7/14/2018

Nyimbo za Mungu | Nitakubali Uishi Moyoni Mwangu Wakati Wote🎼🎹

Unaandamana nami katika misimu minne.
Nikitazama uso Wako wenye upweke, mawimbi ya huzuni yanajaa moyoni mwangu.
Sijawahi kubembeleza huzuni Wako na sikujali kamwe kuhusu upweke Wako;
nikikumbana na maneno Yako ya bidii tena na tena, mimi ni mkaidi sana.
Kila wakati kuumiza moyo Wako na kila wakati kukufadhaisha Wewe;
baada tu ya kupata kuadibiwa ndipo nagundua kidogo.
Ingawa niko upande Wako, siwezi kubeba mzigo kwa ajili Yako.
Sina akili, sielewi ugumu Wako kabisa.
Kwa tamaa na mwili, nilisahau ukweli na maadili.
Nikijawa na majuto, nimeufadhaisha moyo Wako kwa kitambo kirefu.
Siwezi hata kuhisi huzuni kwa uchungu wa maumivu Yako.
Nikitoa sauti kwa uchungu katika upotovu, nikinyoosha mkono wangu wa ulafi kuomba.
Nani ako na dhamiri na akili kugawa masumbuko Yako kidogo?
Moyo Wako ni wenye ukarimu sana, upendo ni wa thamani na kweli.
Nani anaweza kuwa mzuri zaidi na mwenye heshima kuliko Wewe!
Nitakuwa na Wewe milele, na kamwe sitaondoka upande Wako.
Nitakuwa na Wewe milele, na kamwe sitaondoka upande Wako.
Moyo Wako ni wenye ukarimu sana, upendo ni wa thamani na kweli.
Nani anaweza kuwa mzuri zaidi na mwenye heshima kuliko Wewe!
Nitakuwa na Wewe milele, na kamwe sitaondoka upande Wako.
Nitakuwa na Wewe milele, na kamwe sitaondoka upande Wako.
Acha uchangamfu na raha vionekane usoni Mwako,
acha Uishi moyoni mwangu wakati wote.
Acha uchangamfu na raha vionekane usoni Mwako,
acha Uishi moyoni mwangu wakati wote,
ishi moyoni mwangu wakati wote.
kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya 
Sikiliza zaidi: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu, Chanzo cha Mafanikio ya Umeme wa Mashariki 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni