3/03/2018

7. Katikati ya Maafa Niliiona Tabia ya Haki ya Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Kanisa
Li Jing, Beijing
7 Agosti, mwaka wa 2012
Siku hiyo, ilianza kunyesha asubuhi. Nilikwenda kwa mkutano nyumbani mwa ndugu mmoja, wakati mvua ilipoendelea kuongezeka zaidi na zaidi kwa uzito. Kufikia alasiri ilikuwa ikinyesha kana kwamba ilitoka mbinguni moja kwa moja. Wakati tulipomaliza mkutano wetu, mvua ilikuwa imeingia katika ua wa ndugu yangu, lakini kwa sababu nilikuwa na wasiwasi juu ya familia yangu, nilijitahidi kwenda nyumbani. Nusu ya barabara huko, baadhi ya watu waliokimbia hatari waliniambia, "Je, si wewe unatoroka, bado unakwenda nyumbani?" Nilipofika nyumbani, mtoto wangu aliniuliza, "Je, mafuriko hayakukuzoa?" Ni hapo tu nilipojua kwamba sikuwa na Mungu moyoni mwangu. Muda mfupi baadaye, mume wa dada jirani yangu akapanda juu paani, na kuona kwamba nyumba zisizokuwa mbali na yetu zilikuwa zimezolewa. Mkondo ulikuwa unaendelea kuimarika zaidi, na mume wa dada huyo akasisitiza kuwa wampeleke mtoto wao hadi mlimani, lakini huyo dada hakutaka kwenda. Sisi dada wachache tulijadiliana kati yetu wenyewe, kwamba mume wa dada huyo kuhojiana jinsi hii kulikuwa na mapenzi ya Mungu; ni hapo tu tulipomfuata kwa nyumba ya reli juu ya mlima kukesha huko. Huko, tulisikia kutoka kwa wale waliokimbia maafa jinsi maji ya mafuriko yalivyokuwa ya ghasia, na jinsi watu walivyotawanyika pande zote; wengine walikuwa wamepanda paa, baadhi yao walizolewa, wengine walizuiwa na miti ...
Siku iliyofuata nilikwenda kumwona dada fulani. Nyumba yake ilikuwa kando ya mto, barabara kubwa ikiwa mbele yake na mto nyuma. Nyumba yake ilikuwa kabisa katikati ya pande mbili za mafuriko ya maji zilikokutanika. Wakati mafuriko yalipokuja, dada huyu alimwomba Mungu, na kumtegemea Yeye. Maji yalizoa nyumba zingine zote katika mstari wake, yakiziacha yake na ya mwingine mmoja tu bila kudhurika wakati akilala usingizi wa pono usiku. Kwa kweli niliona kwamba wakati mtu ana ulinzi wa Mungu, mtu anaweza kupumzika kwa utulivu katika moyo wake.
Dada mmoja alikuja kuwatafuta shemasi aliyekuwa mkuu wa masuala ya jumla, na mimi, na tukaenda kuikagua nyumba iliyokuwa na mali ya kanisa. Kwa sababu maji yalikuwa yamezoa daraja na barabara, tungeweza tu kufika huko kwa kuzunguka njia ndefu. Kufuata njia, kwa kuangalia kijiji "kilichoporwa", pamoja na miporomoko ya ardhi na mtiririko wa matope na miamba, lilikuwa kweli tukio la kusikitisha; kila mahali uharibifu ulionekana. Tulitembea mbele na kuangalia pande zote, na kuona mahali ambapo nyumba za baadhi ya ndugu wa kiume na wa kike zilikuwa zimezolewa, na baadhi ya zingine zilikuwa zimesalia zikisimama. Zile zilizosalia zote zilikuwa za ndugu wa kiume na wa kike waliotimiza kazi zao. Hili lilinionyesha kwamba wakati watu wanamwamini Mungu, ni wakati tu wanapotafuta ukweli na kutimiza majukumu yao watakapopata ulinzi wa Mungu, na kuokoka katikati ya maafa. Katika kijiji kimoja, kulikuwa na nyumba mbili tu zilizosalia, ya ndugu mmoja mzee, na nyumba moja nyingine. Wakati maji ya mafuriko yalipofika, ndugu huyo mzee aliona kwamba mafuriko yangeiangusha nyumba yake, hivyo kutoka juu ya mlima alipiga ukelele kwa sauti mara mbili, "Mungu! Vitabu vyangu vya neno la Mungu viko ndani!" Kisha akaona jinsi maji ya gharika yalivyoiacha nyumba yake kusalia, na vitabu vya neno la Mungu vilihifadhiwa pia. Kulikuwa na dada ambaye nyumba yake ilikuwa mahali pa kukutana, na ambaye alitimiza kikamilifu kazi yake daima. Ingawa maji yalifurikia mwili wake wote, hakupatwa na madhara hata kidogo. Mafuriko yalizoa mtoto wake, lakini alinyakuliwa na mtu asiyeamini na hakuzolewa hata hivyo. Dada mmoja mzee aliona kuwa maji yalikuwa karibu na mlango, kwamba yalikuwa tayari yamezoa bustani ya mboga ambayo haikuwa mbali na nyumba yake. Kwa hiyo aliomba kwa Mungu, na maji, ambayo yalikuwa yamevunja mabwawa yaliyokuwa imara kwa miaka mingi, yalielekezwa kwingine, na kuiacha nyumba yake ikisimama. Kulikuwa na dada wawili ambao hawakutafuta, na maji ya mafuriko yaliacha nyumba zao zikisimama, lakini yalizoa nyuga. Dada mmoja hakuweza kulikubali jukumu lake la kuhudhuria, alisema familia yake ilipaswa kuimarisha nyumba, na hivyo akawafukuza ndugu na dada; vitabu vyake vya neno la Mungu vilikuwa vimeondolewa. Kulikuwa na dada mwingine ambaye, ingawa alitimiza wajibu wake, alisema kuwa "katika moyo wangu mimi sitaki." Wakati wa maafa alikuwa amezingirwa na maji na kumezwa na mtiririko wa matope na miamba, na jiwe likachana shimo katika matumbo yake. Alilia tena na tena kwa Mungu, na maji yakamuosha kwa mtiririko hadi kwa mti mkubwa, yakimzuia na kuyaokoa maisha yake. Jeraha lake likawa limeambukizwa, na alibidi kufanyiwa upasuaji mwingine. Kulikuwa ndugu mwingine pia aliyetenda kama alivyotaka; wakati wowote kulipokuwa na kitu ambacho kilihitajika kufanywa nyumbani, hangetimiza wajibu wake. Wakati wa maafa aliteseka kwa uzito kupita wote; mafuriko yalizoa nyumba zake zote mbili, zikimwacha na vyumba viwili visivyoweza kukaliwa. Kati ya vitabu vya neno la Mungu, hakuna hata moja kilichobaki. Ndugu huyu pia alikuja kujua kwamba huu ilikuwa ni upendo wa Mungu, na hakutoa lawama.
Wimbo ya maneno ya Mungu "Mungu ni Msingi wa Pekee wa Kuwepo Kwa Mtu" husema: "Wakati maji yanapowameza wanadamu wazima, Mungu huwaokoa kutoka kwa maji yaliyotuama na kuwapa nafasi ya kuishi upya. Wanadamu wanapopoteza imani yao ya kuishi, Mungu huwavuta kutoka kwa ukingo wa kifo, akiwapa ujasiri wa kuishi, ili wamchukue Mungu kama msingi wa kuwepo kwao. Wanadamu wanapomuasi Mungu, Yeye huwafanya kumjua katika uasi wao. Kutokana na asili ya zamani ya ubinadamu na kutokana na huruma ya Mungu, badala ya kuwaua binadamu, Mungu huwaruhusu kutubu na kuanza upya. Wanadamu wanapopatwa na kiangazi, Mungu huwatoa kifoni mradi wamesalia na pumzi moja, kuwazuia kudanganywa na Shetani. Watu wameona mikono Yake mara ngapi; watu wameona uso Wake mkarimu mara ngapi, kuuona uso Wake wa tabasamu; na wameona adhama Yake mara ngapi, kuiona ghadhabu Yake. Ingawa ubinadamu haujawahi kumjua Yeye, Mungu hataukamata udhaifu wao kufanya matata yasiyohitajika. Kupitia ugumu wa ubinadamu, hivyo Mungu ana huuhurumia udhaifu wake. Ni kwa sababu ya kuasi kwa wanadamu, kutokuwa kwao na shukrani, ndiko kunakomfanya Mungu awaadibu kwa viwango tofauti." Kati ya maafa haya, tuliona uweza wa Mungu na wema wa ajabu, jambo ambalo liliimarisha zaidi imani yetu katika kutembea njia ya baadaye. Wakati Mungu alipotoa ghadhabu yake kubwa, tuliona tabia ya Mungu, ambayo haiwezi kukosewa. Ni kwa sababu tu ya uasi wa watu, na kutokuwa kwao na shukrani, ambapo Mungu huwapa watu viwango tofauti vya adabu. Hata hivyo, Mungu hutumia maafa kutufanya tujirudi; Yeye hawaui watu, lakini Anawaruhusu watu kutubu na kuanza upya. Maafa haya yametufanya tuone haki ya Mungu, kuona upendo Wake, wokovu Wake, na hata zaidi ya hivyo yamenifanya nione uweza wa Mungu na utawala Wake. Wale watu ambao kwa kweli hutafuta ukweli, ambao wako tayari kutimiza majukumu yao na kutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu, hupata utunzaji wa Mungu na ulinzi. Wale ambao ni wazembe, wanaolalamika na kupinga, ambao hawataki kufanya kazi zao au kutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu, hupata adhabu wanayostahili. Ni wajibu ambao hutulinda! Ni wajibu ambao hutubariki! Mungu atupe imani, ujasiri, nguvu na hekima ili kutuwezesha, kwa barabara ya baadaye, kubaki wenye bidii na utendaji mwema katika kukamilisha kile Alichotuaminia, na kuturuhusu, kwa kila wajibu, kufanya vizuri iwezekanavyo.
Tungependa kuusema ukweli huu ulioshuhudiwa na macho yetu kwa kila mtu: Mungu ndiye msingi wa pekee wa kuwepo kwetu. Utukufu wote, utajiri, umaarufu na bahati katika dunia ni wa kupita kama mawingu ya muda mfupi. Wakati ambapo maji ya mafuriko yaliyameza maisha ya ubinadamu, maisha ya mwanadamu yalikuwa yasiyo ya maana sana na yalikuwa dhaifu. Hata watu matajiri na maarufu sana hawakuwa na nguvu. Tulipoomba msaada, ni Mungu peke yake angeweza kunyosha mkono wa wokovu, na kuwavuta wale wanaomwamini kwa kweli kutoka kwa poromoko la kifo. Ndugu zangu, tafadhali shikeni kazi ambayo Mungu hutupa. Hebu, katika siku za mwisho, tuwe waaminifu kabisa, na kutoa nguvu zetu wenyewe kwa upanuzi wa injili ya ufalme.
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni