Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Maswali-na-Majibu-Mia Moja-Kuhusu-Kuichunguza-Njia-ya-Kweli. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Maswali-na-Majibu-Mia Moja-Kuhusu-Kuichunguza-Njia-ya-Kweli. Onyesha machapisho yote

6/23/2018

Mungu Aliilinda Familia Yetu Wakati wa Maafa

***********🌼🌼🌼❤️❤️❤️***********
~~~~~~~❤️❤️❤️🌻🌻🌻************🌻🌻🌻❤️❤️❤️~~~~~~
Wang Lan, Beijing
Agosti 6, Mwaka wa 2012
Mnamo Julai 21, mwaka wa 2012, mafuriko makubwa zaidi tangu miaka sitini yalipitia kijijini mwetu kwa nguvu mno. Maafa yalianguka kutoka mbinguni, maji ya mafuriko yalichanganya matope na mawe na kuharibu kijiji chote. Nyumba nyingi ziliharibiwa na maji na maporomoko ya matope.

6/18/2018

Mwenyezi Mungu Amenipa Fursa ya Pili Katika Maisha


Ndugu wawili wa kawaida, Beijing 
                                                        
                                                                     Agosti 15, 2012
Julai 21, mwaka wa 2012 ilikuwa siku isiyosahaulika sana kwangu, pamoja na kuwa siku muhimu zaidi ya maisha yangu.
Siku hiyo, mvua kubwa ilikuwa ikinyesha katika Wilaya ya Fangshan jijini Beijing—ilikuwa kubwa kuliko yoyote iliyowahi kuonekana pale katika miaka sitini na mmoja. Muda mfupi baada ya saa 4 jioni, nilitoka nje mtaani ili kuangalia na nikaona kuwa maji yalikuwa kila mahali. Gari la familia yetu lilikuwa tayari limeelea, na sababu ya pekee gari hilo kutosombwa na mkondo wa maji ilikuwa kwamba lilizuiwa na kitu mbele yake kilicholizuia kusonga.