2/13/2019

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Sura ya 42

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Sura ya 42

Mwenyezi Mungu alisema, Jinsi gani matendo ya Mwenyezi Mungu yalivyo makuu! Jinsi ilivyo ya ajabu! Jinsi ilivyo ya kushangaza! Tarumbeta saba zinatoa sauti, ngurumo saba zinatolewa, bakuli saba zinamwangwa—hii itadhihirika wazi mara moja na hakuwezi kuwa na shaka. Upendo wa Mungu huja juu yetu kila siku na ni Mwenyezi Mungu pekee Anayeweza kutuokoa; kama tunakabiliwa na bahati mbaya au kupokea baraka ni kwa sababu Yake kabisa, na sisi wanadamu hatuna njia ya kuamua hili. Wale wanaojitolea kwa moyo wote kwa Mungu hakika watapewa baraka nyingi, ilhali wale wanaotafuta kulinda maisha yao watapoteza maisha yao; vitu vyote na mambo yote yamo mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Usisitishe hatua zako tena. Mabadiliko makubwa yanakuja mbinguni na duniani; mwanadamu hana njia ya kujificha na kuna kulia kwa uchungu tu, hakuna chaguo lingine. Fuata kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu, kila mwanadamu anapaswa kuwa dhahiri ndani yake kuhusu hatua ambayo kazi Yake imeendelea, hakuna tena haja ya kukumbushwa na wengine. Sasa njoo mbele ya Mwenyezi Mungu mara nyingi, na umwombe kila kitu. Hakika Atakupa nuru ndani na katika nyakati muhimu Atakulinda. Usiwe na hofu! Tayari Anamiliki nafsi yako yote na kwa ulinzi Wake na huduma Yake, kuna nini cha wewe kuogopa? Leo ufanisi wa mapenzi ya Mungu umekaribia, yeyote anayehofu atapoteza. Sikwambii upumbavu. Fungua macho yako ya kiroho, na mbingu itabadilika papo hapo. Je, kuna nini cha kuhofu? Kwa ishara ya upole ya mkono Wake, mbingu na dunia vinaharibiwa mara moja. Kuna haja gani ya mwanadamu kuwa na wasiwasi? Je, vitu vyote haviko mikononi mwa Mungu? Akisema kwamba mbingu na dunia zinapaswa kubadilika, basi zitabadilika. Akisema kwamba tunapaswa kukamilishwa, basi tutakamilishwa. Hakuna haja ya mwanadamu kuwa na wasiwasi, anapaswa kusogea mbele kwa utulivu. Hata hivyo, anapaswa kuwa msikivu sana na kuwa macho sana. Mbingu inaweza kubadilika ghafla! Macho ya mwanadamu yanaweza kufunguliwa wazi kabisa na bado yasiweze kuona chochote. Kuwa macho haraka, mapenzi ya Mungu yametimizwa, mradi Wake umekamilika, mpango Wake umefanikiwa, wanawe wote wamefika kwenye kiti Chake cha enzi, na wanayahukumu mataifa yote na watu wote pamoja na Mwenyezi Mungu. Wale ambao wamekuwa wakilitesa kanisa, na kuwaumiza wana wa Mungu kikatili, wataadhibiwa vikali, hiyo ni kwa hakika! Wale ambao wanajitoa kwa Mungu kwa dhati, na kuunga mkono kila kitu, hakika Mungu atawapenda milele na milele, bila kubadilika kamwe!
kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni