10/20/2017

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana "Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu"



Ha … nyimbo ni nyingi na ngoma ni za madaha;

ulimwengu na miisho ya dunia zinakuwa bahari inayosisimka.

Ha … mbingu ni mpya na dunia ni mpya.

Eneo kubwa la ulimwengu limejaa kusifu; tunapiga ukelele na kuruka kwa shangwe.

Milima yajiunga na milima na maji mengi kujiunga na maji mengi, ndugu wote wa kiume na kike ni wandani.

Twamsifu Mungu bila kukoma. Viumbe wampenda Mungu,

wakija, mbele ya kiti chake cha enzi kwa furaha kuabudu pamoja.

Mungu Amefichua katika Sayuni kwa ulimwengu uadilifu Wake na utakatifu Wake.

Watu wote wa Mungu wanachangamka kwa furaha, wakimtukuza Mungu bila kukoma.

Msifuni Mungu, msifuni Mungu!

Haleluya! Msifuni Mungu, msifuni Mungu!

Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli.

Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.

Sauti inayosifu yapasua mbingu.

Acha sisi, waume kwa wake, wazee kwa vijana, tuwahi pamoja.

Watoa nyimbo nami natoa ngoma, uimbe nami nishirikiane.

Aliyetiwa aibu ni shetani—joka kubwa jekundu; lililotukuzwa ni jina la Mwenyezi Mungu wa kweli.

Tumeona tabia adilifu ya Mungu kutoka kwa kazi Yake.

Mwenyezi Mungu ni Mungu mwadilifu. Watu wote wa Mungu wameiona sura Yake tukufu.

Sisi sote hufuata kumpenda na kumtosheleza Mungu, tukipenda kuwa waaminifu Kwake milele.

Msifuni Mungu, msifuni Mungu!

Haleluya! Msifuni Mungu, msifuni Mungu!

Njooni! Hebu tumsifu Mungu!

Njooni! Hebu tumsifu Mungu!

Kuja!

Milima inashangilia na maji mengi yanacheka,

mataifa yote na watu wote wanacheka kwa furaha. Mtazamo mpya ulioje!

Hiyo mbingu mpya, dunia mpya, na ufalme mpya!

Tunacheza na kuimba nyimbo mpya kwa Mungu; tumefurahi sana!

Nyimbo nzuri sana zaimbiwa Mungu, ngoma za madaha zaidi zawasilishwa kwa Mungu.

Moyo mnyofu umeinuliwa juu kwa Mungu, moyo wa kweli umetolewa juu kwa Mungu.

Watu wote wa Mungu na vitu vyote watamsifu Yeye milele bila kukoma. Ha!

Lo! Sayuni ni tukufu sana!

Makao ya Mungu hung'aa kwa miale ya mwanga. Utukufu wake hung'aa kotekote ulimwengu mzima.

Mwenyezi Mungu huvaa tabasamu, na hukalia enzi Yake akitazama umbo jipya la ulimwengu mzima. Ala!

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Kauli Maalum: Uzalishaji huu wa video ulitengenezwa kama mradi usio wa faida na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Wahusika wanaoonekana katika uzalishaji huu wanafanya kwa msingi wa kutotafuta faida, na hawajalipwa kwa njia yoyote. Video hii isisambazwe kwa mtu mwingine kwa minajili ya faida, na ni matumaini yetu kwamba kila mtu atashiriki kuigawa na kuisambaza hadharani. Wakati unapoisambaza, tafadhali sisitiza chanzo chake. Bila ridhaa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, hakuna shirika, kundi la kijamii, au mtu binafsi anayeweza kubadilisha au kuhudhurisha visivyo maudhui ya video hii. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni