2/16/2018

17 Ufahamu wa Kupata Mwili

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki, Kupata Mwili
Bwana-Yesu, Kupata Mwili
Mwenyezi Mungu alisema, Kumjua Mungu kunapaswa kufanywa kupitia kwa kusoma neno la Mungu na kulielewa neno la Mungu. Watu wengine husema: "Sijamwona Mungu mwenye mwili, hivyo nitawezaje kumjua Mungu?" Neno la Mungu kwa kweli ni maonyesho ya tabia ya Mungu. Kutoka kwa neno la Mungu unaweza kuuona upendo wa Mungu kwa wanadamu, wokovu Wake wa wanadamu, na jinsi Anavyowaokoa ... kwa sababu neno la Mungu linaonyeshwa na Mungu ikilinganishwa na Mungu kumtumia mwanadamu kuliandika. Linaonyeshwa na Mungu binafsi. Ni Mungu Mwenyewe Akielezea maneno Yake mwenyewe na sauti Yake ya ndani. Kwa nini tunayaita maneno ya dhati? Kwa sababu hayo hutolewa kutoka ndani kabisa, Akionyesha tabia Yake, mapenzi Yake, mawazo Yake, upendo Wake kwa wanadamu, wokovu Wake wa wanadamu, na matarajio Yake ya wanadamu. Miongoni mwa maneno ya Mungu kuna maneno makali, maneno ya upole na laini, maneno mengine yenye kuzingatia, na kuna maneno mengine ya ufunuo ambayo hayana utu. Ikiwa unayaangalia tu maneno ya ufunuo, unahisi kwamba Mungu ni mkali kabisa. Ikiwa unaangalia upande wa upole na laini tu, Mungu anaonekana kuwa hana mamlaka mengi. Kwa hiyo hupaswi kuelewa nje ya muktadha katika hili. Lazima uliangalie kutoka kila pembe. Wakati mwingine Mungu huzungumza kwa mtazamo mpole na wenye huruma, na watu wanauona upendo wa Mungu kwa wanadamu; wakati mwingine Yeye huzungumza kwa mtazamo mkali, na watu wanaona tabia ya Mungu isiyoweza kukosewa. Mwanadamu ni mchafu kwa njia ya kusikitisha na hastahili kuuona uso wa Mungu, na hastahili kuja mbele za Mungu. Watu kuja mbele za Mungu sasa ni kwa neema ya Mungu tu. Hekima ya Mungu inaweza kuonekana kutokana na jinsi Mungu anavyofanya kazi na maana ya kazi Yake. Hata kama watu hawajakutana na Mungu, bado wataweza kuona mambo haya katika neno la Mungu. Mtu ambaye ana ufahamu wa kweli anapokutana na Kristo, ufahamu wake unaweza kufanana na Wake, lakini wakati mtu ambaye ana ufahamu wa kinadharia tu anakuja katika mawasiliano na Mungu, hauwezi kufananishwa na Yeye. Kipengele hiki cha ukweli ni siri ya kina zaidi, ni ngumu kuelewa. Yafupishe maneno ambayo Mungu anasema juu ya siri ya kupata mwili, yaangalie kutoka pembe mbalimbali, kisha yajadili mambo haya miongoni mwenu. Unaweza kuomba, na kutafakari na kujadiliana sana kuhusu mambo haya. Labda Roho Mtakatifu huwaangazia na kukuwezesha kuyaelewa. Hii ni kwa sababu huna nafasi ya kuwasiliana na Mungu, na lazima utegemee uzoefu kwa njia hii ili kuihisi njia yako kidogo kidogo, ili kufikia ufahamu wa kweli wa Mungu.
Ukweli kuhusu kumjua Kristo na kumjua Mungu Mwenyewe ni wa kina zaidi. Ikiwa watu huweka mkazo juu ya kutafuta kipengele hiki cha ukweli, hata hivyo, ndani yao watakuwa waangavu na thabiti, na watakuwa na njia ya kutembea. Kipengele hiki cha ukweli kinafanana sana na moyo wa mwanadamu. Ikiwa mtu hana ukweli katika kipengele hiki, atakosa nguvu. Kadri mtu alivyo na maarifa zaidi ya kipengele hiki cha ukweli, ndivyo alivyo na nguvu zaidi. Sasa kuna watu wengine ambao husema: Katika uchambuzi wa mwisho, kupata mwili ni nini? Semi hizi zinaweza kuthibitisha kwamba Yeye ni Mungu mwenye mwili? Je! Maneno haya yanaweza kuthibitisha kwamba Yeye ni Mungu Mwenyewe? Ikiwa Hangesema maneno haya bado Angekuwa Mungu Mwenyewe? Au kama Angekuwa Amesema tu baadhi ya maneno, Angeweza kuwa Mungu bado? Ni nini kinachoamua kwamba Yeye ni Mungu? Je, inaamuliwa tu kwa maneno haya? Hili ni swali muhimu. Watu wengine hutambua maneno haya kwa njia visivyo sahihi kama agizo la Roho Mtakatifu, kwamba Alimaliza kutoa maagizo na kuondoka, kwamba Roho Mtakatifu aliacha kufanya kazi, kwamba mwili huu si zaidi ya mwili wa kawaida na mwili wa nyama, kwamba mwili huu hauwezi kuitwa Mungu, badala yake Anaweza kuitwa Mwana wa Adamu, na hawezi kuitwa Mungu. Watu wengine wanaielewa visivyo kwa njia hii. Basi, asili ya kutoelewa huku iko wapi? Ni kwamba watu hawajaelewa kupata mwili vizuri kabisa, na hawajafukua kwa undani. Watu wanaelewa kupata mwili kwa juu juu sana, na wanao ufahamu wa ujuzi kidogo tu. Ikiwa kusema maneno mengi ni sawa na Kwake kuwa Mungu, basi kusema maneno machache tu, badala ya mengi, pia kunamaanisha kwamba yeye ni Mungu? Kwa kweli kusema Kwake maneno machache pia ni maonyesho ya uungu. Je! Yeye ni Mungu? Kazi ambayo Mungu hufanya ina umuhimu mkubwa. Imeishinda mioyo ya wanadamu na kulipata kundi la watu. Je, kazi hiyo haingekuwa imemalizika, ingewezekana kumjua Yeye kama Mungu Mwenyewe? Hapo awali kulikuwa na watu ambao, wakati kazi ilikuwa imefanyika nusu, walifikiri hivi: Kama ninavyoona, kazi hii inapaswa kubadilika. Nani anayeweza kusema kupata mwili kweli ni nini! Je! Huku ni kuwa na mtazamo wa kutoamini kuhusiana na kupata mwili kwa Mungu? Kwamba unaweza kuwa na shaka kuhusu kupata mwili kwa Mungu kunaonyesha kwamba huamini katika kupata mwili, huamini kwamba Yeye ni Mungu, huamini kwamba Ana dutu ya Mungu, na huamini kwamba maneno Aliyosema yametoka kwa Mungu. Hata zaidi huamini kwamba maneno Aliyosema ni ufunuo wa tabia Yake Mwenyewe, na maonyesho ya dutu Yake. Watu wengine walizungumza kwa njia hii: Kama ninavyoona, njia ya Mungu ya kufanya kazi inapaswa kubadilika. Haijulikani kupata mwili ni nini hasa, na labda lazima kuwe na ufafanuzi mwingine kuuhusu. Kuna baadhi ya watu ambao husubiri na kuona, kuona kama kuna sauti yoyote kwa maneno yaliyonenwa na Mungu mwenye mwili Anayeketi pale, iwapo Anasema ukweli, na kama amesema chochote kipya. Ningekuwa na mashine ya eksirei ningeangalia na kuona ikiwa kuna ukweli wowote ndani ya tumbo Lake. Ikiwa hakuna ukweli, na kama Yeye ni mtu, basi nitatoroka kwa haraka, na sitaamini. Ningeangalia na kuona ikiwa Roho wa Mungu anafanya kazi ndani Yake, ikiwa Roho wa Mungu anamsaidia, na kumwongoza katika usemi Wake. Watu wengine wanashuku kwa njia hii, na daima wana wasiwasi kuhusu shida hii katika mioyo yao. Hali hii ipo kwa sababu gani? Si kwa sababu nyingine yoyote ila utambuzi wa juu juu ndani ya mwili. Hawaujui kikamilifu, na hawajafikia kiwango cha juu katika ufahamu wao. Kwa sasa, wanakubali tu kwamba mtu huyu ana Roho wa Mungu. Kusema, hata hivyo, kwamba ndani Yake kuna dutu ya Mungu, tabia ya Mungu, na kusema kwamba Yeye ana kile Mungu alicho na kile Alicho nacho, Ana Mungu mzima, na kusema kwamba Yeye si mwingine ila ni Mungu, ni vigumu kwa watu wengine kuelewa kikamilifu. Maneno hayanaonekani kufanana na mtu katika mambo kadhaa. Kile wanachoona watu na kile wanachoamini sio dutu ya Mungu. Kwa maneno mengine, kile watu wanachoona ni maneno hayo tu na kazi halisi. Watu hufikiri tu kwamba Mungu alifanya sehemu ya kazi, kwamba Mungu mwenye mwili Anaweza tu kufanya sehemu hii ya kazi. Hakuna mtu hata mmoja anayeamini kwamba ingawa kupata mwili sasa kunaonyesha sehemu hii ya kazi, Ana asili yote ya uungu. Hakuna mtu anayefikiria kwa njia hii. Sasa baadhi ya watu husema: "Kumjua Mungu mwenye mwili ni kugumu sana. Ingekuwa ni Roho wa Mungu anayefanya kazi moja kwa moja tungeweza kuelewa kwa urahisi. Tungeweza kuona moja kwa moja nguvu za Mungu na mamlaka ya Mungu katika kazi ya Roho. Kisha ingekuwa rahisi kumjua Mungu. "Je, neno hili linafaa? Sasa Nawauliza swali hivi: "Ni rahisi kumjua Mungu mwenye mwili au ni rahisi kumjua Roho? Ikiwa Mungu mwenye mwili Alifanya kazi kama Yehova, ni yupi Angekuwa rahisi kumwelewa? "Unaweza kusema Wao wote ni Wagumu kuelewa. Kama kungekuwa na njia, Wote wawili wangekuwa rahisi kuelewa. Kama hakungekuwa na ufahamu wa kiroho, wote wawili wangekuwa wagumu kuelewa. Je! Watu pia hawakuelewa kazi na maneno ya kupata mwili mwanzoni? Je! Wote waliyaelewa visivyo? Watu hawakujua kile ambacho Mungu alikuwa Anafanya; hakuna kitu kilichofanana na mawazo ya watu! Je! Watu wote waliibuka na mawazo? Hii inaonyesha kuwa watu hawamjui Mungu mwenye mwili kwa urahisi. Ni vigumu kama kumjua Roho, kwa sababu kazi ya kupata mwili ni maonyesho ya Roho, ni kwamba tu watu wanaweza kuona na kugusa kupata mwili. Ni nini maana ya ndani ya kupata mwili, hata hivyo, na ni nini kusudi la kazi Yake, inamaanisha nini, ni vipengele gani vya tabia Yake inavyowakilisha, na kwa nini Amefunuliwa kwa njia hii, watu huenda hawaelewi, sivyo? Kwamba huelewi inaonyesha kwamba hujui. Roho alikuja kufanya kazi, kusema seti ya maneno, na kisha Akaondoka. Kile ambacho watu wanafanya ni kuyatii na kuyafanya tu, lakini watu wanajua kwa kweli ni nini? Je! Watu wanaweza kujua tabia ya Yehova kutoka kwa maneno haya? Watu wengine husema kwamba Roho ni rahisi kumjua, kwamba Roho alikuja kufanya kazi Akibeba umbo la kweli la Mungu. Je, Yeye ni mgumu kumjua kivipi? Hakika unaijua picha Yake ya nje, lakini unaweza kujua kiini cha Mungu? Sasa Mungu mwenye mwili ni mtu wa kawaida ambaye unahisi ni rahisi kuwasiliana naye. Hata hivyo, wakati asili Yake na tabia Yake vinavyoonyeshwa, watu wanajua mambo hayo kwa urahisi? Je! Watu hukubali kwa urahisi maneno yale ambayo Alisema ambayo hayalingani na mawazo yao? Sasa watu wote wanasema kuwa kumjua Mungu mwenye mwili ni vigumu. Ikiwa Mungu baadaye Angegeuzwa, basi ingekuwa rahisi sana kumjua Mungu. Watu ambao husema hili huweka wajibu wote juu ya Mungu mwenye mwili. Je! Hiyo ndivyo ilivyo kwa kweli? Hata kama Roho angewasili hungeweza kumjua vile vile. Roho aliondoka mara tu baada ya kumaliza kuzungumza na watu, na hakuwaeleza mambo mengi sana, na hakushiriki na kuishi nao kwa njia ya kawaida. Watu hawakuwa na nafasi ya kumjua Mungu kwa namna ya utendaji zaidi. Faida ya kazi ya Mungu mwenye mwili kwa watu ni kubwa sana. Ukweli ambao huwaletea watu ni wa utendaji zaidi. Unawasaidia watu kumwona Mungu wa utendaji Mwenyewe. Hata hivyo, kujua kiini cha kupata mwili na kiini cha Roho ni vigumu vile vile. Hivi pia ni vigumu kujua.
Kumjua Mungu kunamaanisha nini? Kunamaanisha kwamba mtu anajua upeo wa hisia za Mungu, hii ndiyo maana ya kumjua Mungu. Unasema kwamba umemwona Mungu, ilhali huelewi upeo wa hisia za Mungu, huelewi tabia Yake, na wala hujui haki Yake. Huna ufahamu wa rehema Zake, wala hujui Anachokichukia. Hili haliwezi kuitwa ufahamu wa Mungu. Kwa hivyo, watu wengine wanaweza kumfuata Mungu, lakini hawamwamini Mungu hasa. Hii ndiyo tofauti. Ikiwa unamjua, unamwelewa, ikiwa unaweza kuelewa na kushika baadhi ya kile mapenzi Yake ni, na unaujua moyo Wake, basi unaweza kumwamini kwa kweli, unaweza kujisalimisha Kwake kwa kweli, kumpenda kwa kweli, na kumwabudu Yeye kwa kweli. Ikiwa huelewi mambo haya, basi unafuata tu, mtu anayefuata tu na kufuata umati. Hiyo haiwezi kuitwa kujisalimisha kwa kweli, na haiwezi kuitwa ibada ya kweli. Je! Ibada ya kweli inaweza kuzalishwaje? Hakuna watu wowote wanaomwona Mungu na kumjua Mungu ambao hawamwabudu Yeye, ambaye hawamheshimu. Mara tu wanapomwona Mungu wanaogopa. Kwa sasa watu wako katika wakati wa kazi ya Mungu mwenye mwili. Kadri watu wanavyokuwa na ufahamu wa tabia ya Mungu mwenye mwili na wa kile Alicho nacho na kile Alicho, ndivyo watu wengi watakavyovithamini, na ndivyo watakavyomheshimu Mungu. Mara nyingi, ufahamu mdogo unamaanisha kutokuwa waangalifu zaidi, kiasi kwamba Mungu anachukuliwa kama mwanadamu. Watu wataogopa na kutetemeka ikiwa wanamjua Mungu kwa kweli na kumwona kwa hakika. Kwa nini Yohana alisema, "Yeye anayekuja baada yangu, ambaye mimi sistahili kubeba viatu vyake"? Ijapokuwa ufahamu wake ndani ya moyo wake haukuwa wa kina kirefu sana, lakini alijua kwamba Mungu ni wa ajabu. Ni watu wangapi wanaoweza kumcha Mungu sasa? Bila kuijua tabia ya Mungu, mtu anawezaje kumheshimu? Ikiwa watu hawajui kiini cha Kristo, na hawaelewi tabia ya Mungu, hawawezi hata kumwabudu Mungu kwa kweli. Ikiwa watu wanaona tu kuonekana kwa nje kwa kawaida kwa Kristo na hawajui asili Yake, ni rahisi kwa watu kumchukulia Kristo kama mtu wa kawaida. Wanaweza kuchukua mtazamo usio wa heshima Kwake, wanaweza kumdanganya, kumkataa, kutomtii, kutoa hukumu Kwake, na kuwa na maoni. Wanaweza kuchukua neno Lake kama lisilo na maana, wanaweza kuutendea mwili Wake kama wanavyotaka, wanaweza kuwa na mawazo, na wanaweza kukufuru. Ili kutatua masuala haya mtu lazima ajue kiini cha Kristo, uungu wa Kristo. Hiki ndicho kipengele kikuu cha kumjua Mungu; ndicho watu wote wanaoamini katika Mungu wa utendaji wanapaswa kuingia na kufanikisha.
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo
Yaliyopendekezwa: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni