6/15/2018

Ni Nini Ambacho Kimeidanganya Roho Yangu?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa
Xu Lei     Mji wa Zaozhuang, Mkoa wa Shandong
Siku moja nilipokea taarifa juu ya mkutano. Kwa kawaida hili ni tukio la kufurahisha, lakini mara tu nilipofikiria jinsi kazi yangu hivi karibuni ilikuwa machafuko kabisa, sikuweza kujizuia kuhisi wasiwasi. Kama mkuu wangu angejua jinsi sikuwa nimemaliza kazi yoyote yangu, bila shaka angehitaji kunishughulikia, na huenda hata kunibadilisha na mwingine kaziniNingefanya nini basi? Siku iliyofuata nilikwenda kwa mkutano na moyo mzito. Nilipofika huko, nikaona kwamba mkuu wangu alikuwa bado hajafika, lakini baadhi ya wafanyakazi wenzangu walikuwa hapo tayari.  Niliwaza: "Sijui kazi yoyote yao iko katika hali gani. Katika mkutano wa mwisho, niliwasikia wakisema jinsi karibu walikuwa wamefanya kazi yao, na wakati huu lazima kwa kweli wawe wameimaliza yote. Kama wamemaliza kazi yao yote na ni mimi tu ambaye ni mbaya sana, basi niko kwa shida kubwa." Nilishangaa basi kwamba, wakati tulipokuwa pamoja tukizungumza juu ya hali zetu wenyewe za kazi, wengi wa wafanyakazi wenzangu walikuwa wakisema jinsi hawakuwa wamemaliza sehemu fulani za kazi zao. Niliposikia jambo hili, moyo wangu uliokuwa mzito sana kabla kwa ghafla ulihisi wepesi sana. Niliwaza: "Yaonekana kuwa hakuna mtu aliyemaliza kazi yake, sio mimi tu. Hakuna haja ya kuwa na wasiwasi basi. Hatuwezi kubadilishwa sote." Sehemu kubwa ya hisia zangu zisizokuwa na utulivu wakati huo zilitoweka papo hapo.
Nilipokuwa tu nikianza kupata starehe katika hali yangu ya kujifariji, kifungu katika ushirika kutoka hapo juu kilizurura ndani ya mawazo yangu: "Mtu akileta maoni ya kidunia katika familia ya Mungu, basi hizo ni dhana na yanamdharau Mungu. Watu wengi wana maoni sawa juu ya mambo kama wasioamini. Kwa sababu hawana ukweli ndani yao, mara tu wanapofika kwa familia ya Mungu wao hutumia maoni ya kidunia ili kutazama kazi ya familia ya Mungu, kutoa maoni juu ya mambo ya familia ya Mungu, matokeo yake yakiwa ni wao kusita, kujisababisha wao daima kuwa dhaifu na hasi, kushindwa kutafuta ukweli au kulipa gharama. Je, si hili limesababishwa na ujinga wao?" ("Jinsi ya Kujua Dhana za Wanadamu na Hukumu" katika Ushirika na Mahubiri Kuhusu Kuingia kwa Maisha III). Maneno haya yalinifanya nifikiri juu ya mjibizo wangu muda mfupi uliopita. Nilipofikiria jinsi nilivyokuwa sijamaliza kazi yangu, moyo wangu ulijihisi kuwa mzito sana na sikuweza kuacha kuwa na wasiwasi. Lakini nilipojua kwamba wafanyakazi wenzangu pia hawakuwa wamemaliza kazi yao, mara moja nilihisi utulivu, na nikawaza kwa dhamiri nyepesi kwamba sio mimi tu ambaye kazi yake haikuwa imefanikisha chochote. Kama mkuu wetu angekuwa atushughulikie, basi kila mtu angekuwa na mgao wake. Kwa kuwa wengi wetu sana hatukuwa tumemaliza kazi yetu, msimamizi wetu kwa hakika hangetubadilisha wote. Je, si kufikiria kwa aina hii kulitawaliwa na maoni ya Shetani: "Sio dhambi kama kila mtu huitenda"? Si kwa kweli nilikuwa nikitumia maoni ya Shetani kupimia kanuni za kazi ya kanisaNilikuwa nimetumia maoni yenye mantiki ya Shetani kwa kanisa, nikiyatumia kujiliwaza, kujipendeza—lakini si nilikuwa nikijidhuru tu? Kwa kweli nilikuwa kipofu sana na mjinga! Nikifikiria nyuma, kulikuwa na nyakati nyingi nilipokubali utawala wa maoni haya ya Shetani ili kujifariji. Kwa muda mfupi, niliishi katika mwili bila kuingia kwa maisha na, ingawa nilikuwa na wasiwasi juu ya wokovu wangu mwenyewe, nilipoona baadhi ya ndugu wa kiume na wa kike pia kutokuwa wameingia katika ukweli, sikuwa na wasiwasi na niliacha kujihangaisha. Nilidhani kwamba kama watu wengi sana hawakuwa wameingia katika uzima, basi Mungu hangetuchekecha, Angetucheka? Kwa hivyo, niliishi katika hali ya uholela ya kujiingiza, bila kubeba mzigo halisi kwa ajili ya maisha yangu mwenyewe. Nilipokuwa sijaandika makala yoyote kwa muda mrefu na nilikuwa na hisia za kujishutumu mwenyewe, ningewaona wengine ambao pia hawakuwa wameandika chochote, na shutuma katika moyo wangu ingetoweka. Ningewaza: Sio jambo kubwa kutoandika makala na, hata hivyo, sio mimi pekee ambaye hajaandika moja. Wakati sikuona matokeo yoyote kamwe kutoka kwa kazi yangu ya injiliningehisi wasiwasi. Lakini nilipoona kazi ya injili ya wengine bila matokeo yoyote pia, ningehisi utulivu, nikidhanikwamba kila mtu alikuwa jinsi hii, kwamba haikuwa mimi tu ambaye hakumleta mtu yeyote kanisani. ... Wakati huo, niliona kuwa maoni ya Shetani—" Sio dhambi kama kila mtu huitenda"—yalikuwa yamekita mizizi moyoni mwangu sana sana. Chini ya utawala wa maoni haya, nilikuwa daima nikijipendeza nilipokuwa nikitekeleza kazi zangu, sikuwa nikitia bidi yote katika kazi na sikuwa nikitafuta matokeo bora zaidi. Haikusababisha hasara kubwa tu kwa kazi ya kanisa, lakini pia iliisababishia hasara kubwa sana kwa maisha yangu mwenyewe. Kwa sababu nilikuwa nimekubali sumu ya dhana yenye kosa ya Shetani—" Sio dhambi kama kila mtu huitenda"—Sikuwa nimechukua mzigo halisi katika kazi yangu kwa kanisa, mara zote nikiridhika na kazi ya shingo upande na sikuwa nikitafuta matokeo yoyote; nilikuwa nimepoteza dhamiri na mantiki ambavyo kila mmoja wa viumbe wa Mungu ni lazima wawe navyo. Kwa sababu nilikuwa nimekubali pingu za maoni ya Shetani ya " Sio dhambi kama kila mtu huitenda," daima nilikuwa nikiboronga tu katika harakati za mimi kumfuata Mungu. Sikuwa nimechukulia imani yangu kwa Mungu kuwa ya thamaniyoyote hata kidogo, sikutafuta ukweli kwa bidii, sikujali kuhusu au kuzingatia kuingia kwangu mwenyewe kwa maisha; sikuwa na lengo la kufuatilia, sikuwa na mwelekeo katika maisha. Niliboronga tu na kuishi kwa kufanya kiwango cha chinisana. Ni hapo tu nilipoona kwamba nilikuwa nimedhuriwa vibaya sana na maoni ya Shetani ya "Sio dhambi kama kila mtu huitenda" na nilikuwa nimepoteza dhamiri kabisa, mantiki, uadilifu na heshima ambazo mtu wa kawaida anapaswa kuwa nazo. Nikifikiria kwa makininilikuwa nikiishi ndani ya mawazo yangu na dhana zangu wakati wote, nikiamini "Sio dhambi kama kila mtu huitenda," kwamba kama watu wengi wakifanya dhambi hiyo basi Mungu atatuacha tuponyoke kupitia kwa wavu na bila kumfanya mtu yeyote awajibike, bila kufikiria kamwe kama Mungu angewatendea watu kwa njia hii au la. Wakati huo, sikuweza kujizuia kufikiria maneno ya Mungu, ambayo yanasema: “Anayeasi kazi ya Mungu atatumwa kuzimu; nchi yoyote inayoasi kazi ya Mungu itaangamizwa; taifa lolote linaloinuka kupinga kazi ya Mungu litafutwa kutoka dunia hii, na litakoma kuwepo” (“Mungu Anaongoza Majaliwa ya Wanadamu Wote” katika Neno Laonekana katika Mwili). Maneno ya Mungu yalifanya nitetemeke kwa hofu, kwa kuwa niliona kwamba tabia ya Mungu haitamruhusu mtu yeyote afanye kosa na kwamba Yeye hatategemeza uamuzi Wake juu ya kama kumwangamiza mwanadamu kwa msingi wa idadi ya wenye dhambi au la. Nikifikiria nyuma, watu wa siku za Nuhu walikuwa wenye dhambi na wazinzi na Mungu aliyaangamiza yote yalioishi wakati huo ila familia ya Nuhu. Uharibifu Wake wa mji wa Sodoma pia ulikuwa hivi. Sasa watu katika siku za mwisho wamefikia bilioni kadhaa, idadi iliyozidi kwa mbali ile ya siku za Nuhu. Lakini Mungu hajaweka sheria Yake kando na kuonyesha rehema kwa sababu kuna watenda dhambi wengi katika siku za mwisho; kwa watu hawa Mungu ana chuki tu, adhabu, karaha na kukataliwa, kwa kutumia kila aina ya maafa ya asili na misiba ya kibinadamu ili kuwaangamiza hatua kwa hatua. Mwishonwe, mbali na wachache ambao wameokolewa, Mungu atawaangamiza kabisa wale wote watakaobaki. Ni hapo tu nilipoona jinsi nilivyokuwa nimeelewa kidogo sana tabia ya Mungu. Sikuelewa kwamba Mungu ni mwenye haki, Mungu nimtakatifu ambaye hamruhusu mtu afanye kosa, kiasi kwamba nilikuwa nimeduwazwa na uongo wa Shetani na nilikuwa nimeangukia mipango yake ya hila. Leo, kama haingekuwa kupata nuru ya Mungu, ningekuwa bado ninaishi katika dhambi bila kufikiri kuwa ilikuwa dhambi, mwishowe nikiadhibiwa na Mungu bila hata kujua kwa nini ningekufa—kwa kweli ilikuwa hatari sana!
Ninamshukuru Mungu kwa kunipa nuru Yake ambayo ilinifanya niamke kutoka kwa udanganyifu wa Shetani na kutambua kwamba " Sio dhambi kama kila mtu huitenda" ilikuwa kabisa ni dhana ya uasi ya Shetani. Ulikuwa mpango wa hila wa Shetani wa kuwadhuru na kuwaangamiza wanadamu. Aidha, niliona kwamba Mungu ni mwenye haki, kwamba tabia ya Mungu haitaruhusu kosa lolote, kwamba Mungu atategemeza uamuzi wa mwisho kwa upande wa wanadamu kama wana ukweli au la, na kwamba Yeye hataonyesha huruma ya kipekee kwa mtu ambaye hana ukweli. Kuanzia leo kwendelea, napenda kufanya jitihada kabisa katika kutafuta ukweli, katika kutafuta kumjua Mungu, kutegemeza mtazamo wangu wa mambo yote kwa maneno ya Mungu, kutumia maneno ya Mungu kama kiwango ambacho kwacho nitajifanyia matakwa makali, kuacha uongo wote na udanganyifu wa Shetani, na kutafuta kuwa mtu anayeishi kwa kutumainia ukweli.

Utukufu wote Uwe kwa Mwenyezi Mungu!

kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo Juzuu ya 1
Kuhusu Sisi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni