Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Majina-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Majina-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote

7/05/2018

Kwa Nini Mungu Hutajwa Majina, na Jina Moja Linaweza Kuwakilisha Uzima wa Mungu?

Sura ya 2 Ukweli wa Majina ya Mungu

1. Kwa Nini Mungu Hutajwa Majina, na Jina Moja Linaweza Kuwakilisha Uzima wa Mungu?

Maneno Husika ya Mungu:
Je, Jina la Yesu “Mungu pamoja nasi,” linaweza kuwakilisha tabia ya Mungu kwa ukamilifu wake? Je, linaweza kueleza Mungu kwa ukamilifu? Kama mwanadamu atasema ya kwamba Mungu Ataitwa tu Yesu, na hawezi kuwa na jina lingine kwa sababu Mungu hawezi kubadilisha tabia yake, basi maneno hayo ni kufuru! Je, unaamini kwamba jina la Yesu, Mungu pamoja nasi, linaweza kumwakilisha Mungu kikamilifu? Mungu Anaweza kuitwa majina mengi, lakini baina ya majina haya mengi, hamna moja ambalo linaweza kujumlisha yote ambayo Mungu Anamiliki, na hamna jina moja ambalo linaweza kumwakilisha Mungu kikamilifu.

2/03/2018

Imani za Kimsingi za Kanisa la Mwenyezi Mungu

(1) Mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Mafundisho ya Ukristo yanatoka kwa Biblia, na mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu yanatoka kwa ukweli wote ulioonyeshwa na Mungu tangu wakati wa uumbaji wakati wa kazi ya Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema, na Enzi ya Ufalme. Hiyo ni kusema, Agano la Kale, Agano Jipya, na Biblia ya Enzi ya Ufalme–Neno Laonekana Katika Mwili–zilizoonyeshwa Bwana Yesu aliyekurudi wa siku za mwisho, Mwenyezi Mungu, ni imani za msingi na mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu. Agano la Kale linarekodi kazi ya Yehova Mungu ya kuagiza sheria na amri na kuyaongoza maisha ya mwanadamu wakati wa Enzi ya Sheria;Agano Jipya linarekodi kazi ya ukombozi iliyofanywa na Bwana Yesu wakati wa Enzi ya Neema; na Neno Laonekana Katika Mwili yote ni ukweli kwa ajili ya utakaso na wokovu wa wanadamu ulioonyeshwa na Mwenyezi Mungu wakati wa Enzi ya Ufalme, pamoja na maelezo ya kazi ya hukumu ya Mungu wakati wa siku za mwisho.Biblia ya kweli ni matamko yote ya Mungu wakati wa hatua tatu za kazi, na imani za msingi za Kanisa la Mwenyezi Mungu ni matamko yote ya Mungu wakati wa hatua tatu za kazi, yaani, ukweli wote ulioonyesha na Mungu wakati wa hatua hizi tatu za kazi.