6/11/2019

Wimbo wa Dini | Wimbo wa Onyo Jema

Wimbo wa Dini | Wimbo wa Onyo Jema


Kristo ni mshindi. Kristo ni mshindi.
I
Kwa kumfuata Mungu na kupata ukweli, unaitembea njia ya uzima.
Kwa kutafuta teolojia na kujadili nadharia, unawadhuru wengine na wewe mwenyewe.
Kuhubiri mafundisho na kushikilia sheria kunaonyesha kwamba huna uhalisi.
Kwa kutoa wito kwa sauti na kutotenda, unamdanganya Mungu waziwazi.
Kushindania hadhi na kutafuta umaarufu ni ufidhuli na kujidai.
Kwa kufuata tamaa zako mwenyewe na kukiuka ukweli, unamwasi Mungu.
Kwa kuhodhi mawazo na kumpinga Mungu moyoni mwako, unajiweka dhidi Yake.
Kutokuwa na utambuzi na kumsikiliza kila mtu kunakufanya mpumbavu sana.
Kumwabudu mwanadamu na kufuata mwanadamu kunakufanya mtu asiyeamini.
Huwezi kufikia chochote kwa kutumainia vipaji vyako na kujitegemea.
Kumcha Mungu na kuepuka maovu tu ndiko kunakufanya uwe na hekima.
Kwa kutekeleza wajibu wako kwa kanuni, unapata sifa ya Mungu.
Ee, Kristo ndiye ukweli milele.
Ee, Kristo ndiye ukweli milele.
II
Watu waaminifu si wazembe katika wajibu wao.
Watu wadanganyifu wanaweza kufanya juhudi kiasi, lakini hawana uaminifu.
Ukiwa na moyo mzuri na kutenda matendo mema, Mungu hakika atakuokoa.
Ukiwa na moyo mwovu na ubinadamu mbaya, hakika Mungu atakufunua.
Kwa kutafuta neema na kukataa kuhukumiwa, kweli unamsaliti Mungu.
Kwa kutenda maneno ya Mungu na kuwa na uhalisi, hakika Mungu atakubariki.
Kusababisha mgawanyiko na kuwadanganya watu ni matendo ya Shetani.
Kujiimarisha na kuwafanya wengine wakutii ni ufidhuli wa ajabu sana.
Kuwatega wengine kwa hila na kuanzisha ufalme wako kunakufanya uwe pepo mbaya na mpinga Kristo.
Kumfuata Mungu na kuishi kwa maneno Yake kunakufanya uwe mwenye busara kweli.
Kushuhudia kwa Mungu na kumtukuza Mungu ni huduma ya kweli.
Kumpenda Mungu na kutenda ukweli ni njia ya Petro ya mafanikio.
Ee, Kristo ndiye ukweli milele.
Ee, Kristo ndiye ukweli milele.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni