8/03/2019

Neno la Mwenyezi Mungu | Sura ya 60

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Neno la Mwenyezi Mungu | Sura ya 60


Si jambo rahisi kwa maisha kukua; yanahitaji mchakato, na aidha, kwamba muweze kulipa gharama na kwamba mshirikiane na Mimi kwa uwiano, na hivyo mtapata sifa Yangu. Mbingu na dunia na vitu vyote vinaanzishwa na kufanywa kamili kupitia maneno ya kinywa Changu na chochote kinaweza kutimizwa nami. Matakwa Yangu ya pekee ni kwamba mkue haraka, mchukue mzigo kutoka kwa mabega Yangu na kuuweka kama wenu, mfanye kazi Zangu kwa niaba Yangu, na hilo litauridhisha moyo Wangu. Ni mwana yupi angekataa mizigo ya babake? Ni baba yupi hangefanya kazi usiku na mchana kwa ajili ya mwana wake? Lakini ninyi hamwelewi mapenzi Yangu, hamfikirii mizigo Yangu, maneno Yangu hayana maana kwenu na hamfanyi jinsi maneno Yangu yanavyosema. Daima mnajitawala; ninyi ni wabinafsi kiasi gani! Mnajifikiria wenyewe tu!
Je, kweli unaelewa mapenzi Yangu au unajifanya kutoelewa tu? Kwa nini daima unajishughulisha na mienendo mitundu kama hiyo? Kusema kweli, hiyo ni njia ya kufikia matarajio Yangu? Wakati umepata chanzo cha ugonjwa, mbona hushiriki na Mimi ili upate matibabu? Nitakuambia: Kuanzia siku hii kuendelea hamtakuwa na magonjwa ya mwili tena. Sehemu yenu yoyote ikihisi gonjwa msijishughulishe kutafuta chanzo cha nje. Badala yake, kujeni mbele Yangu na kutafuta kujua nia Yangu—mtakumbuka hili? Hii ni ahadi Yangu: Kuanzia siku hii kuendelea mbele mtaondoka kwa mwili wenu kabisa na kuingia dunia ya roho, yaani, mwili wenu hautasumbuliwa na ugonjwa tena. Mnafurahia hilo? Mnahisi furaha? Hii ni ahadi Yangu na aidha, kile ambacho mmetamani kwa muda mrefu. Leo kimetimika kwa ninyi mliobarikiwa; jambo la ajabu na lisiloeleweka vipi!
Kazi Yangu inaendelea usiku na mchana, muda kwa muda haikomi kamwe. Hii ni kwa sababu tamaa Yangu ya dharura ni kukufanya uupendeze moyo Wangu, na kwamba moyo Wangu utafarijiwa na ninyi hivi karibuni. Wana Wangu! Wakati umefika wa ninyi kushiriki katika baraka Zangu za wema! Zamani, ninyi mliteseka kwa ajili ya jina Langu lakini sasa siku zenu za majaribu zimekwisha. Yeyote akijaribu kuumiza unywele kutoka kwa vichwa vya Wanangu, Sitamsamehe kwa urahisi na hatakuwa huru kamwe. Hii ni amri Yangu ya utawala na yeyote atakayekiuka hii atajihatarisha. Wanangu! Furahieni mpaka mridhike! Imbeni na kuita kwa shangwe! Hamtadhulumiwa na kukandamizwa tena na hamtapitia mateso tena. Hamtalazimika kuendelea kuniamini kwa woga tena, imani yenu inaweza kuwa wazi kwa dunia[a] Liiteni jina Langu takatifu ili liweze kunguruma kwa miisho ya mbali zaidi ya ulimwengu. Acha wao waone, wale waliowaangalia kwa dharau, walioangamizwa na kuteswa na wao, leo kuwa na mamlaka juu yao na kuwatawala, waongoze, na muhimu zaidi, wahukumu.
Mnapaswa kujihusisha na kuingia kwenu pekee, na Nitawapa baraka hata nzuri zaidi ili mweze kuzifurahia, na baraka hizi zitawaruhusu kuonja utamu wao usiolinganika vyema zaidi na kuhisi kwa nguvu siri zao zisizoisha na kwamba ni kubwa sana kuelewa!
Tanbihi:
a. Maandishi ya asili hayana maneno “kwa dunia.”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni