Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mitume. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mitume. Onyesha machapisho yote

3/26/2018

Sura ya 38. Yeye Ambaye Hukosa Ukweli Hawezi Kuwaongoza WengineπŸ“–πŸ€²

πŸ“–πŸ“–πŸ“–***********πŸ‘πŸ‘πŸ‘***********πŸ“šπŸ“šπŸ“š*********πŸ™‚πŸ™‚πŸ™‚πŸ™‚
    Mwenyezi Mungu alisema, Je, kweli mnaelewa kuhusu mabadiliko katika tabia ya mtu? Mabadiliko katika tabia yanamaanisha nini? Je, mnaweza kutambua mabadiliko katika tabia? Ni hali zipi zinaweza kufikiriwa kuwa mabadiliko katika tabia ya maisha ya mtu, na ni hali zipi ambazo ni mabadiliko tu katika tabia ya nje? Tofauti ni ipi kati ya mabadiliko katika tabia ya mtu ya nje na mabadiliko katika maisha ya mtu ya ndani? Je, mnaweza kueleza tofauti? Mnamwona mtu mwenye hamu ya kukimbia pote kwa ajili ya kanisa, na mnasema: "Yeye amebadilika!" Mnamwona mtu akiitelekeza familia yake au kazi, na mnasema: "Yeye amebadilika!" Ikiwa amejitoa mhanga kwa namna hiyo, mnafikiri kwa hakika lazima amebadilika.