1/20/2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 39

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 39 

        Fungua macho yako na uangalie na unaweza kuona nguvu Zangu kuu kila mahali! Unaweza kuwa na uhakika na Mimi kila mahali. Ulimwengu na anga unaeneza nguvu Zangu kuu. Maneno ambayo Nimenena yametimia katika ongezeko la joto la hali ya hewa, mabadiliko ya hali ya hewa, vioja vya watu, ulemavu wa elimumwendo ya kijamii, na udanganyifu wa mioyo ya watu. Jua linakuwa jeupe na mwezi unakuwa mwekundu; Yote yako katika machafuko. Je, bado huoni haya?
Nguvu kuu ya Mungu inafichuliwa katika haya. Bila shaka Yeye ni Mungu mmoja wa kweli—Mwenyezi—ambaye watu wamemwandama kwa miaka mingi! Nani anaweza kuzungumza kwanza na kisha mambo asababishe mambo kutokea? Mwenyezi Mungu wetu pekee. Ukweli huonekana mara tu Anaponena. Unawezaje kukosa kusema kwamba Yeye ni Mungu wa kweli?
Najua moyoni kwamba ninyi nyote mko tayari kushirikiana na Mimi na Ninaamini kwamba wateule Wangu, ndugu Zangu wapendwa wote wana matarajio ya aina hii, lakini hamwezi tu kuingia au kutenda kwa kweli, hamwezi kusalia watulivu na wanyamavu mnapokabiliwa na tukio la hali halisi. Hamyajali kamwe makusudi ya Mungu, na mnaweka maslahi yenu wenyewe kwanza na kuja mbele kwanza. Hebu Niwaambie, njia hii haitaridhisha nia Zangu kamwe! Mwana! Nipe tu moyo wako kabisa. Kuwa wazi! Sitaki fedha zako au vitu vyako wala Sitaki uje mbele Yangu kunitumikia kwa bidii, kwa udanganyifu au kwa akili finyu. Kuwa mtulivu na mwenye moyo safi, subiri na utafute matatizo yanapotokea, nami Nitakupa jibu. Usiwe na shaka! Kwa nini huamini kamwe maneno Yangu kuwa ya kweli? Kwa nini huwezi kuamini katika maneno Yangu? Mkaidi kwa kiwango na bado uko namna hii wakati huu, wewe ni mjinga sana na hujapata nuru hata kidogo! Je, ni kiasi gani cha ukweli muhimu ambacho unakumbuka? Je, umeupitia kweli? Unatatanishwa na kutenda kiholela na kwa haraka unapokumbana na matatizo! Jambo kuu leo ni kwamba mwingie katika roho na kuwasiliana na Mimi zaidi, kama kwamba mara kwa mara mioyo yenu wenyewe hufikiri kuhusu tatizo fulani. Je, mnaelewa? Hili ni muhimu! Kutenda kulikochelewa kwa kweli ni tatizo. Harakisheni, msichelewe! Watu wanaosikia maneno Yangu na wasichelewe bali wayatende mara moja watabarikiwa sana! Nitawapa maradufu! Msiwe na wasiwasi! Fanya kama Ninavyosema, bila kuchelewa hata sekunde! Dhana zenu za kibinadamu mara nyingi huwa hivyo, na ninyi ni wenye kuahirisha mambo, daima mkichelewesha kinachopaswa kufanywa leo hadi kesho. Wavivu na wasio waangalifu. Maneno hayawezi kuelezea! Si kutia chumvi Kwangu bali ni ukweli. Kama huamini hili, basi jichunguze na uiangalie kwa makini hali yako na utagundua kuwa iko hivyo kweli!
kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili
Yaliyopendekezwa : Umeme wa Mashariki Hutoka wapi? Kujua Kanisa la Mwenyezi Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni