12/16/2018

Maneno ya Mungu Huniongoza Kujifunza Jinsi ya Kufundisha Watoto Wangu (II)


Maneno ya Mungu Huniongoza Kujifunza Jinsi ya Kufundisha Watoto Wangu (II)

Xiaoxue, Malesia
Siku moja baada ya mlo mkuu wa siku, nilimfundisha mwanangu mvulana mkubwa jinsi ya kusoma Kichina—maneno rahisi tu, “Mbinguni, dunia, watu, na, dunia, baba, mama….” Nilimfundisha mara chache hasa, lakini bado hakuweza kuandika. Angeandika neno la kwanza na kisha kusahau lililofuata. Hasira ndani yangu ilipanda, na kunyakua rula iliyokuwa juu ya meza na kumgonga mara kadhaa. Nilimpigia kelele kwa sauti kubwa: “Wewe ni mpumbavu jinsi gani! Huwezi hata kujifunza maneno haya machache!” Mwanangu mkubwa alipigwa mpaka akalia, “waa, waa” na kutoroka na kukimbia kusimama pembeni. Nikamkemea, “Njoo hapa na uendelee kuandika!” Mwanangu mkubwa hakuja, hivyo nikamnyakua na kumvuta kwa kiti. Baada ya kuona kwamba mkono wa mwanangu mkubwa ulikuwa amepigwa vibaya na ilikuwa umevimba, nilihisi maumivu makali moyoni mwangu. Nililia na kurudi kwa chumba changu na nikamwomba Mungu: “Mungu! Mara tu mtoto wangu aliponikasirisha, sikuweza kuidhibiti hasira yangu. Sitaki kuwatendea wanangu jinsi hii. Mungu, tafadhali Unisaidie.” Baada ya kuomba, nilitulia polepole.
Baadaye, nilimfundisha kama kawaida, lakini bado hakujifunza. Nilikumbuka kumwomba Mungu na sikukasirika tena. Wakati huo huo, nilianza kujitafakaria. Kwa nini sikuweza kudhibiti hasira yangu wakati mwanangu hakunifurahisha? Nilipokuwa nikiwaza hili, nilifikiria kifungu kimoja cha maneno ya Mungu: “Mara tu binadamu anapokuwa na hadhi, mara nyingi atapata ugumu wa kudhibiti hali ya moyo wake, na kwa hivyo atafurahia kutumia nafasi mbalimbali kueleza kutotosheka kwake na kutoa nje hisia zake; mara nyingi atawaka kwa hasira kali bila sababu yoyote, ili kuonyesha uwezo wake na kuwafanya wengine kujua kwamba hadhi yake na utambulisho wake ni tofauti na ule wa watu wa kawaida. Bila shaka, watu waliopotoka wasiokuwa na hadhi yoyote mara kwa mara pia watapoteza udhibiti wao. Ghadhabu yao mara nyingi husababishwa na uharibifu wa manufaa yao ya kibinafsi. Ili kulinda hadhi yake binafsi na heshima, mwanadamu aliyepotoka mara kwa mara atatoa nje hisia zake na kufichua asili yake yenye kiburi” (“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Baadhi yao huendeleza hali ya kuzuia ghadhabu yao, huku nao wengine wanakimbilia na wanapandwa na hasira kali kila wanapopenda bila ya hata kiwango kidogo zaidi cha kujizuia. Kwa ufupi, ghadhabu ya binadamu inatokana na tabia yake iliyopotoka. Haijalishi kusudi lake, ni la mwili na ni la asili; halina uhusiano wowote na haki au ukiukaji wa haki kwa sababu hakuna kitu katika asili ya binadamu na hali halisi vinavyolingana na ukweli” (“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kupitia kile maneno ya Mungu yalichofichua, niliona kuwa nilikuwa nimepotoshwa kwa kina mno na Shetani na pia nilikuwa na kiburi mno na mjeuri, daima nikiwakandamiza na kuwalazimisha wanangu katika utambulisho wangu na hadhi kama mama yao na mara tu walipokosa kutimiza matakwa na vipimo vyangu, sikuweza kujizuia kuwa na hasira na kuwakaripia na kuwaadhibu kimwili. Kwa kweli sikuwa na sababu kamwe. Si sababu ya kuwa na hasira sana na mwanangu ni kwa kuwa matokeo yake kutoka kufanya mtihani wa kuingia shule yalikuwa mabaya zaidi ya yale ya watoto wote? Hili lilinifanya kuaibika mbele ya wengine. “Kumtendea mtoto wangu kwa ukali sana na kutozijali hisia zake leo sio yote kwa manufaa yake mwenyewe au kumfanya aendeleze haraka utendaji wake wa kitaaluma, lakini kufurahisha majivuno yangu mwenyewe na hamu ya hadhi. Mimi ni wa ubinafsi mno na mwenye kustahili dharau! Ni kwa sababu ya tabia yangu ya kiburi, ya ubinafsi na potovu ndio siwezi kumtii Mungu na daima mimi hutaka kutoroka kutoka kwa ujuzi na mipango ya Mungu na ninataka kuwapangia wanangu kila kitu kwa kutegemeza uwezo wangu na hatimaye kujiletea mimi na wanangu maumivu mengi.” Nilipofikiria hili, nilijichukia na sikuwa na hamu tena ya kuishi kulingana na tabia potovu ya Shetani na kupumbazwa na Shetani. Kwa hiyo nilimwomba Mungu na kumtaka Mungu auweke moyo wangu, kuniongoza kupitia maneno Yake, na kupanga mazingira hata zaidi ya kunibadilisha na kunitakasa. Baadaye, sikuhitaji mengi mno kutoka kwa mwanangu. Badala yake, nilimfunza kwa uvumilivu na kufanya kadri nilivyoweza kuwa mama. Polepole, sikuwa na wasiwasi tena kwa sababu wanangu hawakujifunza, na nilihisi kuburudika hasa na kufurahi. Nilipowatazama wanangu wawili tena, nilitambua kwamba walikuwa wazuri sana na wachangamfu, na nikagundua wakati huo jinsi ilivyokuwa bila haki kwa wanangu wakati nilipowafanya daima waishi kulingana na njia yangu na kukua katika picha ya kipeo sanifu katika mawazo yangu.
Baadaye, kile kilichonishangaza ni kwamba wanangu walianza kubadilika. Awali hawakuwa na umakinifu wowote katika masomo yao na hawakuweza kukaa vizuri wakati wa kufanya kazi zao za nyumbani, wakijibwaga juu ya meza na kutaka kucheza baada ya kuandika maneno machache. Sasa kwa kweli waliweza kukaa chini na kufanya kazi zao za nyumbani kwa bidii. Kwa siku chache zilizopita, mwanangu mkubwa alikuwa hawezi kujifunza herufi za Kichina nilizomfundisha mara nyingi, lakini sasa alizikumbukia baada ya mimi kuzisema mara moja au mbili tu na aliweza kusoma herufi nne au tano pamoja. Hili kwa kweli lilinishangaa; la kutotarajia zaidi, ilhali awali wanangu wawili mara nyingi walipigana wakati walipokuwa pamoja, sasa hatimaye walikuwa na tabia nzuri na hawakupigana tena. Mwanangu mkubwa hata alimpa ndugu yake mdogo kwa utendaji vitu alivyovipenda. Mume wangu alipoona mabadiliko ya wana wetu, aliniuliza kwa mshangao jinsi nilivyokuwa nimewafundisha watoto wetu na kwa nini walikuwa werevu na wenye hekima ghafla. Nikajiwazia: Hili linawezaje kuwa ndilo nililowafundisha? Hili ni tendo la ajabu la Mungu!
Baada ya kupitia hili, nilitulia na kutafakari juu ya njia zangu za awali za kuwafundisha wanangu. Daima nilikuwa nimewafundisha na kuwadhibiti wanangu kutoka kwa nafasi yangu kama mama, kuwafanya wanisikilize na kufanya kile nilichokisema. Nilidhani kwamba hii ndiyo iliyokuwa njia ya kuwafundisha watoto vizuri. Kwa kweli, nilipowafundisha wanangu kwa njia hii, hawakukosa tu kufaulu, lakini kwa kweli walikuwa na upinzani zaidi na zaidi. Lakini nilipoukana mwili wangu na kuacha kuishi kulingana na tabia ya shetani ya ubinafsi, ya kiburi na nikawa tayari kuyatii mamlaka na mipango ya Mungu, kuwakabidhi wanangu kwa Mungu na kutimiza wajibu wangu na majukumu yangu kama mama, wanangu waligeuka kuwa watiifu na wenye hekima. Sasa ninaelewa kwamba ni Mungu pekee aliye na mamlaka na nguvu na kwamba ni maneno ya Mungu tu yanayoweza kuwabadilisha watu na kutufanya tuishi maisha yetu kwa kudhihirisha mfano wa wanadamu halisi. Kwa hiyo nitamtukuza Mungu na kumruhusu Mungu atawale katika nyumba yetu. Kama inavyosemwa katika ushirika na mahubiri: “Unapomleta Mungu katika maisha yako halisi, jambo la kwanza ni kumleta Mungu katika maisha yako ya nyumbani. Katika maisha yako ya nyumbani, kama watu walikuwa wakiisimamia familia yako, basi ni lazima uwaondoe kwa cheo chao. Lazima uziondoe sanamu zote, uyafanye maneno ya Mungu yawe bwana wa nyumba yako, na umruhusu Kristo kutawala. Mume na mke, baba na mtoto, mama na binti—wote ni lazima wasome na kuwasiliana kwa karibu maneno ya Mungu pamoja. Kama kuna matatizo yoyote au kutofautiana, haya yanaweza kutatuliwa kwa njia ya sala, kusoma maneno ya Mungu, na kuwasiliana ukweli kwa karibu. Usifanye kama ulivyozoea kufanya, kumsikiliza mtu fulani. Watu hawafai kufanya kama watu wengine wanavyosema, wanafaa kumtukuza Kristo, na kuyaruhusu maneno ya Kristo kuzitawala familia zao, kuyaruhusu maneno ya Mungu kuchukua madaraka katika nyumba yao. Si huku ni kuleta maneno ya Mungu katika maisha yako halisi?” (ushirika kutoka hapo juu).
Kwa hiyo, nikawaambia wanangu: “Kuanzia leo kwendelea, mama hatakasirika bila busara au kuwapiga tena. Mkifanya makosa, mama atawaambia kwa uvumilivu na mama akifanya makosa, mama atawaomba msamaha. Hebu tujifunze neno la Mungu pamoja na kukua pamoja katika maneno ya Mungu na si kufanya mambo ambayo Mungu hayapendi, sawa?” Wanangu wakasema kwa furaha: “Sawa!” Baadaye, sikutenda tena nikitumia hadhi yangu kama mama yao kuwakandamiza. Tulipokabiliwa na masuala fulani, sote tulimheshimu Mungu kama mkuu na kumruhusu Kristo atawale nyumbani mwetu. Wakati mwingine nilizungumza nao kwa sauti kubwa na waliniambia: “Mama, Mungu hatakupenda unapokuwa jinsi hii.” Walipofanya kitu kibaya, mimi pia ningewaelezea sababu na kuwaambia jinsi Mungu anavyopenda tutende na kila wakati walisikiliza kwa makini. Polepole, uhusiano wangu na wanangu ukawa wa karibu zaidi na zaidi. Daima niliwasomea maneno ya Mungu na kusikiliza nyimbo za neno la Mungu pamoja nao. Waliporudi kutoka shuleni awali, daima walikuwa wakiangalia katuni kama vile “Robot” kwa kompyuta ya iPad. Siku hizi, mara nyingi wanangu huniambia: “Mama, tutaangalia kompyuta ya iPad kwa muda, lakini hatutaangalia kile usichokipenda. Je, tunaweza kutazama video za nyimbo za neno la Mungu?” Kisha wanazitazama kimya kimya, na wakati mwingine wanaweza kuzitazama kwa zaidi ya saa moja.
Shukrani ziwe kwa Mwenyezi Mungu kwa kuyabadilisha maisha yangu na ya wanangu kwa maneno Yake! Katika siku za nyuma nilikuwa asiyejua na mjinga na niliwafundisha wanangu nidhamu kwa kutegemeza asili yangu ya kiburi. Sikujua kuwaleta wanangu mbele ya Mungu na kwa hivyo jinsi nilivyozidi kuwafundisha nidhamu ndivyo walivyoasi zaidi. Sasa ninaelewa kuwa ni maneno ya Mungu pekee yanayoweza kutubadilisha na kutufanya tuishi kwa kudhihirisha mfano wa mtu halisi. Kuanzia sasa kwendelea, nitajifunza kulitukuza neno la Mungu na kuwashawishi watoto kumwamini na kumfuata Mungu. Utukufu wote ni wa Mwenyezi Mungu!
kutoka katika Ushuhuda wa Injili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni