2/23/2019

Ni kwa Kufanya Kazi Katika Mwili Pekee Ndiyo Mungu Anaweza Kumpata Binadamu

I
Kupitia katika neno la Mungu wa utendaji,
unyonge wa mwanadamu na uasi yanahukumiwa na kufichuliwa.
Kisha wanadamu wanapokea kile wanachohitaji.
Wanaona kuwa Mungu amekuja katika ulimwengu huu wa binadamu.
Kazi ya Mungu wa utendaji ina nia ya kumwokoa kila mmoja kutoka kwa ushawishi wa Shetani,
kuwaokoa wait kutoka kwa uchafu na tabia iliyopotoshwa na Shetani.
Kupatwa na Mungu kunamaanisha kufuata mfano Wake kama mfano kamili wa mwanadamu.
Mfuate Mungu wa matendo, ishi ubinadamu wa kawaida,
fuata maneno Yake na mahitaji, fuata kile Anachosema kabisa,
na ufanikishe kile Anachotaka, kisha utapatwa na Mungu.
II
Mungu alikuwa mwili, Akiruhusu watu kuona matendo Yake.
Roho Wake alichukua mwili, ili mwanadamu amguse Mungu,
ili watu wamtazame Mungu na kuja kumjua.
Kwa njia hii ya matendo pekee ndiyo Mungu anawafanya watu kuwa wakamilifu.
Wale wanaoweza kuishi maisha yao kulingana na Yeye
na kufuata moyo Wake, ni wale wanaopatwa na Mungu.
Kupatwa na Mungu kunamaanisha kufuata mfano Wake kama mfano kamili wa mwanadamu.
Mfuate Mungu wa matendo, ishi ubinadamu wa kawaida,
fuata maneno Yake na mahitaji, fuata kile Anachosema kabisa,
na ufanikishe kile Anachotaka, kisha utapatwa na Mungu.
III
Kama Mungu angenena tu mbinguni na asije chini duniani,
watu wangewezaje kumjua Yeye?
Na maneno matupu tu kuonyesha kazi Yake, na sio maneno Yake kama ukweli.
Mungu anakuja kama mfano, ili mwanadamu amwone na kumgusa, amwone na kupatwa na Yeye.
Kupatwa na Mungu kunamaanisha kufuata mfano Wake kama mfano kamili wa mwanadamu.
Mfuate Mungu wa matendo, ishi ubinadamu wa kawaida,
fuata maneno Yake na mahitaji, fuata kile Anachosema kabisa,
na ufanikishe kile Anachotaka, kisha utapatwa na Mungu.

kutoka kwa "Unapaswa Kujua kuwa Mungu wa Vitendo ni Mungu Mwenyewe" katika Neno Laonekana katika Mwili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni