4/08/2019

Matamshi ya Mungu | Sura ya 36

Mwenyezi Mungu wa kweli, Mfalme katika kiti cha enzi, hutawala ulimwengu mzima, Anakabiliana na mataifa yote na watu wote, kila kitu chini ya mbingu hung’aa kwa utukufu wa Mungu. Viumbe vyote hai katika miisho ya ulimwengu vitaona. Milima, mito, maziwa, ardhi, bahari na viumbe vyote viishivyo, katika nuru ya uso wa Mungu wa kweli wamefungua mapazia yao, kuhuishwa, kama kuamka kutoka kwa ndoto, kuchipuka kwa kuvunja uchafu!  Ah! Mungu mmoja wa kweli, Huonekana mbele ya dunia. Je, nani anathubutu kumpokea kwa upinzani? Kila mmoja hutetemeka kwa hofu. Hakuna ambao hawajaridhishwa kabisa, mara kwa mara kuomba msamaha, wote kwa magoti yao mbele Yake, vinywa vyote vikimuabudu! Mabara na bahari, milima, mito, vitu vyote kumsifu bila kikomo! Vuguvugu la upepo mwanana wa masika huja na masika kuleta mvua mzuri wa masika. Mikondo ya mito, kama watu, huchanganya huzuni na furaha, kumwaga machozi ya kuwiwa na kujilaumu. Mito, maziwa, chafuko na mawimbi, yote yanaimba, yakihimidi jina takatifu la Mungu Wa kweli! Sifa hizi zinavuma kwa wazi sana! Mambo yote ya zamani ambayo kwa wakati mmoja yalikuwa yamepotoshwa na Shetani, kila mmoja atafanyia upya, atabadilika, na kuingia katika hali mpya kabisa …
Hili ni tarumbeta takatifu linasikika! Sikiliza. Sauti hiyo, tamu sana, ni kiti cha enzi kinatoa mlio, kutangaza kwa mataifa yote na watu, wakati umefika, hatima ya mwisho imefika. Mpango Wangu wa usimamizi umemalizika. Ufalme Wangu huonekana hadharani duniani. Falme za duniani zimekuwa ufalme wa Mungu Wangu. Matarumbeta Yangu saba yanasikika kutoka kwenye kiti cha enzi, na ni maajabu gani yatatokea! Watu katika miisho ya dunia watakurupuka pamoja kutoka kila upande kwa nguvu ya lundo na uwezo wa radi, baadhi yao baharini, baadhi yao wakiendesha ndege, baadhi yao watakuja kwa magari ya kila muundo na ukubwa, baadhi yao watakuja mgogoni mwa farasi. Angalia kwa karibu. Sikiliza kwa makini. Hawa wapandao farasi wa kila rangi, pepo kuchochewa, wenye majivuno na waadhimu, kama kuchukua uwanja wa vita, wao hawajali kifo. Ni wanaume, wanawake, watoto wangapi miongoni mwa milio ya farasi na kelele za watu kwa Mungu wa kweli watakanyagwa na kwato mara moja, baadhi yao wafu, baadhi yao wakivuta pumzi yao ya mwisho, baadhi yao wakiwa wamevunjika, pasipo na mtu wa kuwatunza, kupiga kelele kwa kupagawa, kulilia anga. Wana waasi! Jinsi gani hii isiwe miisho yenu ya mwisho?
Hufurahia kuona watu Wangu, ambao husikia sauti Yangu, na kukusanyika kutoka kila taifa na nchi. Watu wote, uhifadhi Mungu wa kweli daima katika midomo yao, kusifu na kuruka juu na chini bila kukoma! Wao hushuhudia kwa ulimwengu, kushuhudia Mungu wa kweli kwa sauti kama sauti ya ngurumo la maji mengi. Watu wote watasongamana katika ufalme Wangu.
Matarumbeta Yangu saba yatapaza sauti, kuamsha walio lala! Shughulika kwa haraka, muda hujakwisha. Angalia maisha yako! Fungua macho yako na uone ni wakati upi sasa. Ni nini unatafuta? Kuna nini ya kufikiri? Na ni nini kilicho cha kushikilia? Je, inawezekana kuwa bado hujafikiria tofauti katika thamani kati ya kupata maisha Yangu na mambo yote unayopenda na kushikilia? Acha kuwa makaidi na kucheza kila mahali. Usikose nafasi hii. Wakati huu hautakuja tena! Simama mara moja, tenda kufanyisha roho yako mazoezi, kutumia zana mbalimbali kukuwezesha na kuzuia kila njama na hila za Shetani, na umshinde Shetani, ili kufanya uzoefu wa maisha yako kuwa na kina, kuishi kwa kudhihirisha tabia Yangu, kufanya maisha yako ikomae, yenye majira ya kitaalamu, na daima kufuata nyayo Zangu. Sio kwa kukata tamaa, sio kwa udhaifu, daima kusonga mbele, hatua kwa hatua, moja kwa moja hadi mwisho wa barabara!
Wakati matarumbeta saba zitatoa sauti tena, itakuwa mwito wa hukumu, hukumu ya wana waasi, hukumu ya mataifa yote na watu wote, na kila taifa litajisalimisha mbele ya Mungu. Uso wa utukufu wa Mungu hakika utaonyeshwa mbele ya mataifa yote na watu wote. Kila mtu atakuwa ameridhishwa kabisa, kupiga kelele kwa Mungu wa kweli bila kikomo. Mwenyezi Mungu Atakuwa Mtukufu zaidi, na wanangu watashiriki katika utukufu, kushiriki ufalme nami, kuhukumu mataifa yote na watu wote, kuadhibu maovu, kuokoa na kuwa na huruma juu ya watu ambao ni Wangu, kuleta uthabiti na utulivu kwa ufalme. Kupitia sauti ya matarumbeta saba, kundi kubwa la watu litaokolewa, kurudi mbele Yangu kupiga magoti na kuabudu, kwa sifa daima!
Wakati matarumbeta saba zitatoa sauti mara nyingine tena, utakuwa mwisho wa enzi, mlipuko wa sauti wa tarumbeta ya ushindi dhidi ya ibilisi Shetani, saluti katika mwanzo wa maisha ya wazi wa ufalme duniani! Sauti hii ya kifahari sana, sauti hii inayoguruma pande zote za kiti cha enzi, mlipuko wa sauti ya tarumbeta inayotikisa mbingu na dunia, ni ishara ya mpango Wangu wa usimamizi, na hukumu ya Shetani, kuadhibu duniani hii ya zamani kwa kifo kabisa, jahanamu! Huu mlipuko wa sauti ya tarumbeta unaashiria kwamba lango la neema ni linafungika, kwamba uhai wa ufalme utaanza duniani, ambayo ni kamilifu kabisa. Mungu Huokoa wale wanaompenda. Mara tu watakaporudi kwa ufalme Wake, watu duniani watakabili njaa, ndwele ya kufisha, na mabakuli saba ya Mungu, tauni saba zitaanza kutumika kwa mfululizo. Mbingu na dunia zitapita, lakini neno Langu halitapita! 
Chanzo: Sura ya 36
  Jifunze zaidi: Chanzo cha Mafanikio ya Umeme wa Mashariki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni