6/20/2018

Matokeo ya Mwisho Ambayo Kazi ya Mungu Inalenga Kufanikisha

Katika nyingi ya kazi ya Mungu,
mtu yeyote aliye na uzoefu wa kweli anahisi uchaji na heshima Kwake,
ambayo ni zaidi ya sifa.
Hukumu Yake na kuadibu
vinawafanya watu waone tabia Yake,
na kumcha katika mioyo yao.
Mungu ni wa kuchiwa na kutiiwa,
kwa sababu nafsi Yake na tabia Yake ni tofauti na vitu vilivyoumbwa,
ni kuu kuliko vitu vilivyoumbwa.
Ni Mungu tu Anayestahili uchaji na utiifu.
Wale waliopitia kazi ya Mungu, walio na ufahamu wa kweli kumhusu,
wote wanahisi heshima Kwake.
Wale wanaoshikilia mawazo yao dhidi ya Mungu
na wasiomchukulia kama Mungu hawamchi,
hawajashindwa ingawa wanamfuata.
Hawana utiifu kiasili.
Kazi ya Mungu ya aina hii ni kufanikisha hili:
Vitu vyote vilivyoumbwa vinamcha Muumba.
Vyote vinaweza kumwabudu Mungu na kumtii katika utawala Wake bila masharti.
kwa sababu nafsi Yake na tabia Yake ni tofauti na vitu vilivyoumbwa,
ni kuu kuliko vitu vilivyoumbwa.
Ni Mungu tu Anayestahili uchaji na utiifu.
Haya ndiyo kazi Yake itafanikisha mwishowe.
Kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili
Sikiliza nyimbo: Msifuni Mwenyezi Mungu 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni