1/25/2018

Kazi ya Kueneza Injili Ni Kazi ya Kuokoa Binadamu Pia

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu
    Mwenyezi Mungu alisema, Watu wote wanahitaji kuelewa kusudio la kazi Yangu ulimwenguni, yaani, lengo la mwisho la kazi Yangu na ni kiwango kipi ambacho lazima Nitimize katika kazi hii kabla inaweza kukamilika. Kama watu, wanaotembea na Mimi hadi leo, hawaelewi kazi Yangu inahusu nini, basi hawajakuwa wakitembea na Mimi bure? Watu wanaonifuata Mimi wanafaa kujua mapenzi Yangu. Nimekuwa nikifanya kazi ulimwenguni kwa maelfu ya miaka, na ningali nafanya hivyo sasa. Ingawaje kunavyo vipengele vingi hasa vilivyojumuishwa katika kazi Yangu, kusudio lake linabakia lilelile. Kwa mfano, ingawaje nimejazwa na hukumu na adabu kwake binadamu, bado ni kwa ajili ya kumwokoa binadamu, ili niweze kueneza kwa njia bora zaidi injili Yangu na kupanua zaidi kazi Yangu miongoni mwa Mataifa baada ya binadamu kufanywa kuwa kamili. Kwa hiyo sasa, kwa wakati ambapo watu wengi tayari wametamauka pakubwa, ninaendelea na kazi Yangu, nikiendeleza kazi ambayo lazima nifanye ili kuhukumu na kuadibu binadamu. Licha ya ukweli kwamba binadamu amechoshwa na kile ninachosema na licha ya ukweli kwamba hana tamanio la kujali kuhusu kazi Yangu, ningali natekeleza wajibu Wangu kwa sababu kusudio la kazi Yangu halijabadilika na mpango Wangu asilia hautabadilika. Kazi ya hukumu Yangu ni kumfanya binadamu kunitii Mimi kwa njia bora zaidi, na kazi ya adabu Yangu ni kuruhusu binadamu kuwa na mabadiliko bora zaidi. Ingawaje kile ninachofanya ni kwa minajili ya usimamizi Wangu, sijawahi kufanya chochote ambacho hakikufaidi binadamu. Hiyo ndiyo maana ninataka kufanya mataifa yote nje ya Israeli kuwa matiifu tu kama Waisraeli na kuwabadilisha kuwa binadamu halisi, ili niwe na mahali pa usalama katika nchi zilizo nje ya Israeli. Huu ndio usimamizi Wangu; ndiyo kazi ninayotimiza katika nchi za Mataifa. Hata sasa, watu wengi bado hawauelewi usimamizi Wangu kwa sababu hawajautilia maanani, badala yake wanafikiria tu kuhusu mustakabali na hatima yao. Haijalishi ni nini ninachosema, watu hawajali kazi Yangu, badala yake wanalenga tu hatima zao za baadaye. Kwa hiyo kama hilo litaendelea, kazi Yangu itapanuliwa vipi? Injili Yangu itaenezwa vipi kotekote ulimwenguni? Lazima mjue kwamba wakati kazi Yangu inapanuka, nitawatawanya, Nitawaadhibu kama vile tu Yehova alivyoyaadhibu makabila ya Israeli. Haya yote yatafanywa ili injili Yangu iweze kuongezeka kotekote kwenye ulimwengu mzima, ili kazi Yangu iweze kuenezwa kwa Mataifa. Kwa hiyo, jina Langu litasifiwa na watu wazima na watoto kwa pamoja na jina Langu takatifu litatukuzwa kwa vinywa vya watu kutoka makabila na mataifa yote. Katika enzi ya mwisho, Nitafanya jina Langu litukuzwe miongoni mwa Mataifa, kufanya matendo Yangu kuonekana na mataifa mengine ili waniite Mwenyezi kwa sababu ya matendo Yangu, na kuyafanya maneno Yangu kutimika karibuni. Nitawafanya watu wote kujua kwamba Mimi siye tu Mungu wa Waisraeli, lakini Mimi ni Mungu wa Mataifa yote, hata mataifa yale niliyoyalaani. Nitawafanya watu wote kuona kwamba Mimi ndimi Mungu wa viumbe vyote. Hii ndiyo kazi Yangu kubwa zaidi, kusudio la mpango wa kazi Yangu katika siku za mwisho, na kazi ya kutimizwa tu katika siku za mwisho.

    Kazi ambayo nimekuwa nikisimamia kwa maelfu ya miaka inafichuliwa kabisa tu kwa binadamu kwenye siku za mwisho. Ni sasa tu ndipo nimelifumbua fumbo kamili la usimamizi Wangu kwa mwanadamu. Binadamu anajua kusudio la kazi Yangu na zaidi ya yote anapata uelewa wa mafumbo Yangu yote. Na nimemwambia binadamu kila kitu kuhusu hatima ambayo amekuwa akiijali. Tayari nimemfichulia binadamu mafumbo yote yaliyofichwa kwa zaidi ya miaka 5,900. Yehova ni nani? Masiha ni nani? Yesu ni nani? Mnafaa kuyajua haya yote. Mabadiliko makubwa ya kazi Yangu yamo katika majina haya. Je, mmeelewa haya? Mnafaa kutangaza jina Langu takatifu vipi? Mnafaa kueneza jina Langu katika taifa lolote ambapo majina Yangu yoyote yameitwa? Kazi Yangu tayari imeanza kupanuka, na nitaeneza ukamilifu wake katika mataifa yote. Kwa sababu kazi Yangu imetekelezwa ndani yenu, nitawapiga kama vile Yehova alivyowapiga wale wachungaji wa nyumba ya Daudi kule Israeli, na kuwasababisha kutawanywa miongoni mwa mataifa yote. Kwani katika siku za mwisho, nitapondaponda mataifa yote na kusababisha watu wao kuenezwa tena. Nitakaporudi tena, mataifa yatakuwa tayari yamegawanywa kwa mipaka iliyowekwa na mwako wa moto Wangu utakayokuwa ukichoma. Katika wakati huo, nitajionyesha upya kwa binadamu kama jua la kuchoma, nikijionyesha kwao hadharani kwa taswira ya yule Aliye Mtakatifu ambaye hawajawahi kumwona, nikitembea miongoni mwa mataifa yote, kama vile tu Mimi, Yehova, nilivyotembea miongoni mwa makabila ya Wayahudi. Kuanzia hapo kuendelea, nitawaongoza watu huku wakiishi ulimwenguni. Watauona utukufu Wangu hapo na wataona pia nguzo ya wingu hewani ili uwaongoze, kwani ninaonekana katika sehemu takatifu. Binadamu ataiona siku Yangu ya haki na maonyesho Yangu ya utukufu. Hilo litafanyika nitakapoutawala ulimwengu mzima na kuwaleta wana wengi mbele ya utukufu. Wote watainama kila pahali, nalo hema Langu takatifu litaundwa miongoni mwao juu ya mwamba wa kazi ambayo natekeleza sasa. Watu watanihudumia pia hekaluni. Madhabahu, yaliyojaa mambo machafu, ya kuchukiza, kuvunjwavunjwa vipandevipande na nitajenga upya mengine. Madhabahu matakatifu yatarundikwa wanakondoo na ndama waliozaliwa karibuni. Nitaangusha hekalu lililopo leo na kujenga jingine upya. Hekalu lililopo sasa na lililojaa watu wenye chuki litaporomoka. Hekalu nitakalojenga litajaa watumishi watiifu Kwangu. Kwa mara nyingine watasimama na kunihudumia Mimi kwa utukufu wa hekalu Langu. Kwa hakika mtaiona siku Yangu ya utukufu mkuu. Mtaiona siku ambayo nitaliangusha hekalu na kujenga lingine upya. Mtaona pia siku ya kuletwa kwa hema Langu takatifu hapa ulimwenguni. Huku nikigandamiza hekalu, ndivyo nitakavyoleta hema Langu takatifu hapa ulimwenguni, kama vile tu ambavyo watu wanavyoniona Mimi nikishuka. Baada ya kuangamiza mataifa yote, nitayakusanya pamoja upya, nikilijenga hekalu Langu na kuandaa madhabahu Yangu ili wote waweze kutoa kafara zao Kwangu, kunihudumia Mimi hapo, na kujitolea kwa uaminifu katika kazi Yangu kwenye mataifa mengineyo. Itafanywa namna tu ambavyo wana wa Israeli wanavyofanya sasa, na joho la kuhani na taji la mfalme, utukufu Wangu mimi, Yehova, ukiwa miongoni mwao na uadhama Wangu ukivinjari juu yao na ukiwa nao. Kazi Yangu katika Mataifa yatatekelezwa pia katika njia hiyo. Kama vile kazi Yangu kule Israeli ilivyokuwa, ndivyo kazi Yangu kwenye mataifa ya wasio Wayahudi itakavyokuwa kwa sababu nitaongeza kazi Yangu kule Israeli na kuieneza kwenye mataifa yale mengine.

    Sasa ndio wakati ambao Roho Wangu anafanya kazi pakubwa, na wakati ninapofanya kazi miongoni mwa mataifa ya wasio Wayahudi. Hata zaidi, ndio wakati ambapo ninaweka katika kundi tofauti viumbe wote na kuweka kila kiumbe kwenye uainishaji wake wa pekee ili kazi Yangu iweze kuendelea haraka zaidi na kwa njia ya kufaa zaidi. Kwa hiyo, bado ninahitaji kwamba ujitoe mzimamzima kwa minajili ya kazi Yangu yote; aidha, unafaa kutambua waziwazi na kuwa na hakika ya kazi ile yote ambayo nimefanya ndani yako, na kuweka nguvu zako zote katika kazi Yangu ili iweze kuwa ya kufaa zaidi. Hilo ndilo ambalo lazima uelewe. Msipigane tena wenyewe kwa wenyewe, kutafuta mbinu za usuluhishi, au kutafuta raha za mwili, mambo ambayo yanaweza kuchelewesha kazi Yangu na kuharibu mustakabali wako mzuri. Hilo lingekuangamiza tu, na kwa vyovyote vile halingekulinda. Je, hungekuwa mjinga? Kile ambacho unafurahia leo kwa tamaa ndicho kile kile ambacho kinaharibu mustakabali wako, huku yale maumivu unayopitia leo ndiyo yaleyale ambayo yanakulinda. Lazima ufahamu waziwazi kuhusu jambo hilo, ili uepuke majaribio ambayo yatakuwa magumu kujinasua kutoka na kuepuka kuingia kwenye ukungu mzito unaozuia jua katika maisha yako. Wakati ukungu huu mzito utakapotoweka, utajipata katika hukumu ya siku kuu. Kufikia wakati huo, siku Yangu itakuwa imekaribia binadamu. Utatorokaje hukumu Yangu? Utawezaje kuvumilia joto kali la jua? Ninapompa binadamu wingi Wangu, haufurahii kwa dhati, lakini badala yake anautupa nje kwenye sehemu zisizotambulika. Wakati siku Yangu itakapowadia, binadamu hataweza tena kugundua wingi Wangu au kupata ukweli mkali niliompa zamani sana. Ataomboleza na kulia kwa kutokuwepo kwa mwangaza unaofuata kuingia katika giza totoro. Kile mnachoona leo ni upanga tu mkali wa kinywa Changu. Bado hamjakiona kiboko kilicho katika mkono Wangu au moto ninaotumia kumchoma binadamu, na ndiyo maana mngali mna kiburi na msio na kadiri mbele Yangu. Ndiyo maana bado mnapigana na Mimi katika nyumba Yangu, huku mkipinga kile ambacho nawaambia. Binadamu haniogopi Mimi. Akiwa angali katika uhasama na Mimi hadi leo, angali haniogopi kamwe. Mnao ulimi na meno ya wale wasio na haki kinywani mwao. Maneno na matendo yenu ni kama yale ya yule nyoka aliyemshawishi Hawa na kumfanya kutenda dhambi. Mnahitaji wenyewe kwa wenyewe kulipiza kisasi, na mnashindana kwa ajili ya cheo chako, umaarufu wako, na faida yako mbele Yangu, ilhali hamjui kwamba ninatazama maneno na matendo yenu kwa siri. Kabla hata hamjaja mbele Yangu, nimezijua akili zenu kabisa. Siku zote binadamu hutamani kutoroka kutoka mkono Wangu na kuepuka uangalizi wa macho Yangu, lakini sijawahi kuepuka maneno au matamshi yake. Badala yake, kwa kusudio kuu huwa ninayaruhusu kufikia macho Yangu ili niweze kuadibu udhalimu wake na kuhukumu uasi wake. Kwa hiyo, maneno na matendo fiche ya binadamu siku zote yanawekwa katika kiti Changu cha hukumu, na haijawahi kumtoka binadamu, kwa sababu uasi wake ni mwingi mno. Kazi Yangu ni kuteketeza na kusafisha maneno na matendo yote ya binadamu yaliyotamkwa na kufanywa mbele ya Roho Wangu. Kwa njia hiyo, baada ya Mimi kuondoka ulimwenguni, binadamu wataweza bado kuendeleza utiifu Kwangu, na bado watanihudumia kama vile watumishi Wangu watakatifu wanavyofanya katika kazi Yangu, wakiruhusu kazi Yangu hapa ulimwenguni kuendelea mpaka siku itakapokamilika.
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Kuhusu Sisi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni