6/09/2018

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kujijua Mwenyewe Hasa Ni Kujua Asili ya Binadamu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kujijua Mwenyewe Hasa Ni Kujua Asili ya Binadamu 

La muhimu katika kufikia badiliko la tabia ni kujua asili ya mtu mwenyewe, na hili ni lazima litoke kwa ufunuo na Mungu. Ni katika neno la Mungu tu ambapo mtu anaweza kujua asili yake ya kutia kinyaa, afahamu katika asili yake mwenyewe sumu mbalimbali za Shetani, atambue kuwa yeye ni mjinga na mpumbavu, na atambue dalili dhaifu na hasi katika asili yake mwenyewe. Mara haya yanapojulikana kikamilifu, na unaweza kwa hakika kunyima mwili, daima kutekeleza neno la Mungu, na kuwa na mapenzi ya kujiwasilisha kikamilifu kwa Roho Mtakatifu na kwa neno la Mungu, basi umeianza njia ya Petro. Bila neema ya Mungu, kama hakuna kupata nuru na mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu, ingekuwa vigumu sana kuitembea njia hii, kwa sababu watu hawana ukweli na hawawezi kujisaliti wenyewe. Kuitembea njia ya kukamilishwa ambayo Petro aliitembea, hasa mtu ni lazima awe na dhamira ya kufanya hivyo, anapaswa kuwa na imani, na amtegemee Mungu. Zaidi ya hayo, yeye lazima ajiweke chini ya kazi ya Roho Mtakatifu, na katika kila kitu asichepuke kutoka kwa neno la Mungu. Hivi ndivyo vipengele kadhaa muhimu, ambavyo hakuna hata kimoja kinachoweza kukiukwa. Ni vigumu sana kujitambua mwenyewe ndani ya uzoefu. Bila kazi ya Roho Mtakatifu ni vigumu sana kuingia ndani yake. Kuitembea njia ya Petro mtu lazima azingatie juu ya kujijua mwenyewe, na juu ya kuufikia badiliko la tabia. Paulo aliitembelea njia ambayo haikutafuta uzima, na haikulenga kujijua. Paulo hasa alisisitiza kazi, sifa nzuri na ushawishi wa kazi. Motisha yake ilikuwa kupata baraka za Mungu badala ya kazi na mateso yake, kupokea thawabu kutoka kwa Mungu. Motisha yake haikuwa sahihi. Yeye hakusisitiza uzima, wala hakutilia mkazo juu ya badiliko la tabia. Alilenga tu juu ya tuzo. Kwa kuwa alitafuta lengo lisilofaa, njia aliyoitembelea bila shaka pia ni mbaya. Hili limeletwa na majisifu na majivuno yake. Kwa dhahiri, yeye hakuwa na ukweli wowote, na wala hakuwa na dhamiri au sababu. Katika kuwaokoa watu, Mungu hasa hubadilisha watu kwa kubadilisha tabia zao. Kusudi la maneno ya Mungu ni kufikia katika watu matokeo ya badiliko katika tabia, kiasi kwamba watu wanaweza kumjua Mungu, wajiweke chini Yake, na kumwabudu Yeye kwa njia ya kawaida. Hili ndilo lengo la maneno ya Mungu na la kazi Yake. Njia ya Paulo ya kutafuta ni ukiukaji wa moja kwa moja na katika mgongano na nia ya Mungu. Ni kuwa na malengo yanayopingana kabisa. Njia ya Petro ya kutafuta, hata hivyo, inafanana kabisa na nia ya Mungu, ambayo hasa ni matokeo ambayo Mungu hutamani kutimiza kwa wanadamu. Kwa hiyo njia ya Petro imebarikiwa na hupokea sifa ya Mungu. Kwa sababu njia ya Paulo ni ukiukaji wa nia ya Mungu, Mungu kwa hiyo huichukia kabisa, na huilaani. Kuitembelea njia ya Petro mtu lazima aijue nia ya Mungu. Kama mtu anaweza kwa kweli kuielewa kikamilifu nia ya Mungu katika maneno Yake, ambayo inamaanisha kukielewa kile Mungu anachotaka kukifanya kwa mwanadamu na hatimaye yale matokeo Yeye hutamani kutimiza, ni hapo tu ambapo mtu anaweza kufahamu sawasawa ni njia ipi ya kufuata. Kama huielewi kikamilifu njia ya Petro, na una tamaa tu ya kuifuata, hutakuwa na uwezo wa kuianza. Kwa maneno mengine, unayajua mafundisho mengi, lakini hatimaye umeshindwa kuingia katika ukweli. Ingawa kuingia kwako kunaweza kuwa kwa juujuu, huwezi kutimiza matokeo ya kweli. Siku hizi watu wengi wana ufahamu wa juujuu sana wa wao wenyewe. Hawajapata kujua wazi mambo ambayo ni sehemu ya asili yao kamwe. Wao wanajua tu dalili chache mbovu zao wenyewe, mambo ambayo huenda wakafanya, au makosa yao machache, na hivyo wanaamini kuwa wanajijua wenyewe. Wakitii zaidi sheria chache, kuhakikisha kwamba hawana makosa katika maeneo fulani, na wafaulu kuepuka kufanya makosa machache, huwa basi wanajiona kuwa na ukweli katika imani yao kwa Mungu na kwamba wataokolewa. Haya ni mawazo ya binadamu kabisa. Je, ukishikilia haya, kwa kweli utaweza kutofanya makosa? Je, badiliko la kweli wa tabia umefikiwa? Je, kwa kweli umeishi kwa kudhihirisha mfano wa mwanadamu? Je, unaweza kumridhisha Mungu kweli? Hakika sivyo, hili ni kwa uhakika. Imani katika Mungu hufanya kazi tu wakati mtu ana viwango vya juu, kupata ukweli na mabadiliko katika tabia ya maisha yake. Kwa hivyo kama ujuzi wa mtu juu yake mwenyewe ni wa juujuu sana, haitawezekana kutatua matatizo, na tabia yake ya maisha haitakuwa na mabadiliko kabisa. Ni muhimu kujijua mwenyewe kwa ngazi ya kina, ambayo inamaanisha mtu kuijua asili yake mwenyewe, na kujua ni vipengele vipi vimejumuishwa katika asili ya mtu mwenyewe, kutoka ambapo vipengele huibuka na jinsi vinavyokuja kuwa. Aidha, unaweza kuchukia mambo haya kweli? Je, umeona nafsi yako mwenyewe mbaya na asili yako mbovu? Ikiwa mtu kwa hakika anaweza kuuona ukweli kujihusu mwenyewe, basi ataanza kujichukia mwenyewe kabisa. Wakati unapojichukia mwenyewe kabisa na kisha unatenda neno la Mungu, utakuwa na uwezo wa kunyima mwili, na kuwa na nguvu ya kutekeleza ukweli bila shida. Kwa nini watu awali walikuwa na uwezo wa kuufuata mwili? Kwa sababu walijiona kuwa wazuri kiasi. Walijihisi kuwa waadilifu na waliothibitishwa, bila kuwa na makosa, hasa sahihi kabisa. Kwa hiyo wao wangetenda kwa dhana kuwa haki ilikuwa upande wao. Wakati mtu anapotambua asili yake ya kweli ilivyo, jinsi ilivyo mbaya, jinsi inavyostahili kudharauliwa, na jinsi ilivyo ya kusikitisha, basi hajivunii nafsi yake mwenyewe sana, hajigambi ovyo ovyo sana, hajifurahii kama alivyokuwa hapo awali. Yeye huhisi, "Napaswa kuwa mwenye ari na mwenye kuhusika na mambo halisi, na kutenda neno la Mungu kiasi. Kama sivyo, siwezi kufikia kiwango cha kuwa mwanadamu, na nitaona aibu kuishi mbele ya Mungu. "Kwa hakika yeye hujiona kuwa hafifu, kama kweli asiye na maana. Kwa wakati huu ni rahisi kwake kutekeleza ukweli, naye huonekana zaidi kama mwanadamu. Ni pale tu mtu kwa hakika hujichukia kabisa ndipo anapoweza kunyima mwili. Ikiwa mtu hajichukii kabisa, hataweza kunyima mwili. Mtu kujichukia kunajumuisha mambo machache: kwanza, kujua asili yake mwenyewe; pili, kujiona kama yeye ni mwenye shida na wa kudharaulika, kujiona kuwa mdogo sana na asiye na maana, na kuona nafsi yake kuwa yenye kudharaulika, nafsi yake chafu. Mtu anapoona kikamilifu kile alicho kwa hakika na matokeo haya yakafikiwa, basi kwa kweli hujijua mwenyewe, na tunaweza kusema kwamba amekuja kujijua mwenyewe kikamilifu. Ni hapo tu anapoweza kwa hakika kujichukia mwenyewe, kufikia hata kujilaani mwenyewe, akihisi kwa kweli kwamba amepotoshwa sana na Shetani, kiasi kwamba hafanani tena na mwanadamu. Kisha siku moja, wakati tishio la kifo cha karibu sana linapoonekana, yeye huhisi, "Aa! Ni adhabu ya haki ya Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye haki. Kwa hakika mimi lazima nife! "Wakati huu, yeye hatalalamika, wala kumlaumu Mungu, akihisi tu kwamba yeye ni wa kudharaulika, mchafu sana na mpotovu, kwamba yeye ni lazima aangamizwe na Mungu na roho kama yake haifai kuishi duniani, na hivyo hatapinga, sembuse kumsaliti, wala kulalamika dhidi ya Mungu. Iwapo yeye hajijui mwenyewe, na bado hujiona kuwa mzuri sana, wakati kifo kinapomtishia, yeye huhisi, "Nimeamini katika Mungu vizuri sana. Jinsi nilivyotafuta! Nimejitolea mengi sana, nimeumia hivyo, na hatimaye Mungu ananiuliza nife. Sijui haki ya Mungu iko wapi. Kwa nini Mungu ananiuliza nife? Mtu kama mimi akifa, ni nani atakayeokolewa? Je! Si jamii ya wanadamu itafikia mwisho? "Kwanza, ana dhana juu ya Mungu. Pili, ana malalamiko; hakuna kutii kokote kamwe. Kwa mfano, wakati Paulo alipokaribia kufa, hakujijua mwenyewe. Wakati adhabu kutoka kwa Mungu ilipofika, hakukuwa na muda wa kutubu.
kutoka kwa Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo
Sikiliza zaidi: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu, Chanzo cha Mafanikio ya Umeme wa Mashariki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni