2/25/2018

Sura ya 44. Kuutoa Ukweli Ndiyo Njia ya Kweli ya Kuwaongoza Wengine

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Kanisa
Kuutoa Ukweli Ndiyo Njia ya Kweli ya Kuwaongoza Wengine 
Mwenyezi Mungu alisema,Ikiwa mnataka kufanya kazi nzuri katika kuwaongoza wengine na kuhudumu kama mashahidi wa Mungu, la muhimu zaidi, lazima uwe na ufahamu wa kina wa kusudi la Mungu katika kuwaokoa watu na kusudi la kazi Yake. Lazima uyaelewe mapenzi ya Mungu na mahitaji Yake mbalimbali ya watu. Unapaswa kuwa mwenye utendaji katika juhudi zenu; upitie tu kiasi unachoelewa na kuwasiliana tu kile unachokijua. Usijisifu, usitie chumvi, na usiseme maneno yasiyopaswa. Ukitia chumvi, watu watakuchukia na utahisi mwenye kushutumiwa baadaye; hili ni jambo lisilofaa kabisa. Unapotoa ukweli kwa wengine, si lazima uwe wa kushurutisha ili wao waweze kuupata ukweli. Ikiwa wewe mwenyewe huna ukweli, ilhali unakuwa mwenye kushurutisha kwa wengine, watakuogopa. Lakini hiyo haimaanishi kuwa wanauelewa ukweli. Katika kazi fulani za utawala, ni vizuri kwako kuwashughulikia na kuwapogoa wengine na kuwaadhibu kwa kiwango fulani. Lakini ikiwa huwezi kuutoa ukweli na unajua tu jinsi ya kuwa mwenye kuwalazimisha na kuwakaripia wengine, upotovu na uovu wako utafunuliwa. Muda unavyopita, kama vile watu hawawezi kupata maisha au mambo ya utendaji kutoka kwako, watakuja kukuchukia, kuhisi chukizo kwako. Wale ambao hawana utambuzi watajifunza mambo mabaya kutoka kwako; watajifunza kushughulikia na kuwapogoa wengine, kuwa na hasira, kukasirika. Je, hiyo si sawa na kuwapeleka wengine kwenye njia ya Paulo, njia ya kuelekea kuangamia kabisa? Je, huo sio utenda uovu? Kazi yako inapaswa kulenga kuwasiliana ukweli na kutoa maisha kwa wengine. Ikiwa yote unayofanya ni kuwashughulikia na kuwahubiria wengine bila kufikiri, watawezaje kuuelewa ukweli daima? Wakati unapoendelea, watu watakuona jinsi wewe ulivyo kwa kweli, nao watakuacha. Unawezaje kutarajia kuwaleta wengine mbele ya Mungu kwa njia hii? Huku kunakuwaje kufanya kazi? Utazivuruga kazi zako zote ukiendelea kufanya kazi kwa njia hii. Aidha, ikiwa kila mtu anakuepuka, ni kazi gani unayotarajia kukamilisha basi? Zamani, viongozi wengine walitenda hasa kwa njia hii. Walishindwa kufanya kazi nzuri na za utendaji; wakati mipango ya kazi ilitoka kwa aliye juu, walishindwa kuiweka katika matokeo mazuri. Hawakufanya kazi maalum. Yote waliyofanya ilikuwa ni kuwasiliana barua zao na mafundisho au kushughulika na kuwapogoa wengine kwa upofu. Matokeo yake, watu walikuja kuwaogopa na kuwakwepa. Waliivuruga kazi na kisha wakadai kuwa walikuwa wanapata tu mienendo yao. Mwishowe, waliondolewa, na kutumwa nyumbani.
Huwezi kumtumikia Mungu ikiwa tabia yako haijabadilika. Watu wengine huweka visingizio kwa ajili yao wenyewe, wakisema: "Ninawasiliana na watu wa Kichina, na watu wa Kichina wamepotoka kabisa. Matokeo yake, nimekuwa mpotovu kwa sababu ya ushawishi wao juu yangu. Kwa hivyo, ikiwa nimefanya makosa, hakika, ni ya kusamehewa. Ikiwa ningekuwa na mawasiliano na wageni na kunufaika na ushawishi wao, ningeweza kuwa mtu bora. "Hoja hii haiwezekani. Mabadiliko ya tabia ya mtu si kitu ambacho kinaweza kusomwa kutoka kwa wengine. Maarifa, uadilifu, utambuzi, tabia, mtindo wa kuzungumza, na mambo mengine yote ya nje yanaweza kusomwa kutoka kwa wengine; lakini maisha na ukweli vinaweza kupatikana tu kutoka kwa neno la Mungu. Unapokula na kunywa maneno ya Mungu, lazima ufuatilie njia sahihi ili uuelewe ukweli, lakini hili si sawa na kuuweka ukweli katika vitendo na kuingia katika uhalisi. Ili kuuelewa ukweli, mtu lazima ale na kunywa kwa njia hii. Chukua kula na kunywa kwa kifungu kuhusu ukweli wa upendo kwa Mungu, kwa mfano. Neno la Mungu linasema: "Upendo ni hisia safi na isiyo na dosari. Katika upendo, hakuna shaka, hakuna vizuizi, hakuna umbali, ambapo unatumia moyo wako kupenda na kuwa na mawazo." Huu ndio ufafanuzi wa upendo. Huu ndio ukweli. Hili ndilo Mungu anasema kuhusu upendo. Lakini utampenda nani? Je, utampenda mume wako? Mke wako? Ndugu zako? Hapana! Mungu anapozungumza juu ya upendo, Hazungumzi kuhusu upendo kwa mwanadamu mwenzako, bali kuhusu upendo wa mwanadamu wa Mungu. Hii ndio aina ya upendo wa kweli. Jinsi ya kuuelewa ukweli huu? Inamaanisha kwamba Mungu anataka watu wasiwe na shaka kumhusu au kwenda mbali kutoka Kwake; upendo huu ni safi, na hauna dosari. Kukosa dosari kuna maana kwamba matarajio yako kuelekea kwa Mungu sio badhirifu; kunamaanisha kwamba upendo wako kwa Mungu hauna masharti na hauhitaji sababu; kunamaanisha kwamba unampenda Mungu na hakuna mwingine. Mbali na Mungu, hakuna chochote kingine kinachoweza kuchukua moyo wako; hisia hii ni safi na haina dosari. Hisia hii inachukua nafasi fulani katika moyo wako; wewe daima unafikiri kumhusu Yeye na kumkosa Yeye, na kumkumbuka Yeye katika kila wakati. Kupenda kunamaanisha kupenda kwa moyo wako. Kupenda kwa moyo wako kunajumuisha kuwa na mawazo, kujali na kukumbuka kwa hamu. Ili kupenda kwa moyo wako, lazima kwanza ujifunze kuelewa. Kwa wakati wa sasa, wakati unapokosa ufahamu, unapaswa kuutumia moyo wako kumtamani, kumwonea shauku, kumtii, kumtunza, kumsihi, na kumlilia; unapaswa hata kuweza kushiriki katika mawazo na wasiwasi Wake. Lazima uuweke moyo wako katika mambo haya. Usiunge mkono kwa maneno matupu, ukisema: "Mungu! Ninafanya hili kwa ajili Yako, na ninafanya lile kwa ajili Yako!" Ni wakati tu unapompenda na kumridhisha Mungu kwa kutumia moyo wako ndio unakuwa na maana muhimu ya utendaji. Ingawa husemi hivyo kwa sauti sana, uko na Mungu moyoni mwako, moyoni mwako unamfikiri Yeye. Unaweza kumwacha mume wako, mke wako, watoto wako, jamaa zako; lakini moyo wako hauwezi kuwa bila Mungu. Bila Mungu, huwezi kuishi kabisa. Huwezi kumwacha. Hii ndiyo maana ya kuwa na upendo na kuwa na Mungu moyoni mwako. Kuna mengi sana yanayohusu kuwa na upendo na kumtunza Mungu kwa moyo wako. Huu ndio upendo wa kweli ambao Mungu anahitaji kwako; kwa maneno mengine, lazima umpende na kumtunza kwa moyo wako, na daima umweke katika akili yako. Tumia moyo wako, si maneno yako, kutenda. Usitumie vitendo vyako kama aina ya maonyesho ya nje, lakini badala yake, kimsingi, tenda kwa moyo wako, uache moyo wako udhibiti tabia yako, uvidhibiti vitendo vyako vyote. Hakupaswi kuwa na motisha, kusiwe na uzinzi, kusiwe shaka; hivi ndivyo moyo safi unapaswa kuwa. Kuhusu shaka, kuwa na shaka kunamaanisha nini? Kunamaanisha wewe daima unashangaa: "Je, ni haki kwa Mungu kufanya hivi? Kwa nini Mungu asema hivi? Ikiwa hivi ndivyo Mungu anavyosema, lakini hakuna sababu nyuma yake, sitalitii. Ikiwa Mungu afanya hivyo, lakini sio haki, sitatii. Nitaiacha kwa sasa." Kutohodhi mashaka kuna maana ya kutambua kwamba chochote kile ambacho Mungu anasema na kufanya ni sawa, na kwa Mungu hakuna wema au ubaya. Mwanadamu lazima amtii Mungu, amtunze Mungu, amridhishe Mungu, na kushiriki katika mawazo Yake na mahangaiko Yake. Bila kujali kama kila kitu ambacho Mungu anakifanya kinaonekana kuwa cha maana au kinachofaa kwako au la, ikiwa kinaridhiana na mawazo yako, na bila kujali ikiwa kinaeleweka kwako au ikiwa kinapatana na mawazo yako, lazima utii daima na lazima uwe na heshima, moyo wenye utii kwa kila kitu ambacho Mungu hufanya. Hata hivyo, si kutenda kwa aina hii ni kwa kupatana na na ukweli? Je, sio maonyesho na mazoezi ya upendo? Kwa hivyo, ikiwa huelewi mapenzi ya Mungu, ikiwa huelewi madhumuni ya maneno Yake, ikiwa huelewi lengo au matokeo ambayo Anatafuta kutimiza, ikiwa huelewi kile ambacho maneno Yake yanatafuta kutimiza na kukamilisha katika mwanadamu, basi bado huulewi ukweli. Kwa nini Mungu asema kile Anasemacho? Kwa nini Anasema kwa toni hiyo? Kwa nini Yeye ni mwenye bidii sana na mwaminifu katika kila neno Analosema? Kwa nini huchagua kutumia maneno fulani, na sio mengine? Unajua? Ikiwa sio, inamaanisha kuwa huelewi mapenzi ya Mungu au madhumuni Yake, huelewi muktadha nyuma ya maneno Yake. Ikiwa hulifahamu jambo hili, basi unawezaje kuupata ukweli? Kuufikia ukweli kunamaanisha kuwa unaelewa mapenzi Yake kupitia katika kila neno ambalo Anasema. Mara unapoelewa, unaliweka katika vitendo. Unaishi kwa kudhihirisha neno la Mungu, na kulifanya kuwa uhalisia wako. Ni hapo tu, ndipo unaweza kusema kwamba unaufahamu ukweli kwa kweli. Ni wakati tu unapokuwa na ufahamu wa kina wa neno la Mungu ndipo unaweza kuushika ukweli kwa kweli. Unalielewa tu neno la Mungu kwa kiwango cha juu juu. Kwa mfano, unasema, "Mungu Anataka tuwe waaminifu na sio wadanganyifu; kwa hiyo, lazima tuwe waaminifu." Lakini kwa nini Mungu anataka watu wawe waaminifu na sio wadanganyifu? Kwa nini Mungu anataka watu wampende? Kwa nini Anahitaji hilo kutoka kwa watu? Kwa nini Yeye hufanya ufafanuzi kama huo? Kila kitu husemwa kutimiza matokeo fulani. Ukweli ambao Mungu anaonyesha unaelekezwa kwa wale ambao wana kiu ya ukweli, wale wanaotafuta ukweli na wale wanaopenda ukweli. Na kwa wale ambao wanajihusisha na barua na mafundisho na wanapenda kutoa hotuba ndefu na za utukufu, hawatapata ukweli kamwe. Wanajidanganya wenyewe. Watu kama hao wana maoni yasiyo sahihi ya kusoma maneno ya Mungu; kama vile msimamo wao haujafungama, vivyo hivyo ndivyo mtazamo wao ulivyo. Watu wengine wanajua tu kuchunguza maneno ya Mungu, kujifunza kile ambacho Mungu anasema kuhusu kubarikiwa na juu ya hatima ya mwisho ya mwanadamu. Ikiwa maneno ya Mungu hayafanani na mawazo yao, wanakuwa hasi na kuacha kutafuta. Hili lina maana kwamba hawana shauku katika ukweli. Yote wanayotaka ni kuchukua njia ya mkato, kutafuta njia za kufanya mema ili waweze kujionyesha vizuri na mwishowe kupata hatima nzuri. Mtu wa aina hii anaweza kula na kunywa maneno ya Mungu, lakini hajapata ukweli. Bado kuna watu wengine ambao hula na kunywa maneno ya Mungu, lakini wanapita tu katika mizunguko; wanafikiri wameupata ukweli kwa kuelewa maana halisi ya maneno ya Mungu. Wao hawana hekima kama nini! Kula na kunywa maneno ya Mungu si sawa na kuufahamu ukweli; kuusoma ukweli si kuwa sawa hasa na kuuelewa ukweli. Neno la Mungu ni ukweli. Hata hivyo, kusoma maneno ya Mungu haimaanishi kwamba utaelewa maana yake hasa na kuupata ukweli. Kula na kunywa maneno ya Mungu ama kutakuletea ukweli au kukuletea barua na mafundisho. Hujui ni nini maana ya kuupata ukweli. Unaweza kuyashikilia maneno ya Mungu katika kiganja cha mkono wako; lakini baada ya kuyasoma, bado unashindwa kuyaelewa mapenzi ya Mungu, unapata tu barua na mafundisho kiasi. Kwanza kabisa, unapaswa kutambua kwamba neno la Mungu sio halisi vile; Neno la Mungu ni lenye kina kabisa. Bila uzoefu wa miaka mingi, unawezaje kulielewa neno la Mungu? Hata sentensi moja itahitaji maisha yako yote kuielewa kikamilifu. Unasoma maneno ya Mungu, lakini huelewi mapenzi ya Mungu; huelewi madhumuni ya maneno Yake, asili yake, matokeo yanayotafuta kutimiza, au kile yatakachotimiza. Wewe huelewi chochote kuhusu mambo haya, kwa hivyo unawezaje kuuelewa ukweli? Unaweza kuwa umepindua kurasa za kitabu mara nyingi; unaweza kuwa umekisoma mara nyingi. Labda unaweza kukariri vifungu vyake vingi kwa moyo, lakini bado hujabadilika; bado hujafanya maendeleo yoyote. Uhusiano wako na Mungu uko mbali na na wenye kufarakana kama ulivyokuwa. Bado kuna vizuizi kati yako na Mungu, kama hapo awali. Bado unaendelea kuwa na shaka Kwake. Sio tu kwamba humfahamu Mungu, lakini unampinga na hata kumkufuru. Unatoa visingizio kwa Mungu na una dhana juu Yake. Katika hali hii, unawezaje kusema kwamba umepata ukweli? Kila mtu ana nakala ya neno la Mungu ambalo anasoma kila siku, na anachukua maelezo kutoka kwa mawasiliano ya ukweli, lakini mwishowe, watu tofauti wanapata matokeo tofauti. Wengine huzingatia mafundisho, wakati wengine wanazingatia kutenda kwao. Wengine wanaona afadhali kujifunza jambo ambalo ni kubwa na la ajabu, wakati wengine wanapenda kujifunza kuhusu hatima ya baadaye ya mwanadamu. Wengine wanapendelea kujifunza maagizo ya utawala, wakati wengine wanatafuta maneno ya faraja. Wengine wanapendelea kusoma unabii, wakati wengine wanapendelea kusoma maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa. Na bado wengine wanapendelea kuwa "wana Wangu." Lakini haya yanawapatia nini mwishowe? Siku hizi, kuna waumini wapya ambao wanasema: "Angalia jinsi neno la Mungu linanavyofariji! 'Wana Wangu, wana Wangu!' Nani mwingine duniani angetupa faraja kama hiyo?" Hata hivyo, hawaelewi maneno haya yanalengwa kwa nani, bado hawajaelewa; Na hata baada ya kukubali kazi mpya ya Mungu[a] kwa kipindi cha mwaka mmoja au miwili, watu wengine bado wanakosa kuelewa. Wanasema mambo haya bila hisia yoyote ya aibu, bila kuaibika au kuona haya. Je, hii ndiyo maana ya kuuelewa ukweli? Hata hawaelewi mapenzi ya Mungu, lakini wanadhubutu kuchukua nafasi ya wana wa Mungu! Watu kama hao hujifunza nini kutoka kwa neno la Mungu? Wanachofanya tu ni kueleza vibaya na kulibadili neno la Mungu. Wale wanaokirihishwa na ukweli kamwe hawataupata ukweli, bila kujali ni kiasi gani wanasoma neno la Mungu. Wao ni chukizo kwa ukweli, na hata kama utauwasilisha kwao, hawatazingatia. Wale wanaopenda ukweli, baada ya kusoma maneno ya Mungu, watatafuta na kuyashika mapenzi ya Mungu; watachunguza, na kuwasiliana ukweli na wengine. Ni mtu wa aina hii tu ndiye aliye na matumaini ya kuupata ukweli. Kuna wale wanaopenda kuchunguza maneno ya Mungu. Wao huwa daima wanajishughulisha na jinsi Mungu atavyogeuzwa na wakati Mungu atakapoondoka hatimaye. Daima wao hujishughulisha kuhusu siku ya Mungu, lakini wanakosa shughuli yoyote kuhusu maisha yao wenyewe. Masuala haya ambayo wanayajali sana ni shughuli ya Mungu Mwenyewe. Ikiwa wewe huuliza maswali ya aina hii daima, unaingilia amri za utawala za Mungu, unaingilia kati mpango wa usimamizi wa Mungu. Huku ni kukosa akili. Hili ni kosa dhidi ya tabia ya Mungu. Ikiwa kwa kweli unataka kuuliza, ikiwa kwa kweli unataka kujua, ikiwa kwa kweli huwezi kujidhibiti, basi omba kwa Mungu na useme: "Ee Mungu, sitaki kushiriki katika mambo haya, yanahusiana na mpango Wako wa usimamizi. Hayo ni masuala Yako Mwenyewe, na ni lazima nisiingilie kati." Mtu anawezaje kuelewa mambo ya Mungu? Mungu hazungumzi juu ya kazi Yake Mwenyewe au kuhusu mpango Wake wa usimamizi. Ikiwa Mungu hafanyi kitu fulani kijulikane, ina maana kuwa Hataki watu wajue. Kila kitu ambacho Mungu anataka watu wajue kiko katika kitabu cha neno la Mungu, na hakika unapaswa kukisoma. Yote ambayo unahitaji kuelewa yamo ndani ya kitabu hiki; kuna ukweli mwingi ambao unapaswa kuuelewa. Unaweza kuupata ndani ya kitabu hiki. Kuhusu kitu chochote ambacho kimeachwa, hupaswi kuchunguza sana ndani ya mambo haya. Ikiwa kuna kitu ambacho Mungu hakuambii, basi bila kujali jinsi unavyochunguza sana, haina maana. Kila kitu unachopaswa kujua, Mungu amekwisha kukujulisha. Kitu chochote ambacho hupaswi kujua, Mungu hatasema au kukifanya kijulikane. Leo, wengi wenu hamjapata kuingia katika njia sahihi. Hujui hata jinsi ya kusoma neno la Mungu, lakini bado wewe ni mzembe katika kazi zenu. Ili uuelewe ukweli, bado una njia ndefu ya kwenda. Je, unaweza kupata ukweli kama husomi kwa makini neno la Mungu na kujiwekeza katika kazi yako?
Tanbihi:
a. Nakala ya awali inaacha "kazi mpya ya Mungu."
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo
Yaliyopendekezwa: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni