9/03/2018

Mfuate Mungu Katika Njia Yenye Mabonde

Kila ambacho nimewahi kuwa nacho, mimi hukitumia kwa Mungu.
Kila nilicho nacho nakitoa; najitoa mwenyewe Kwake.
Familia imenitelekeza; nimekashifiwa na dunia.
Basi, njia ya kumfuata Mungu ina mabonde, imejaa na mawe na miiba.
Nilitoa kila kitu changu ili kueneza ufalme wa Mungu mbali.
Nimeona misimu ikija na kuenda.
Najua kilicho mbele, huzuni ama furaha.
Mungu anafaa tu kuuliza na nitatii.
Katika njia ya kumpenda Mungu, nakumbana na majaribu machungu.
Hatari na dhiki, nakumbana navyo bila malalamishi.
Ingawa mwili wangu unaumia sana, Mungu ndiye ambaye moyo wangu unampenda.
Nitaenda kutembea kila mahali, kushuhudia yote ambayo Mungu ametenda.
Mateso na majaribu yananilemeza.
Katika mema na mabaya, nimeishi.
Bado, nitafanya mapenzi ya Mungu, nimpe Yeye yote niliyo nayo,
niteseke maisha yangu yote kwa ajili ya Mungu.
Mateso na majaribu yananilemeza.
Katika mema na mabaya, nimeishi.
Bado, nitafanya mapenzi ya Mungu, nimpe Yeye yote niliyo nayo,
niteseke maisha yangu yote kwa ajili ya Mungu, niteseke maisha yangu yote kwa ajili ya Mungu.
kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Sikiliza zaidi: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu, Chanzo cha Mafanikio ya Umeme wa Mashariki  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni