini kwamba "Kila andiko limetolewa kwa msukumo wa Mungu," yote katika Biblia ni neno la Mungu. Je, kauli ya aina hii inakubaliana na ukweli? Biblia ni ushahidi wa Mungu pekee, rekodi ya kazi ya Mungu tu, na haijaundwa kwa matamshi ya Mungu kikamilifu. Ndani ya Biblia, ni maneno yaliyonenwa na Yehova Mungu, maneno ya Bwana Yesu, unabii wa Ufunuo na maneno ya manabii yaliyotolewa kwa msukumo wa Mungu pekee, ndiyo neno la Mungu. Mbali na hayo, mengi ya yaliyosalia yanahusiana na rekodi za kihistoria na ushuhuda wa uzoefu wa mwanadamu. Ikiwa ungependa kujua undani wa Biblia, basi tafadhali angalia video hii!

Video Sawa: Filamu za Kikristo | "Toka Nje ya Biblia" | Is Believing in the Bible Believing in God?

7/24/2019

“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Imefichuliwa: Uhusiano Kati ya Mungu na Biblia | Clip 2/6


“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Imefichuliwa: Uhusiano Kati ya Mungu na Biblia | Swahili Gospel Movie Clip 2/6


Wachungaji na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa dini wanaamini kuwa maneno na kazi zote za Mungu yamo ndani ya Biblia, kwamba wokovu wa Mungu katika Biblia ni mkamilifu na mradi watu waweke msingi wa imani yao katika Bwana katika Bibilia na washikilie Bibilia, basi wanaweza kunyakuliwa na wanaweza kuingia katika ufalme wa mbinguni. Je, kweli ukweli uko namna hii? Je, ni Mungu ambaye anaweza kufanya kazi kutuokoa, au Biblia? Je, ni Mungu ambaye anaweza kuonyesha ukweli, au Biblia? Ili kujifunza zaidi, tafadhali angalia video hii!

Tazama Zaidi: Tushughulikie Vipi Umeme wa Mashariki kwa Njia Inayolingana na Mapenzi ya Bwana?

6/08/2019

“Kupita Katika Mtego” – Kufunua Ukweli wa Maelezo ya Viongozi wa Kidini ya Biblia | Clip 2


“Kupita Katika Mtego” – Kufunua Ukweli wa Maelezo ya Viongozi wa Kidini ya Biblia | Filamu za Injili  (Movie Clip 2/7)


          Wachungaji na wazee wa ulimwengu wa dini mara nyingi huelezea Biblia kwa watu na kuwafanya washikilie Biblia. Kwa kufanya hivi, je, kwa kweli wanamwinua Bwana na kutoa ushahidi kwa ajili Yake? Watu wengi hawawezi kufahanu hili. Wachungaji na wazee huinua maneno ya mwanadamu ndani ya Biblia, kutumia maneno ya mwanadamu ndani ya Biblia kuchukua nafasi ya Bwana na kupinga maneno ya Bwana, na kuwaongoza watu katika ushirikina na kuabudu Biblia, ili Mungu atakapofanya kazi Yake mpya watu wengi wanajua tu Biblia na hawamjui Mungu, hata mpaka ambapo wanampiga Mwenye mwili msumari msalabani kulingana na Biblia. Kulingana na ukweli huu, je, wachungaji na wazee wa ulimwengu wa dini kweli wanamtukuza Bwana kwa kuelezea Biblia? Video hii fupi itakufunulia ukweli.

         Tazama Video: “Njia ya Kwenda katika Ufalme wa Mbinguni ni Yenye Hatari” – Kwa Nini Mafarisayo Wanampinga Mungu? | Swahili Gospel Film Clip 5/6

6/05/2019

Filamu za Kikristo | "Toka Nje ya Biblia" | Is Believing in the Bible Believing in God?


Filamu za Kikristo | "Toka Nje ya Biblia" | Is Believing in the Bible Believing in God?

       Wang Yue alikuwa ni mhubiri katika kanisa la nyumbani nchini China. Kwa moyo wake wote alihubiri na kuchunga kanisa la Bwana. Lakina wakti kanisa lake lilipoendelea kuwa tupu zaidi, alpatwa na wasiwasi lakini hangeweza kufanya chochote kulihusu. Alkiwa amepotea katika mateso na kushangazwa, yeye kwa bahati nzuri alikuja kukubali injili ya ufalme wa Mwenyezi Mungu. Alipofurahia utele wa neno la Mungu, yeye alielewa kwa kina upana wa wokovu wa Mungu. Hii ilifanya mateso na kudhoofika kwa kukosa kutwaliwa na Mungu na kuanguka katika giza iwe ya ukweli zaidi kwake. ]

5/13/2019

"Ivunje Laana" (6) - Je, Utiifu kwa Wachungaji na Wazee wa Kanisa ni Sawa na Kumtii Mungu?

"Ivunje Laana" (6) - Je, Utiifu kwa Wachungaji na Wazee wa Kanisa ni Sawa na Kumtii Mungu?

Waumini wengine huamini kwamba wachungaji na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa kidini wamechaguliwa na kuteuliwa na Bwana, na kwamba wote ni watu wanaomtumikia Bwana. Hivyo wanaamini kwamba kuwatii tu wachungaji na wazee wa kanisa ni kumtii Bwana, na kwamba kuwaasi au kuwahukumu wachungaji na wazee wa kanisa ni kumpinga Bwana. Wao huamini hata kuwa, katika makanisa, wachungaji na wazee wa kanisa peke ndio huelewa Biblia na huweza kuelezea Biblia, na almradi kile kinachohubiriwa au kufanywa na wachungaji na wazee wa kanisa kinakubaliana na Biblia na kina msingi katika Biblia, basi watu wanapaswa kuwatii na kuwafuata.

5/11/2019

“Ivunje Laana” – Je, Imani katika Biblia ni Sawa na Imani katika Bwana? (Clip 4/7)

Filamu za Injili | “Ivunje Laana” Movie Clip: Je, Imani katika Biblia ni Sawa na Imani katika Bwana?

Wachungaji wengi sana na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa kidini huamini kwamba Biblia inamwakilisha Bwana, na kwamba kuamini katika Bwana ni kuamini katika Biblia, na kuamini katika Biblia ni kuamini katika Bwana. Wao huamini kwamba mtu akiachana na Biblia basi hawezi kuitwa muumini, na kwamba mtu anaweza kuokolewa na anaweza kuingia katika ufalme wa mbinguni almradi ashikilie Biblia. Je, Bibilia inaweza kweli kumwakilisha Bwana? Je, uhusiano kati ya Biblia na Bwana ni upi hasa? Bwana Yesu alisema, "Tafuta katika maandiko;

5/09/2019

“Toka Nje ya Biblia” – Mungu Hufanya Kazi Kulingana na Biblia? (Clip 1/2)


Filamu za Injili | “Toka Nje ya Biblia” Movie Clip: Mungu Hufanya Kazi Kulingana na Biblia?


Wakati Bwana Yesu alkuwa akifanya kazi Yake katika Enzi ya Neema, akihubiri  kwamba ufalme wa mbinguni umekaribia na kuwaleta watu katika njia ya toba, Mafarisayo Wayahudi walimhukumu Yeye, wakisema kwamba maneno na kazi Yake zilikuwa kinyume na sheria za Agano la Kale, eti kuwa zilienda zaidi ya Agano la Kale, na kuwa yalikuwa ni uzushi. Katika siku za mwisho, Mwenyezi Mungu anafanya kazi Yake ya hukumu akianza na familia ya Mungu na anaelezea ukweli wote ambao unatakasa na kumuokia mwanadamu, na wachungaji na wazee wa ulimwengu wa kidini wanahukumu, wakisema kuwa maneno na kazi ya Mwenyezi Mungu huenda zaidi ya Biblia, na kwamba ni uzushi.

5/01/2019

"Sauti Nzuri Ajabu" (3) - Je, Hakuna Maneno au Kazi ya Mungu Nje ya Biblia?


Dondoo za Filamu za Injili "Sauti Nzuri Ajabu" (3) - Je, Hakuna Maneno au Kazi ya Mungu Nje ya Biblia? 

Watu wengi katika ulimwengu wa kidini wanasadiki kwamba maneno yote ya Mungu yako ndani ya Biblia, na chochote kilicho nje ya Biblia hakina kazi Yake na maneno. Hawatafuti nje ya Biblia matamko Yake katika kurudi Kwake. Je, wataweza kukaribisha kurudi kwa Bwana kama wataendelea kushikilia wazo hili? Je, Mungu angeweza kuzuiliwa tu kwa kuongea maneno yaliyo ndani ya Biblia? Biblia inasema: "Na pia kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya, ambayo, yote yakiandikwa, ninafikiri kwamba hata dunia yenyewe haingetosha vitabu hivyo ambavyo vitaandikwa" (Yohana 21:25). Mungu anasema: "Yote yaliyoandikwa katika Biblia ni machache na hayawezi kuwakilisha kazi yote ya Mungu" (Neno Laonekana katika Mwili).

Soma Zaidi: Neno la Mwenyezi Mungu

4/09/2019

Dondoo ya Filamu ya Bwana Wangu Ni Nani – Je, Kazi na Maneno Yote ya Mungu Yamo katika Biblia?


Dondoo ya Filamu ya Bwana Wangu Ni Nani – Je, Kazi na Maneno Yote ya Mungu Yamo katika Biblia?

Dunia nzima ya kidini yote huamini kwamba kazi na maneno ya Mungu yote yamo katika Biblia, na kwamba isipokuwa Biblia, hakuna maneno yaliyonenwa na Mungu na kazi Yake. Kwa hiyo, ili mradi uko mwaminifu kwa Biblia, hili litahakikisha kwamba utaweza kuingia ufalme wa mbinguni. Je, mawazo haya yanapatana na ukweli wa kazi ya Mungu? Kuna maneno ya Mungu nje ya Biblia? Ni nini hasa kitakachomwongoza mwanadamu kuingia ufalme wa mbinguni? Je, ni kushika Biblia, ama ni kufuata nyayo za Mwanakondoo? Dondoo hii itafichua majibu yote kwako!

Sikiliza zaidi: Neno la Mwenyezi Mungu

9/26/2018

Kwa Nini Mafarisayo Wanampinga Mungu?



"Njia ya Kwenda katika Ufalme wa Mbinguni ni Yenye Hatari" (5) - Kwa Nini Mafarisayo Wanampinga Mungu?

Mafarisayo wa dunia ya kidini wote wana maarifa nyingi ya Maandiko na wamemtumikia Mungu kwa miaka mingi, na bado hawatafuti na kuchunguza kuonekana na kazi ya Mungu mwenye mwili tu, lakini kinyume na hayo, wanahukumu vikali, kushutumu, na kupinga. Hili hakika ni la kushangaza! Hivyo kwa nini Mafarisayo wa dunia ya kidini wanamshutumu na kumpinga Mungu? Mungu anasema, "Wale wanaosoma Biblia kwa makanisa makubwa hukariri Biblia kila siku, lakini hakuna yeyote anayeelewa madhumuni ya kazi ya Mungu.

5/28/2018

Enda Nje ya Biblia: Hudhuria Karamu ya Ufalme wa Mbinguni Pamoja na Bwana

Watu wengi ambao wana imani katika Bwana huhisi kwamba maneno na kazi ya Mungu vyote viko katika Biblia, kwamba wokovu wa Mungu kama ulivyoelezewa katika Biblia tayari umejaa, kwamba imani katika Mungu lazima iwe kwa msingi wa Biblia na kwamba kama imani yetu kwa Mungu ni kwa msingi wa Biblia, basi kwa hakika tutanyakuliwa kuingia katika ufalme wa mbinguni. Dhana hizi za kidini hutenda kama kamba zisizoonekana ambazo huzifunga kwa uthabiti na kuzisonga fikira zetu kiasi kwamba hatuitafuti kazi ya Roho Mtakatifu na hutufanya tusiweze kuitii kazi ya sasa ya Mungu.

3/26/2018

Dondoo ya Filamu ya Bwana Wangu Ni Nani – Ni nini uhusiano kati ya Mungu na Biblia?👏🎬


Umeme wa MasharikiUtambulisho 
🎉🎉🎉🎉🎉🎉🎉🎉🎉🎉*******************👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏
Kwa miaka elfu mbili, tumemwamini Bwana kulingana na Biblia, na wengi wetu sana huamini "Biblia inamwakilisha Bwana, kumwamini Mungu ni kuamini Biblia, kuamini Biblia ni kumwamini Mungu," Je, mawazo haya ni sahihi? Kumwamini Mungu kunamaanisha nini kwa kweli? Kunamaanisha nini kuamini Biblia? Ni nini uhusiano kati ya Biblia na Mungu? Je, imani pofu na kuabudu Biblia yanamaanisha kwamba tunamwamini na kumwabudu Mungu? Video hii itafichua majibu kwako!

11/20/2017

Video za Kikristo | Kuelezea Wazi Uhusiano Kati ya Biblia na Mungu | "Biblia na Mungu" (Swahili Subtitles)


Video za Kikristo | Kuelezea Wazi Uhusiano Kati ya Biblia na Mungu | "Biblia na Mungu" (Swahili Subtitles)

Liu Zhizhong ni mzee katika kanisa moja la mtaani la nyumba nchini China. Amekuwa muumini kwa zaidi ya miaka 30, na amesisitiza bila kukoma kwamba “Biblia ni ufunuo wa Mungu,” “Biblia inamwakilisha Mungu, kuamini katika Mungu ni kuamini katika Biblia, kuamini katika Biblia ni kuamini katika Mungu.” Moyoni mwake, Biblia ni kuu. Kwa sababu ya upendo na imani yake pofu katika Biblia, hajawahi kutafuta au kuitazama kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho. Hadi siku moja, alipowazuia waumini kusoma maneno ya Mwenyezi Mungu mtandaoni, akawa na fursa ya kukutana na wahubiri kutoka katika Kanisa la Mwenyezi Mungu.