12/14/2018

Nyimbo za kanisa | Kanuni za Kutafuta Njia ya Kweli

Nyimbo za kanisa | Kanuni za Kutafuta Njia ya Kweli

I
Ni kanuni gani za msingi zinazoonyesha njia ya kweli?
Ona kama Roho anafanya kazi, kwa ukweli unaonyeshwa;
ona ni nani anayeshuhudiwa, na anakuletea nini.
Kwani imani kwa Mungu inamaanisha imani kwa Roho wa Mungu.
Imani katika Mungu mwenye mwili ni imani katika ukweli kwamba
Yeye ni mfano halisi wa Roho wa Mungu,
Yeye ni Roho wa Mungu ambaye anachukua umbo la mwili,
Yeye ni Neno ambalo sasa limekuwa mwili.
II
Unafaa kuona pia kama ukweli upo katika njia hii.
Ukweli, ambao ni tabia ya kawaida ya mwanadamu,
mawazo ya kawaida, mtazamo, hekima, na maarifa ya msingi ya kuwa mwanadamu.
Ukweli, ambao Mungu aliazimia kwa mwanadamu kitambo wakati wa uumbaji.
Je, njia hii inaelekea kwa maisha ya kawaida?
Je, ukweli wake unamhitaji mwanadamu kuishi ubinadamu wa kawaida?
Je, ni jambo la utendaji, ni la wakati unaofaa?
Kama kuna ukweli katika njia hii, uzoefu wa mwanadamu utakuwa wa kweli,
ubinadamu wao na akili vitakuwa kamili,
maisha yao ya kiroho na maisha yao katika mwili yatakuwa na mpangilio zaidi,
hisia zao zitakuwa za kawaida zaidi.
III
Sasa kuna sheria moja zaidi ya wewe kujua njia ya kweli.
Je, njia hii inamsaidia mwanadamu kua katika maarifa yake ya Mungu, katika maarifa yake ya Mungu?
Ukweli unafaa kutia msukumo wa upendo kwa Mungu katika moyo wa mwanadamu
na unapasa kumleta mwanadamu karibu zaidi na uwepo Wake.
Ukweli unaleta uhalisi, unatoa mahitaji kwa maisha.
Tafuta kanuni hizi, kisha utafute njia ambayo ni ya kweli,
tafuta njia iliyo ya kweli, tafuta njia iliyo ya kweli.
kutoka katika "Ni Wale tu Wanaomjua Mungu na Kazi Yake Ndio Wanaoweza Kumridhisha Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwil
Sikiliza nyimbo: Nyimbo za injiliKuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni