5/15/2019

Neno la Mungu | Sura ya 59

Tafuta mapenzi Yangu zaidi katika mazingira unayoyakabili na kwa hakika utapata kibali Changu. Ilmradi uwe tayari kwenda katika utafutaji na kuhifadhi moyo ambao unanicha, Mimi Nitakupea yote unayokosa. Kanisa sasa linaingia utendaji rasmi na mambo yote yanaingia kwenye alama sahihi. Mambo hayako yalivyokuwa wakati mlipokuwa na limbuko la mambo yajayo. Lazima msiwe wa kuchanganyikiwa au kuwa bila utambuzi. Ni kwa nini Mimi nahitaji kwamba muingie ndani ya uhalisi katika kila kitu? Je, kweli umelipitia jambo hili? Je, mnaweza kweli kunikidhi Mimi katika kile Ninachohitaji kwenu, kama vile Ninavyowakidhi nyinyi? Usiwe mdanganyifu! Sio zaidi ya stahamala Yangu kwenu tena na tena na bado hamna uwezo wa kujua ni kipi kizuri kwenu tena na tena, na kukosa kuonyesha shukrani!
Haki Yangu, uadhama Wangu, hukumu Yangu na upendo Wangu—mambo yote haya ambacho ni kile Anacho na alicho—je, umeyaonja kwa kweli? Kweli nyinyi ni wapumbavu sana na hamtambui mapenzi Yangu. Mara kwa mara Nimewaambia kwamba karamu Ninazoziandaa lazima zionjwe na nyinyi wenyewe, bado mnakataa hili tena na tena na hamuwezi kutofautisha mazingira mazuri na yale mbaya. Ni gani kati ya mazingira haya yamebuniwa na nyinyi wenyewe? Na ni gani ambayo yamepangwa kwa mikono Yangu? Msijitetee! Ninaona kila kitu kwa dhahiri kabisa na ni tu kwamba usitafute. Nini zaidi Ninaweza sema?
Daima Nitawaridhisha ambao wanatambua mapenzi Yangu na Mimi sitawaruhusu wateseke au wapate madhara. Jambo la muhimu sasa ni kwamba mna uwezo wa kuchukua hatua kwa mujibu wa mapenzi Yangu, na wale ambao wanatenda hili kwa hakika watapokea baraka Zangu na kuwa chini ya ulinzi Wangu. Ni nani kati yenu kwa kweli anaweza kabisa kutumia rasilmali kwa ajili Yangu na kutoa yote yao kwa ajili Yangu? Nyinyi nyote mu shingo—upande, mawazo yenu yanaenda pande zote, yakifikiria juu ya nyumbani, dunia ya nje, chakula na mavazi. Licha ya ukweli kwamba uko mbele Yangu ukifanya mambo kwa ajili Yangu, katika moyo wako bado unafikiria mke, watoto na wazazi wako walio nyumbani-je, haya yote ni mali yako? Mbona usiwakabidhi mikononi Mwangu? Je, hunisadiki vya kutosha? Au ni kwamba unahofia Nitafanya mipango isiyofaa juu yako? Mbona daima wewe hukumbuka kwa hamu nyumbani kwako? Na kukumbuka watu wengine! Je, Ninamiliki nafasi fulani moyoni mwako? Na bado unazungumzia kuhusu kuniruhusu Mimi kutawala ndani yako na kumiliki nafsi yako nzima-haya yote ni uongo mdanganyifu! Ni wangapi kati yenu ambao ni wa kanisa kwa mioyo yenu yote? Na ni nani kati yenu hawafikiri juu yao, lakinii ni wa ufalme wa leo? Fikiria kwa makini sana kuhusu hili.
Mmenisukuma hadi kiasi hiki, hivyo Ninaweza kutumia tu mikono Yangu kuwachochea mbele; Sitawashawishi tena mbele. Hii ni kwa sababu mimi ni Mungu Mwenye hekima, na Mimi huwtendea watu tofauti kwa njia tofauti, kutegemea jinsi ninyi ni waaminifu Kwangu. Mimi ni Mungu Mwenyezi—ni nani anathubutu kuzuia hatua Zangu za mbele? Yeyote anayethubutu kuniasi, mkono wa amri Zangu za utawala kuanzia sasa kuendelea utakuwa milele juu yao, ili kwamba wapate kujua uweza Wangu. Kile Ninahamu nacho sio watu wengi sana, lakini wachache waliochaguliwa. Mimi Nitamuacha na kumwadhibu yeyote ambaye ni muasi, mdanganyifu, yeyote anayejishughulisha katika tabia potovu na ya ulaghai. Usifikirie tena kuwa Mimi ni Mwenye rehema, au kwamba Mimi ni mwenye upendo na mkarimu; hii ni wewe tu ujiendekeza mwenyewe. Najua kuwa Nitakavyokuendekeza zaidi ndivyo zaidi unaendelea kuwa hasi na kutoonyesha hisia zaidi, na hutakuwa tayari kujitoa mwenyewe. Wakati watu ni wagumu kwa kiasi hiki Ninaweza tu kuwachochea wao na kuwalazimisha wao mbele wakati wote. Fahamu hili! Kuanzia sasa Mimi ni Mungu Ambaye Anahukumu; Mimi tena si mwenye rehema, mkarimu na mwenye upendo tena wa ubunifu wa mtu!
Chanzo: Sura ya 59 
Kujua zaidi: Chanzo cha Mafanikio ya Umeme wa Mashariki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni