1/06/2018

Umeme wa Mashariki | 13 Maana ya Utendaji wa Watu Kuamua Matokeo Yao

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,kanisa
hukumu,ukweli
neno la Mwenyezi Mungu13.Maana ya Utendaji wa Watu Kuamua Matokeo Yao
Kwa sasa, utendaji wa watu unaamua matokeo yao, lakini huu utendaji ni upi? Je, unaujua? Nyinyi mnaweza kufikiri kwamba hili linarejelea tabia ya watu iliyopotoka ikijionyesha kazini mwao, lakini halimaanishi lile. Utendaji huu unanena kuhusu ikiwa unaweza kuweka ukweli kwenye vitendo au la na ikiwa unaweza kusalia mwaminifu na kujizatiti unapotenda wajibu wako au la, na vilevile mtazamo wako wa kumwamini Mungu, msimamo wako kwa Mungu, uamuzi wako wa kuteseka kwa ajili ya ugumu, mtazamo wako kwa kukubali hukumu na kupogolewa, kiwango chako cha mabadiliko na idadi ya dhambi kubwa. Haya yote yanachangia katika utendaji wako. Utendaji huu haumaanishi kiwango cha mwisho cha kufichua tabia yako iliyopotoshwa, lakini badala yake umefanikiwa kwa kiasi gani katika imani yako kwa Mungu. Iwapo matokeo ya watu yangeamuliwa kulingana na maonyesho ya asili yao, basi hakuna mtu ambaye angeokolewa. Je, hii ingekuwaje haki ya Mungu? Ikiwa wewe ni kiongozi, asili yako itajionyesha zaidi, na yeyote ambaye atajionyesha zaidi hatakuwa na uhakika sana wa kusalia. Kama hii ingeamua matokeo ya watu, basi kadiri watu wangezidi kutenda kazi katika kiwango cha juu, ndivyo wangezidi kumalizika haraka; kadiri wangezidi kuwa katika kiwango cha juu, ndivyo wangezidi kuonyesha asili yao katika kiasi kikubwa. Kama hali ingekuwa hivi, basi ni nani ambaye angethubutu kutekeleza wajibu wake? Kwa njia hii, je, haingekuwa kwamba wale ambao hawatekelezi wajibu wao wangeokolewa wote?
Utendaji huu unahusiana na ikiwa wewe ni mwaminifu na umejitoa kwa Mungu au la, ikiwa una upendo kwake au la, ikiwa unaweka ukweli kwenye matendo au la na vilevile ni katika kiwango gani ambacho umebadilika. Ni kulingana na utendaji huu kwamba hukumu yako inaamuliwa; si kulingana na kiwango cha upotovu wa tabia yako kinachojionyesha. Ukifikiria jinsi hii, umetafsiri vibaya mapenzi ya Mungu. Asili yote ya wanadamu ni sawa, ni vile tu kuna ubaya na uzuri wa ubinadamu. Hata usipoonyesha, asili yako bado ni sawa na yule anayeonyesha. Mungu Anajua vyema kilicho katika undani wa mwanadamu. Huhitaji kuficha chochote — Mungu huchunguza mioyo ya watu na mawazo. Ikiwa upotovu wako mwingi unafichuliwa wakati unapofanya kazi katika kiwango cha juu, Mungu atauona; ikiwa hutafanya kazi na usifichuliwe, je, Mungu hajui kuuhusu? Je, huku si kuamini uongo wako? Ukweli ni kwamba Mungu Anajua asili yako nje na ndani, bila kujali ulipo. Mungu Anajua vyema wale wote wanaofanya kazi yao, lakini je, si pia Ajua wale wasiofanya? Watu wengine hudhani kuwa hao viongozi walio kwenye hadhi ya juu wanachimba makaburi yao tu, kwa sababu upotovu wao mwingi utajifichua na kuonekana na Mungu pasi na kuepuka. Je, ungefichuliwa sana vile iwapo hawangeifanya kazi? Kufikiria kwa jinsi hii ni kwa upuzi! Ikiwa Mungu hauoni, basi si Hataweza kuuhukumu? Kama hali ingekuwa ile, je, haingekuwa kwamba wale ambao hawafanyi kazi wangesalia wote? Kulingana na kuelewa kwa mwanadamu, Mungu hangeona mabadiliko ya wale ambao hufanya kazi, bila kujali mabadiliko hayo ni makuu kiasi gani; Mungu Angewahukumu tu kulingana na maonyesho yao ya upotovu. Kinyume na hayo, Mungu hangewahukumu wale ambao wanaonyesha machache, licha ya kubadilika kwa kiasi kidogo. Je, unaamini kuwa hii ni haki ya Mungu? Je, mtu yeyote anaweza kusema kuwa Mungu ni mwenye haki iwapo Angefanya hili? Je, huku sio kutafasiri kubaya kwako ambako kunapelekea kuelewa kwa Mungu kubaya? Basi, je, imani yako kwa Mungu si ni ya uongo? Je, huku si kuamini kuwa Mungu sio mwenye haki daima? Je, si imani kama ile ni kufuru kwa Mungu? Ikiwa huna kitu chochote kilicho hasi na lolote jema halifichuliwi pia, bado huwezi kuokolewa. Jambo kuu ambalo huamua matokeo ya watu ni utendaji wao mwema. Lakini, hakuwezi kuwa na kitu hasi sana vilevile—kama ni kikuu kiasi cha kuleta maafa au adhabu, basi wote wataangamizwa. Kama kungekuwa jinsi mnavyofikiria, wale walio wafuasi wa kiwango cha chini wangepata wokovu mwishowe, na wale ambao ni viongozi wangekwisha. Una wajibu ambao lazima uutekeleze; lakini unapoutekeleza wajibu huo, utafichua upotovu wako licha yako mwenyewe, ni kama unakwenda kwa gilotini. Kama matokeo ya watu yangeamuliwa na asili yao, hakuna yeyote ambaye angeokolewa—kama hali kweli ingekuwa hii, basi, je, haki ya Mungu ingekuwa wapi? Haingeonekana kabisa. Nyinyi nyote mmeelewa mapenzi ya Mungu visivyo.
2. Utendaji Huu ni Kwa Ajili ya Kazi ya Mungu kwa Watu
Acheni niwape mfano: Katika shamba la miti ya matunda, mwenyewe hunyunyuzia maji na kutia mbolea, kisha husubiri matunda. Miti ambayo inazaa matunda ni mizuri na inahifahdiwa; ile ambayo haizai matunda bila shaka ni mibaya na haitahifadhiwa. Fikiria hali hii: Mti unazaa matunda, lakini una ugonjwa, na baadhi ya matawi mabaya yanahitaji kupogolewa. Je, mtu huu unapaswa kuhifadhiwa? Unapaswa kuhifadhiwa, na utakuwa mzuri baada ya kupogolewa na kutibiwa. Fikiria hali nyingine: Mti hauna maradhi, lakini hauna matunda—mti kama huu haufai kuhifadhiwa. Je, huku “kuzaa matunda” kunamaanisha nini? Kuna maana ya kazi ya Mungu kuwa na athari. Mungu anapofanya kazi kwa watu, asili yao haina vingine ila kujionyesha, na kwa ajili ya upotovu wa Shetani hawataepuka kuwa na dhambi, lakini katikati ya haya kazi ya Mungu ndani yao itazaa matunda. Ikiwa Mungu haoni hivyo, lakini Anaona tu asili ya mwanadamu ikionyeshwa, basi ule hautaitwa wokovu wa mwanadamu. Tunda la watu kuokolewa linadhihirishwa hasa katika kutekeleza wajibu kwao na kuweka ukweli kwenye matendo. Mungu huangalia kiwango cha watu cha mafanikio katika sehemu hizo na pia ukubwa wa dhambi zao. Hali hizi mbili zinachangia katika kuamua matokeo yao na ikiwa watasalia au la. Mathalani, watu wengine walikuwa wapotovu sana, wakijitolea kabisa kwa miili yao, na wala sio kwa familia ya Mungu. Hawakutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu hata kidogo, lakini sasa wanatekeleza wajibu wao kwa shauku na wako na moyo mmoja na Mungu—kwa huu matazamo, je, kumekuwa na mabadiliko? Haya ni mabadiliko. Ni mabadiliko haya ambayo Mungu Anataka. Pia, watu wengine walipenda kusambaza mawazo walipokuwa nayo, lakini sasa wanapokuwa na mawazo mengine, wanaweza kuwa watiifu na kufuatilia ukweli, bila kuyasambaza au kufanya kinyume na Mungu. je, kumekuwa na mabadiliko? Naam! Watu wengine wanaweza kuwa wamepinga wakati mmoja waliposhughulikiwa na kupogolewa tena, lakini sasa wanapopogolewa na kushughulikiwa, wanaweza kujifahamu. Baada ya kuyakubali, wanapitia mabadiliko ya kweli—je, hii si athari? Naam! Hata hivyo, bila kujali mabadiliko yako ni makuu kiasi gani, asili yako haiwezi kubadilishwa kwa mara moja. Haiwezekani kutofichua dhambi zozote, lakini ikiwa kuingia kwako kutafanywa kwa kawaida, hata kwa uasi mwingine, utakuwa na ufahamu wake wakati huo. Ufahamu huu unaweza kukuletea mabadiliko ya mara moja na hali yako itaimarika na kuwa nzuri zaidi na zaidi. Unaweza kuwa na dhambi mara moja au mbili, lakini sio kila mara. Haya ni mabadiliko. Haimaanishi kwamba mtu aliyebadilika kwa kitengo fulani hana dhambi zozote tena; huo sio ukweli. Aina hii ya mabadiliko ina maana kuwa mtu aliyepitia kazi ya Mungu anaweza kuweka ukweli mwingi kweye vitendo na anaweza kutenda baadhi ya yale ambayo Mungu anahitaji. Dhambi zao zitapungua na kuwa chache zaidi na zaidi na matukio ya kuasi yatakuwa machache na madogo. Unaweza kuona kutokana na haya kuwa kazi ya Mungu imekuwa na athari; kile ambacho Mungu anataka ni kujionyesha kama huku ambako matokeo haya yamefanikishwa kwa watu. Hivyo, jinsi ambavyo Mungu Anashughulikia matokeo ya watu na Anavyomtendea mtu ni yenye haki kabisa, mwafaka na isiyo na mapendeleo. Unahitaji tu kutia bidii katika kutumia rasilmali yako kwa ajili ya Mungu, kuweka moyo wako wote katika kutenda ukweli ambayo unapaswa bila kusita, na Mungu hawezi kukutendea isiyo haki. Ebu fikiria: je, wale wanaoweka ukweli kwenye vitendo wanaweza kuadhibiwa na Mungu? Watu wengi wanashuku tabia ya Mungu yenye haki na wanachelea kuwa bado wataadhibiwa ikiwa wataweka ukweli kwenye vitendo; wanaogopa kuwa Mungu hataona uaminifu wao na kujitolea kwao. Watu wengine wanakuwa wa kutoonyesha hisia baada ya kupogolewa na kushughulikiwa; wanahisi wanyonge kiasi cha kutotekeleza wajibu wao na wanapoteza uaminifu wao na kujitolea kwao. Kwanini hivi? Hili kwa kiasi ni kwa ajili ya watu kukosa ufahamu kuhusu kiini cha matendo yao ambayo hupelekea kutokubali kupogolewa na kushughulikiwa. Pia kwa kiasi ni kwa ajili ya watu kutoelewa umuhimu wa kushughulikiwa na kupogolewa, wakiamini hilo kuwa ishara ya kuamuliwa kwa matokeo yao. Kwa sababu hiyo, kimakosa watu huamini kuwa wakiwa na uaminifu fulani na kujitolea kwa Mungu, basi hawawezi kushughulikiwa na kupogolewa; wakishughulikiwa, haiwezi kuwa haki ya Mungu. Kutoelewa kama huku kunawafanya wengi kutoaminika na kutojitolea kwa Mungu. Hakika, yote ni kwa sababu watu ni waongo sana; hawataki kupitia ugumu—wanataka kupata baraka kwa njia rahisi. Hawana ufahamu wa haki ya Mungu. Si kwamba Mungu hajafanya lolote la haki ama kwamba hatafanya lolote la haki, ni tu kwamba watu daima hawafikiri kwamba Anayofanya Mungu ni haki. Machoni pa wanadamu, kama kazi ya Mungu haipatani na mapenzi ya mwanadamu ama kama si matarajio yao, ina maana kuwa Yeye si mwenye haki. Watu kamwe hawatambui wakati kile wanachofanya si sahihi ama haiambatani na ukweli; katu hawatambui kwamba wanampinga Mungu. Kama Mungu hangewashughulikia ama kuwapogoa watu kwa ajili ya dhambi zao na wala kuwakaripia kwa sababu ya makosa yao, lakini daima angekuwa mtulivu, kamwe bila kuwakasirisha, daima bila kuwakosea, na daima bila kufunua makovu yao, lakini angewakubalia kula na kuwa na wakati mzuri na Yeye, basi watu hawangelalamika kuwa Mungu sio mwenye haki. Wangesema kuwa Mungu ni mwenye haki kwa unafiki. Kwa hivyo, watu bado hawaamini kuwa kile ambacho Mungu Anahitaji ni utendaji wao baada ya kubadilishwa kwao. Je, Mungu angekuwa vipi na uhakika kama wangeendelea na hayo? Kama Mungu angewasuta watu kidogo, hawangeamini tena kuwa Yeye huona utendaji wao baada ya mabadiliko. Wangeacha kuamini kuwa Yeye ni mwenye haki, na hawangekuwa na radhi kubadilishwa. Kama watu wangeendelea na hali hii, wangehadaiwa na mawazo yao wenyewe.
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo
 Jifunze zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni