4/05/2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 35

Ngurumo saba zinatoka kwenye kiti cha enzi, zinautikisa ulimwengu, zinageuza mbingu na ardhi, na zinavuma angani! Sauti hiyo inapenya sana kiasi kwamba watu hawawezi kuepuka wala kujificha. Nuru ya ghafla ya umeme na sauti ya radi zinatumwa mbele, zikiiangusha chini mbingu na ardhi papo hapo, na watu wamekaribia kufa. Kisha, dhoruba ya mvua kali inafagia ulimwengu wote kwa kasi ya umeme, ikianguka kutoka angani! Katika pembe za mbali za dunia, kama mvua inayonyesha ndani ya kila pembe na kila mwanya, hakuna doa hata moja linalobaki, na inavyoosha wote kutoka kichwa hadi kidole, hakuna kinachojificha kutoka kwake wala hakuna mtu yeyote awezeya kujikinga kutoka kwake. Sauti za ngurumo, kama mng’ao wa mzizimo wa miali ya umeme, zinawafanya watu kutetemeka kwa hofu! Mapanga ya makali-kuwili yanawaangusha wana wa uasi, na adui anakabiliwa na janga bila maficho kabisa ya kukimbilia, vichwa vyao vikizunguka katika vurugu ya dhoruba, na, kupigwa hadi wazirai, wanaanguka wakiwa wafu mara moja kwenye maji yanayopita na kusombwa. Wanakufa kwa urahisi bila njia yoyote ya kuokoa maisha yao. Ngurumo hizo saba zinatoka Kwangu na zinafikisha nia Yangu, ambayo ni kupiga na kuwaangusha wana wa kwanza wa Misri, kuadhibu waovu na kutakasa makanisha Yangu, ili yote yawe na uhusiano wa karibu sana, yafikirie na kutenda kwa njia moja, na ni ya moyo mmoja na Mimi, na ili makanisa yote ulimwenguni yaweze kujengwa kuwa kitu kimoja. Hili ndilo kusudi Langu.
Wakati ngurumo inatoa sauti, mawimbi ya kelele yanazuka. Baadhi wanaamshwa kutoka usingizini mwao, na, kutiwa wasiwasi sana, wanatafuta ndani ya nafsi zao na kukimbia kurudi mbele ya kiti cha enzi. Wanasitisha kufanya hila na kudanganya na kutenda uhalifu, na watu kama hawa hawajachelewa sana kuamshwa. Natazama kutoka kwenye kiti cha enzi. Naangalia kwa kina ndani ya mioyo ya watu. Naokoa wale ambao wana hamu na Mimi kwa bidii, na Ninawaonea huruma. Nitawaokoa katika umilele wanaonipenda mioyoni mwao zaidi ya mengine yote, wale ambao wanaelewa mapenzi Yangu, na wanaonifuata hadi mwisho wa njia! Mkono Wangu utawashikilia kwa usalama ili wasikabiliwe na tukio hili na wasikutane na madhara. Baadhi, wanapoona tukio hili la mwanga wa umeme ukimulika kwa ghafla, wanakuwa na maumivu katika mioyo yao kiasi kwamba watapata ugumu wa kutoa sauti, na majuto yao yamekuja kwa kuchelewa mno. Wakiendelea katika kutenda kwa njia hii, watakuwa wamechelewa mno. Ah, kila kitu, kila kitu! Yote yatakuwa yametendeka. Hii ni mojawapo ya njia Zangu za wokovu. Nawaokoa wale wanaonipenda na kuwaangusha waovu. Nafanya ufalme Wangu kuwa thabiti na imara duniani na Mimi nawafanya watu wote wa kila taifa katika ulimwengu mzima kujua ya kwamba Mimi ndiye muadhama, Mimi ni moto mkali, Mimi ni Mungu anayetafuta ndani kabisa ya moyo wa kila mtu. Tangu sasa kwenda mbele, hukumu ya kiti cheupe cha enzi inafunuliwa hadharani kwa wengi na inatangazwa kwa watu wote ya kwamba hukumu imeanza! Ni bila shaka ya kwamba wote ambao hawazungumzi yaliyomo katika mioyo yao, wale ambao wanahisi daghadagha na wanadhubutu kutotilia maanani, wale ambao hupoteza muda, wanaoelewa matakwa Yangu lakini hawana nia ya kuyaweka katika vitendo, lazima wahukumiwe. Lazima mchunguze kwa makini nia na maazimio yenu nyinyi wenyewe, na mchukue nafasi zenu zilizo sahihi, wekeni katika vitendo kikamilifu yale Ninayoyasema, wekeni umuhimu kwenye uzoefu wa maisha yenu, wala msitende kwa shauku kwa nje, lakini fanyeni maisha yenu yakue, komavu, imara na yenye uzoefu, na pale tu ndio mtaupendeza moyo Wangu.
Wanyime watumishi wa Shetani na roho waovu wanaovuruga na kuharibu yale Mimi najenga fursa zozote kutumia vitu kwa maslahi yao. Lazima wawekewe mipaka na kuzuiwa kwa ukali na wanaweza tu kutendewa hivyo kwa kutumia mapanga yenye makali. Wabaya zaidi lazima wang’olewe mara moja ili wasiweze kusababisha tishio katika siku zijazo. Na kanisa litakuwa limekamilika, hakutakuwa na ulemavu wowote, na litakuwa na afya, lililojawa na uhai na nguvu. Kufuatia umeme wa kumulika kwa ghafla, mngurumo wa radi unatoa sauti. Lazima msipuuze, na ni lazima msikate tama lakini fanyeni yote mnayoweza kufikia nafasi hii, na hakika mtaweza kuona kile ambacho mikono Yangu hutenda, kile Ninachopata, kile Ninachotupa, kile Nakamilisha, kile Nang’oa, kile Naangusha. Haya yote yatafunuliwa mbele ya macho yenu ili muone wazi uweza Wangu.
Kutoka katika kiti cha enzi mpaka mwisho wa ulimwengu mzima, ngurumo saba zinatoa mwangwi. Kundi kubwa la watu wataokolewa na kujiwasilisha mbele ya kiti Changu cha enzi. Kufuatia nuru hii ya uhai, watu wanatafuta mbinu za kuishi na hawawezi kujisaidia ila kuja Kwangu, kupiga magoti katika ibada, vinywa vyao vinaita jina la mwenyezi Mungu wa kweli, na wanatoa sauti ya kusihi kwao. Lakini kwa wale ambao wananipinga, watu wanaofanya mioyo yao kuwa migumu, mngurumo unasikika katika masikio yao na bila shaka ni lazima waangamie. Haya kwa urahisi ni matokeo ya mwisho kwa ajili yao. Wanangu wapendwa ambao ni washindi watakaa Sayuni na watu wote wataona watakachopata, na utukufu mkubwa utaonekana mbele yenu. Hii kweli ni hasa baraka kuu ambayo utamu wake ni vigumu kuweka katika maneno.
Wakati sauti ya ngurumo saba inatokea, kuna wokovu wa wale wanaonipenda, wanaonitamani kwa mioyo ya ukweli. Wale ambao ni Wangu na Niliowaamulia kabla na kuwateua wote wana uwezo wa kurudi kwa jina Langu. Wanaweza kusikia sauti Yangu, ambayo ni mwito wa Mungu. Hebu wale walio katika mwisho wa dunia waone ya kwamba Mimi ni mwenye haki, Mimi ni mwaminifu, Mimi ni upendo, Mimi ni huruma, Mimi ni muadhama, Mimi ni moto mkali, na hatimaye Mimi ni hukumu bila huruma.
Hebu wote walio duniani waone ya kwamba Mimi ndiye Mungu halisi Mwenyewe na Aliye mkamilifu kabisa. Watu wote wameshawishika kwa dhati na hakuna anayethubutu kunipinga tena, kunihukumu au kunisingizia tena. Vinginevyo, watakutana mara moja na laana na maafa yatawapata. Wao watalia na kusaga meno tu na wataleta uharibifu wao wenyewe.
Hebu watu wote wajue, na ijulikane hadi mwisho wa ulimwengu, ili kila mmoja na kila mtu ajue. Mwenyezi Mungu ndiye Mungu mmoja na wa kweli, wote tena na tena watapiga magoti chini kumuabudu na hata watoto ambao wamejifunza tu kuzungumza wataita “Mwenyezi Mungu”! Wale maafisa wanaoshikilia madaraka wataona kwa macho yao wenyewe Mungu wa kweli akionekana mbele yao na wao pia watasujudu wenyewe katika ibada, wakiomba rehema na msamaha, lakini watakuwa wamechelewa mno kwa maana wakati wa mauti yao umefika; lazima litendeke kwao: kuwahukumu kwa shimo lisilopimika. Nitaileta enzi nzima kufika tamati, na kuimarisha ufalme Wangu hata zaidi. Mataifa yote na watu watajiwasilisha mbele Yangu milele! 
Chanzo: Sura ya 35
Sikiliza zaidi: Neno la Mwenyezi Mungu—Sura ya 36

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni