6/14/2019

Neno la Mungu | Sura ya 88

Watu hawawezi tu kuwaza kiasi ambacho mwendo Wangu umezidisha kasi: Ni ajabu ambayo imetokea isiyoeleweka kwa mwanadamu. Tangu uumbaji wa dunia, mwendo Wangu umeendelea na kazi Yangu haijawahi kusimama. Ulimwengu wote hubadilika siku kwa siku na watu pia wanabadilika mara kwa mara. Hizi zote ni kazi Zangu, mipango Yangu yote na hata zaidi, usimamizi Wangu—hakuna mtu anayejua au kuelewa hivi vitu. Wakati tu Mimi Mwenyewe Ninapowaambia, wakati tu Ninapowasiliana nanyi uso kwa uso kuihusu ndipo unajua kidogo; vinginevyo, hakuna kabisa anayejua mpango makini wa mpango Wangu wa usimamizi. Hii ndiyo nguvu Yangu kuu na hata zaidi matendo Yangu ya ajabu, ambayo hakuna anayeweza kubadilisha. Kwa hivyo, kile Ninachosema leo hutimika, na hii haiwezi kubadilika tu. Katika fikira za kibinadamu hakuna hata ufahamu kidogo juu Yangu—yote ni kuropoka kwa upuuzi! Usifikiri kwamba umepata ya kutosha au kwamba umekamilika! Ninakwambia, bado una mbali pa kwenda! Kwa mpango Wangu wote wa usimamizi, mnajua kidogo tu, kwa hivvyo lazima msikize kile Ninachosema na mfanye chochote Ninachowaambia mfanye. Tendeni kulingana na mapenzi Yangu katika kila kitu na hakika mtakuwa na baraka Zangu; yeyote aaminiye anaweza kupokea, huku yeyote asiyeamini atakuwa na “hakuna” ambayo alidhania imekamilika ndani yake. Hii ni haki Yangu, na, hata zaidi ni uadhama Wangu, hasira na adabu—Sihurumii moyo wa yeyote au mawazo, wala matendo yao yote.
Kusikiliza maneno Yangu watu wengi huogopa na kutetemeka kwa kipaji kilichojikunja kwa wasiwasi. Je Nimekukosea? Je inawezekana kuwa kwamba wewe siye mmoja wa watoto wa joka kuu jekundu? Unajifanya kuwa mzuri! Na kujifanya kuwa mwana Wangu mzaliwa wa kwanza! Je unafikiri Mimi ni kipofu? Je unafikiri Siwezi kutofautisha kati ya watu? Mimi ndiye Mungu anayechunguza mioyo ya ndani ya watu: Hili ndilo Ninalowaambia wana Wangu na ndilo Ninalowaambia pia—watoto wa joka kuu jekundu. Ninaona kila kitu kwa wazi, bila kosa lolote. Ningekosaje kujua kile Ninachokifanya? Niko wazi kabisa kukihusu! Kwa nini Nasema kwamba Mimi ni Mungu Mwenyewe, Muumbaji wa vitu vyote ulimwenguni? Kwa nini Nasema kwamba Mimi ndiye Mungu anyechunguza mioyo ya ndani ya watu? Ninajua vyema hali ya kila mtu. Je mnafikiri sijui cha kufanya au cha kusema? Hili haliwahusu—muwe makini msiuwawe kwa mkono Wangu; katika njia hiyo mngepata hasara. Amri Zangu za utawala hazina msamaha. Je mnaelewa? Haya yote hapa juu ni sehemu ya amri Zangu za utawala.Kuanzia siku ile Ninayowaaambia, ikiwa kuna ukiukaji wowote zaidi kutakuwa na adhabu, kwa sababu awali hamkuelewa.
Sasa Nawatangazia rasmi amri Zangu za utawala (zinaanza kazi kuanzia siku zilipotangazwa rasmi, kutoa adabu tofauti kwa watu tofauti):
Natimiza ahadi zangu, na kila kitu kiko mikononi Mwangu: Yeyote aliye na shaka hakika atauwawa. Hakuna nafasi ya huruma yoyote ile. Wataangamizwa mara moja, kuondoa chuki kutoka kwa moyo Wangu. (Kutokana na hili inadhibitika kwamba yeyote anayeuwawa lazima asiwe mmoja wa wanachama wa ufalme Wangu, na lazima awe wa ukoo wa Shetani.)
Kama wazaliwa wa kwanza wa kiume ni sharti mtunze nafasi zenu na mfanye waajibu wenu vema na msiwe watu wadaku. Ni sharti mjitolee kwa mpango Wangu wa usimamizi, popote muendapo ni sharti muwe na ushuhuda huo mzuri Kwangu na kulitukuza jina Langu. Msifanye vitu vyenye aibu, bali muwe mfano kwa wana Wangu wote na watu Wangu. Msikose kutokuwa na mipaka hata kwa muda kidogo: Lazima muonekane kila mara kwa kila mtu kwa utambulisho wa wazaliwa wa kwanza wa kiume, sio kuwa watumwa, bali kutembea kwa hatua kubwa kwa kujiamini. Nawaomba mlitukukuze jina Langu, sio kulitia aibu jina Langu. Wale ambao ni wazaliwa kwanza wa kiume kila mmoja ana kazi yake, na hawawezi tu kufanya chochote wanachotaka kufanya. Hili ndilo jukumu nililowapa, ambalo halipaswi kuepukwa, na lazima mjitolee wenyewe kutimiza Nilichowaaminia kwa mioyo yenu yote, kwa akili zenu yote na kwa nguvu zenu zote.
Baada ya hili, katika Ulimwengu wote, jukumu la kuongoza wana Wangu wote na watu Wangu wote limekabidhiwa wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume kutimiza, na yeyote asiyeweza kulitimiza kwa moyo wake wote na akili yake yote, Nitamuadibu. Hii ni haki Yangu—Sitawahurumia au kuwabembeleza hata wazaliwa Wangu wa kiume wa kwanza.
Ikiwa kuna yeyote kati ya wana Wangu wote au kati ya watu Wangu wote anayemdhihaki na kumtusi mmoja wa wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume, Nitamuadhibu vikali kwa sababu wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume wananiwakilisha Mimi, na kile mtu anachowafanyia ananifanyia Mimi pia. Hii ndiyo kali zaidi kwa amri Zangu za utawala. Natoa mwito kwa wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume kutoa haki Yangu kulingana na mapenzi yao dhidi ya yeyote miongoni mwa wana Wangu wote na watu Wangu wote anayekiuka hii amri.
Taratibu Namtenga yeyote anayenitazama kipuuzi; akilenga tu chakula Changu, mavazi na usingizi; akishughulikia tu mambo Yangu ya nje na hashugulikii kuzingatia mzigo Wangu; na hatilii maanani kutimiza kazi yake inavyostahili. Hili linaelekezwa kwa wote walio na masikio.
Yeyote amalizaye kunifanyia huduma lazima aondoke kwa staha bali asiwe na kelele. Kuwa makini, la sivyo Nitapambana nawe. (Hii ni ya ziada).
Wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume watachukua fimbo ya chuma kuanzia sasa na kuendelea na kuanza kutekeleza mamlaka Yangu kutawala mataifa yote na watu, kutembea kati ya mataifa yote na watu na kuzifanya hukuma Zangu, haki, na uadhama kati ya mataifa yote na watu. Wana Wangu wote na watu Wangu wote wataniogopa, watanipa sifa, watanishangilia, na kunitukuza bila kukoma kwa sababu mpango wangu wa usimamizi umekamilika na wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume wanaweza kutawala nami.
Hii ni sehemu ya amri Zangu za utawala. Na baadaye Nitawaambia kulingana na kiwango cha maendeleoa ya kazi. Kutokana na amri za utawala zilizoko hapo juu mtaona mwendo Ninaoutumia kufanya kazi Yangu, na kuona hatua ambayo kazi Yangu imesogea. Hili ndilo thibitisho.
Nimeshamhukumu Shetani, kwa sababu mapenzi Yangu hayapingwi, na kwa sababu wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume wametukuzwa pamoja nami. Na tayari Nimetumia haki Yangu na uadhama kuelekea dunia na vitu vyote ambavyo ni mali ya Shetani. Sikiinui kidole wala kumsikiliza Shetani kabisa (kwa sababu hastahili kuongea na Mimi). Nazidi tu kufanya kile Ninachotaka kufanya. Kazi Yangu inaendelea kwa ulaini, hatua kwa hatua na mapenzi Yangu hayapingwi nchini kote. Hili limemwaibisha Shetani kwa kiwango na ameangamizwa kabisa, lakini hili halijatimiza mapenzi Yangu. Naruhusu pia wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume ks amri Zangu za utawala juu ya mambo yote yaliyo ya Shetani. Kwa upande mmoja, kile Ninachomruhusu Shetani kuona ni hasira Yangu kumuelekea; kwa upande mwingine Namruhusu auone utukufu Wangu (kuona kwamba wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume ndio mashahidi wakubwa sana kwa udhalilishaji wa shetani). Simuadhibu Mimi binafsi, bali Naruhusu wazaliwa wangu wa kwanza wa kiume kutekeleza haki Yangu na uadhama. Kwa sababu alikuwa anawanyanyasa wana Wangu, kuwatesa wana Wangu na kuwaonea wana Wangu, leo, baada ya huduma yake kuisha, Nawaruhusu wazaliwa Wangu wa kwanza wa kiume waliokomaa kumwangamiza. Shetani amekuwa hana nguvu dhidi ya maangamizi. Kiharusi cha mataifa yote duniani ndio ushuhuda bora zaidi, watu kupigana na nchi zikiwa vitani ni onyesho dhahiri la kuanguka kwa ufalme wa Shetani. Kwamba Sikuonyesha ishara zozote na maajabu kabla ilikuwa kwa ajili ya kumdhalilisha Shetani na kulitukuza jina Langu hatua kwa hatua. Wakati shetani ameangamizwa kabisa Naanza kuonyesha nguvu Zangu: kile Ninachosema kinatokea, na vitu vya kuvuka mipaka ambavyo havina usawa na dhana za kibinadamu vitatimika (hili linahusu baraka zinazokuja karibuni). Kwa sababu Mimi ndiye Mungu Mwenyewe aliye hai na Sina amri, na Nazungumza kulingana na mabadiliko katika mpango Wangu wa usimamizi, kwa hivyo kile Nilichosema zamani sio lazima kiwe cha kutumika sasa. Msishikilie fikira zenu wenyewe! Mimi siye Mungu anayezingatia amri. Na Mimi, kila kitu ni huru, cha kuvuka mipaka, na kimeachiliwa kabisa. Labda kilichosemwa jana kimepitwa na wakati leo au kimewekwa kando leo (lakini amri Zangu za utawala, kwa sababu zimetangazwa rasmi hazibadiliki). Hizi ndizo hatua katika mpango Wangu wa usimamizi. Msishikilie kanuni. Kila siku kuna mwanga mpya, ufunuo mpya, na huo ndio mpango Wangu. Kila siku mwanga wangu utafichuliwa kwako na sauti Yangu itaachiliwa kwa Ulimwengu. Je unaelewa? Huu ni wajibu wako, jukumu ambalo Nimekuaminia. Ni lazima usilipuuze hata kwa muda mfupi. Watu Ninaoidhinisha, Nitawatumia mpaka mwisho, na hili halitabadilika kamwe. Kwa sababu Mimi ni mwenyezi Mungu, Najua mtu wa aina gani anapaswa kufanya kitu kipi, na mtu wa aina gani anaweza kufanya kitu kipi. Huu ndio uweza Wangu.
Chanzo: Sura ya 88
Makala Husika: Matamshi ya Mungu | Sura ya 89

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni