7/19/2018

Filosofia ya Shetani Inanasa na Kuharibu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, kanisa
Wu You    Mji wa Hechi, Mkoa wa Guangxi
Wakati fulani uliopita, kanisa lilinipangia kuishi na familia mwenyeji kwa sababu za kazi. Wakati nilipofanya ushirika kwanza na ndugu wa kiume na wa kike wa familia hii mwenyeji, walisema, "Tunaogopa sana kuomba katika ushirika. Tunajua cha kusema tunaposali peke yetu, lakini linapokuja suala la kuomba wakati wa ushirika, hatujui hasa cha kusema." Niliposikia hili, nilijiwazia, "Tusiposali wakati wa ushirika hatutaweza kupokea kazi ya Roho Mtakatifu, na mawasiliano hayatakuwa na ufanisi. Ni lazima tuombe!" Lakini hata hivyo nikafikiria tena, nikifikiri kuwa kama kwa kweli waliogopa kuomba, si wangetunga maoni kunihusu kama ningesisitiza kwamba waombe? Ili kutimiza wajibu wangu katika kuhariri makala, ningehitaji kukaa na familia mwenyeji kwa muda mrefu. Na je kama wangetunga maoni kunihusu na hawakutaka kunikaribisha kwa sababu sikukubaliana na matakwa yao? Nadhani ni lazima nikubaliane na matakwa yao. Hivyo, wakati wa kipindi cha mwezi uliofuata, hatukuomba wakati wa ushirika. Hii ilisababisha mawasiliano juu ya maneno ya Mungu kuwa ya kuchusha na yasio na ladha, na bila kabisa kunurishwa kwa Roho Mtakatifu. Mara nyingi tungeenda nje ya mada. Hatua kwa hatua, hali ya ndugu wa kiume na wa kike ikawa ndogo kuliko kawaida, na hawakuwa tayari kuwa na ushirika. Hata wakati tulikuwa na ushirika, daima walikuwa wakisinzia na katika maisha ya kila siku walishindwa kuweka umuhimu juu ya kula na kunywa neno la Mungu. Walitazama runinga wakati wowote walipokuwa na muda, na hawakuwa na upendo vivyo kwangu, hata wakisita kunizungumzia. Nikikabiliwa na hali hii, nilihisi uchungu sana na kuchanganyikiwa: nilifuata matakwa yao katika kila kitu, na sikuwakosea. Kwa nini walikuwa jinsi hii?
Wakati tu nilipokuwa nimekanganywa sana na hali hii, maneno ya Mungu yalinipatia nuru: “Iwapo huna uhusiano unaofaa na Mungu, haijalishi unachofanya kudumisha uhusiano wako na watu wengine, haijalishi jinsi gani unafanya kazi kwa bidii au ni nguvu kiasi gani unaweka ndani yake, bado ni ya falsafa ya mwanadamu ya maisha. Unadumisha nafasi yako miongoni mwa watu kupitia mtazamo wa mwanadamu na falsafa ya mwanadamu ili kwamba wakupe wewe sifa. Hauundi uhusiano unaofaa na watu kulingana na neno la Mungu. Iwapo hutilii maanani uhusiano wako na watu lakini unadumisha uhusiano unaofaa na Mungu, ikiwa uko tayari kumpa Mungu moyo wako na ujifunze kumtii, kwa kawaida sana, uhusiano wako na watu wote utakuwa unaofaa. … Uhusiano unaofaa kati ya watu unaundwa juu ya msingi wa kumpa Mungu moyo wako; haufanikishwi kupitia jitihada za binadamu” (“Ni Muhimu Sana Kuanzisha Uhusiano wa Kufaa na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kupitia maneno ya Mungu ghafla niliona mwanga. Kama ilivyoelekea kuwa, hali hii iliibuka kwa sababu kwa upofu nilikuwa nimelenga kudumisha uhusiano wa mwili kati ya watu, na sio kulenga kujenga uhusiano wa kawaida na Mungu. Nikifikiria nyuma juu ya jinsi nilivyoelewana na familia yangu mwenyeji, ili kuwafanya wawe na taswira nzuri kwangu, na wawe radhi kunikaribisha, niliwafuata katika kila kitu na nilifanya kila kitu kuwafadhili, bila kuzingatia kanuni za kweli au kama vitendo vyangu vingewafaidi. Nilipopata habari juu ya hofu yao ya kuomba wakati wa ushirika, sikuwasiliana nao kuhusu ukweli ufaao ili kuwasaidia kuelewa maana na umuhimu wa kuomba; badala yake, ili kulinda maslahi yangu mwenyewe, niliwasikia na nilifikiria juu ya hamu yao ya kutosali wakati wa ushirika, ambayo ilifanya kuingiliana kwetu kuwe uhusiano wa kimwili kabisa wa kibinadamu. Kutokana na kwamba hakukuwa na sala, kutafuta, au kukabidhi, hakukuwa na njia ya kufikia upataji nuru wa Roho Mtakatifu na uongozi Wake wakati wa ushirika, au kupata riziki kupitia kula na kunywa neno la Mungu. Kama matokeo, hali zetu zikawa chini ya kawaida, na hatukuweza kudumisha uhusiano wa kawaida. Nilikuwa najua vyema umuhimu wa sala. Sala huwasaidia watu kusisimuliwa na Roho wa Mungu, na ni njia ya Roho Mtakatifu kufanya kazi. Sala inaweza kutusaidia kupata nuru zaidi kutoka kwa Roho Mtakatifu ili kuelewa ukweli vyema. Aidha, kuomba kabla ya ushirika daima ni njia ya kuonyesha mahali pa Mungu katika moyo wa mwanadamu, kuonyesha kwamba mwanadamu humheshimu Mungu juu ya yote. Lakini bado nilikuwa nikifuata falsafa ya maisha ya Shetani—"Kuwa na hekima ya kidunia kwa ajili ya kudumu kibinafsi"—kufuta maombi ili kudumisha uhusiano wangu. Hili lilionyesha kwamba sikuwa na nafasi ya Mungu kabisa ndani ya moyo wangu, na kwamba nilikuwa nikitawaliwa kabisa na falsafa ya Shetani ndani. Daima nilijitahidi kudumisha uhusiano wa kimwili na watu—tabia hii ilitokana na kukubali kwangu kwa jumla filosofia ya kishetani "Kuwa na hekima ya kidunia kwa ajili ya kudumu kibinafsi." Ilipotosha moyo wangu na nafsi yangu, kunifanya kuwa mwoga, wa ubinafsi na wa kudharauliwa, kunisababisha kuwa mdhalimu, na kutoweza kuweka ukweli katika matendo. Niliweza kukumbuka mara nyingi katika siku za nyuma wakati nilipokuwa nikimpinga Mungu nikimotishiwa na kujilinda: Nilipokuwa nikiongoza kanisa, niliwaona watu wakieneza dhana fulani, kueneza uhasi, kuvuruga maisha ya kanisa, lakini sikuthubutu kuwazuia, kwa hofu kwamba kama ningesema jambo lingehatarisha maslahi yangu. Katika kusimamia kazi ya injili, nilijiondoa punde ndugu wa kiume na wa kike walipolalamika kuwa mambo yalikuwa magumu sana, na sikuthubutu kuwauliza zaidi, nikihofia ningewakosea na kupoteza nafasi yangu katika mioyo yao. Kwa kufanya hivyo, nilisababisha kazi yetu ya injili kuwa hafifu. Nikifanya kazi na kundi lililohusika na kuhariri makala, niligundua kwamba dada niliyekuwa nikifanya kazi naye hakuwa makini kuhusu kazi yake lakini niliogopa kumwambia, kwa hofu kwamba angekosa furaha na kukuza chuki dhidi yangu ambayo ingeathiri upatanifu wetu. … Wakati huu, niliona wazi kwamba katika kila kitu nilichokifanya, lengo langu daima lilikuwa kwa mtazamo wa wengine kunihusu na tathmini yao kwangu. Nililinda nafasi yangu na picha katika mioyo ya watu wengine, na kuzingatia faida zangu na hasara. Inaweza kusemwa kuwa niliishi kabisa kwa filosofia ya Shetani ya "Kuwa na hekima ya kidunia kwa ajili ya kudumu kibinafsi." Ilikuwa imekuwa kanuni ya vitendo vyangu, msingi wa jinsi nilivyofanya kazi kama mtu. Mungu huwauliza watu kujitolea ili kupigania haki na ukweli, kuwa na ujasiri wa kutotii kwa udhalimu wa nguvu za giza, na kusimama imara, si kufuata mkondo, au kuwa na udhalimu. Hata hivyo, falsafa hii ya kishetani ya "Kuwa na hekima ya kidunia kwa ajili ya kudumu kibinafsi" inawaongoza watu vibaya kuwa wenye ubinafsi na kukubali kushindwa na majeshi ya giza. Hawazingatii kanuni au msimamo katika chochote ambacho wanafanya, lakini tu kama kitakuwa cha manufaa ya kibinafsi kwao. Hii filosofia ya Shetani ya "Kuwa na hekima ya kidunia kwa ajili ya kudumu kibinafsi " ni kanuni hasi ambayo huupinga ukweli kabisa—chombo kinachotumiwa na Shetani kuwapotosha watu. Katika kuishi kwa kanuni hii, watu huwa tu wadanganyifu zaidi, wenye hila, wenye ubinafsi, na wenye kustahili dharau. Hatua kwa hatua wao hupoteza hizo sifa ambazo hufanya mwanadamu halisi. Falsafa ya Shetani hunasa na kuharibu. Sitaki kuishi na falsafa hii tena! Mara nilipotambua haya yote, niliwasiliana na ndugu wa kiume na wa kike wa familia mwenyeji juu ya ukweli kuhusu sala. Mara walipoelewa maana na umuhimu wa sala, walikuwa tayari kufanya sala wakati wa ushirika na, kwa hilo, hali zao zikabadilika.
Kama nimekabiliwa na uhalisi wa hali hiyo, nilijifunza kwamba kuishi kwa filosofia ya kishetani ni hatari kwa kila njia. Kuanzia sasa kwendelea, naapa kufuatilia ukweli kikamilifu, kubaini moja kwa moja njia zote za falsafa za shetani ambazo nimezikubali, na kuacha kuishi kulingana na falsafa hizo. Ninataka kumruhusu Mungu, na neno la Mungu litawale moyoni mwangu na kuchukua mamlaka. Acha ukweli uwe bwana wa moyo wangu ili nipate kuishi kwa neno la Mungu katika kila kitu.
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo Juzuu ya 1

Jifunze zaidi: Neno la Mwenyezi Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni