3/07/2018

๐Ÿ“–๐Ÿ˜‡Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tamko la Saba๐Ÿคฒ๐Ÿ˜Š

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu,

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tamko la Saba

Matawi yote ya magharibi yanapaswa kuisikiliza sauti Yangu:
Je, mmekuwa waaminifu Kwangu hapo awali? Je, mmekuwa mkiyasikia maneno Yangu mazuri ya ushauri? Je, mnayo matumaini ambayo ni halisi na yasiyo na mashaka? Utiifu wa mwanadamu, mapenzi yake, imani yake—hamna kipatikanacho ila kutoka Kwangu, hamna hata kimoja ila kilichotawazawa na Mimi. Nyie watu Wangu, myasikiapo maneno Yangu, je mnaielewa nia Yangu? Mnaiona roho Yangu? Mlipoipitia njia ya huduma hapo awali mlikumbana na panda-shuka, maendeleo mazuri na vikwazo, na zilikuwepo nyakati mlipokuwa katika hatari ya kuanguka na hata kunisaliti Mimi;

3/06/2018

๐ŸŽต๐ŸŽผUmeme wa Mashariki | Maonyesho Kamili ya Mamlaka ya Muumba๐ŸŽง๐Ÿ˜„

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki ,Nyimbo

Umeme wa Mashariki | Maonyesho Kamili ya Mamlaka ya Muumba

Kwa mamlaka ya Muumba, miujiza yaonekana,
ikiwa na mvuto kwa mwanadamu,
Mwanadamu hutazama kwa butwaa.
Nguvu Zake huleta furaha;
mwanadamu hustabishwa, kwa furaha tele.
Kwa kupendezwa na kushangaa, Yeye hushangilia.
Mwanadamu huguswa waziwazi;

✍️๐ŸŒน๐Ÿ’–10. Upendo wa Mungu ni wa Kweli Kabisa๐Ÿ™‚

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Kanisa
Wenzhong , Beijing
Agosti 11, mwaka wa 2012
Usiku wa Julai 21, mwaka wa 2012, tulikuwa na mafuriko makubwa hapa, ambayo hutokea kwa nadra. Ningependa kumwambia kila mtu aliye na kiu ya Mungu kile nilichokipitia kwa kweli na kukiona wakati huo.
Siku hiyo mume wangu nami tuliutunza uga wa chakula kikavu cha mifugo wa dada yangu. Wakati wa usiku mvua nzito iliendelea kunyesha, na tulienda kulala mapema sana. Saa nne kasorobo usiku ndugu mkwe wangu wa kiume aliita akisema: “Wanaelekea kufungua hodhi! Kila kitu kitafurikiwa!

3/05/2018

๐Ÿ“–๐Ÿ“–Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III๐Ÿ‘๐Ÿ˜‡

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,Injili
9. Yesu Atenda Miujiza.
1) Yesu Awalisha Watu Elfu Tano.
(Yohana 6:8-13) Mmoja wa wanafunzi wake, Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia, Yupo mvulana hapa, aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili: lakini hivi ni nini kwa watu wengi kama hawa? Naye Yesu akasema, Wafanye watu hawa waketi chini. Na mahali pale palikuwa na majani mengi. Basi wale wanaume wakaketi, wapatao elfu tano kwa jumla. Kisha Yesu akaichukua ile mikate; na baada ya kutoa shukrani, akawagawia wafuasi wake, nao wafuasi wake wakawagawia walioketi; na vile vile wale samaki kwa kiasi walichoweza. Waliposhiba, aliwaambia wanafunzi wake, Kusanyeni vipande vilivyobaki, ili chochote kisipotee. Basi wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya mikate mitano ya shayiri vilivyobaki baada ya wale watu kula.

๐Ÿ˜‡๐Ÿ˜‡Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tamko La Ishirini Na Saba๐Ÿ“–๐ŸŒน

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tamko La Ishirini Na Saba

Mienendo ya binadamu haijawahi kuugusa moyo Wangu kamwe, wala kuonekana Kwangu kama kitu cha thamani. Machoni mwa mwanadamu, Mimi humweka katika sheria kali kila wakati, na kila mara Nimemweka chini ya mamlaka kali. Ndani ya matendo yote ya mwanadamu, ni mambo machache sana anayonifanyia Mimi, na mara nyingi hapana kitendo chake kisimamacho imara machoni Pangu. Hatimaye, kila kitu kinachomhusu mwanadamu kimeporomoka polepole mbele Yangu, na ni katika nyakati kama hizi ndipo matendo Yangu hudhihirika, na kumfanya kila mmoja, katika upotovu wake, kunitambua Mimi.

3/04/2018

Umeme wa Mashariki | 62. Sababu ya Kweli ya Kazi Isiyofaa

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Kanisa

Umeme wa Mashariki | 62. Sababu ya Kweli ya Kazi Isiyofaa
Xinyi Mji wa Xi’an, Mkoa wa Shaanxi
Katika ziara zangu za karibuni kwa makanisa, mara nyingi niliwasikia viongozi na wafanyakazi wakisema kwamba watu wengine, baada ya kuhudhuria ushirika na mimi, waligeuka hasi, wanyonge na walikosa motisha ya kuendelea kutafuta. Wengine walisema ilikuwa vigumu sana kumwamini Mungu na walimwelewa Mungu visivyo. Wengine walisema kwamba hali zao zilikuwa nzuri kabla ya wao kukutana na mimi, lakini punde tu waliponiona, walihisi shinikizo kubwa mno na wasio na raha.

52 Dalili za Udanganyifu Ndani ya Mwanadamu na Asili ya Mwanadamu Ambazo Humsaliti Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Ugumu ambao watu wanaweza kuukabili kwa urahisi katika uzoefu wao, vitu ambavyo vinawasababisha watu kuanguka kwa urahisi, na pahali ambapo udhaifu wa jaala wa kila mtu upo yote ni masuala ambayo lazima mtu awe na ujuzi nayo. Kwa nini unaanguka, unamwacha Mungu na kupoteza imani ya kuendelea na ukimbiziaji wako wa ukweli unapokabiliana na mambo fulani? Kwa sasa, kila mtu yumo hatarini mwa mambo haya. Bila kujali kiwango cha imani uliyo nayo kwa kawaida, shauku yako ni kubwa kiasi gani, wewe ni shupavu na asiyekubali kushindwa jinsi gani, ni kitu cha aina moja pekee kinaweza kufanyika ambacho kinaweza kufanya kila mmoja kushtuka na kuanguka kwa urahisi.

3/03/2018

7. Katikati ya Maafa Niliiona Tabia ya Haki ya Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Kanisa
Li Jing, Beijing
7 Agosti, mwaka wa 2012
Siku hiyo, ilianza kunyesha asubuhi. Nilikwenda kwa mkutano nyumbani mwa ndugu mmoja, wakati mvua ilipoendelea kuongezeka zaidi na zaidi kwa uzito. Kufikia alasiri ilikuwa ikinyesha kana kwamba ilitoka mbinguni moja kwa moja. Wakati tulipomaliza mkutano wetu, mvua ilikuwa imeingia katika ua wa ndugu yangu, lakini kwa sababu nilikuwa na wasiwasi juu ya familia yangu, nilijitahidi kwenda nyumbani. Nusu ya barabara huko, baadhi ya watu waliokimbia hatari waliniambia, "Je, si wewe unatoroka, bado unakwenda nyumbani?" Nilipofika nyumbani, mtoto wangu aliniuliza, "Je, mafuriko hayakukuzoa?" Ni hapo tu nilipojua kwamba sikuwa na Mungu moyoni mwangu.

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (2)

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (2)

Kazi na kuingia kwenu ni duni kabisa; mwanadamu hafikirii kwamba kazi ni muhimu na hata yeye ni mzembe zaidi na kuingia. Mwanadamu haoni haya kuwa mafunzo mazuri anayopaswa kuingia ndani; kwa hivyo, katika uzoefu wake wa kiroho, kwa kweli yote ambayo mwanadamu huona ni njozi za kiajabu. Si mengi yanatakiwa kutoka kwenu kuhusu uzoefu wenu katika kazi, lakini, kama yule anayetakiwa kukamilishwa na Mungu, mnapaswa kujifunza kumfanyia Mungu kazi ili hivi punde muweze kuupendeza moyo wa Mungu.

3/02/2018

Umeme wa Mashariki | Sura ya 5

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Umeme wa Mashariki | Sura ya 5

Mwenyezi Mungu alisema, Wakati Roho Wangu anatoa sauti, Anaonyesha hali nzima ya tabia Yangu. Je, wewe unalifahamu hili? Kutolifahamu hili katika hatua hii itakuwa sawa na kunipinga moja kwa moja. Je umeona umuhimu ulioko humu? Je, unajua juhudi kiasi gani, kiasi gani cha nguvu, Ninatumia juu yako? Je, unaweza thubutu kuweka wazi kila ulichofanya mbele Yangu? Na mna ujasiri wa kujiita watu Wangu usoni Mwangu—hamna hisia za aibu, pia, bila mantiki yoyote! Wakati mmoja au mwingine, watu kama hawa watafukuzwa kutoka katika nyumba Yangu. Usithubutu kunidanganya, ukifikiri kwamba umesimama kwa ajili ya ushuhuda Wangu!

Yote kuhusu Mjadala wa "Iwapo Biblia Inatiwa Msukumo na Mungu"



Utambulisho
Kwa miaka elfu mbili, dunia ya kidini imetegemea kile alichosema Paulo kuhusu Biblia kutiwa msukumo na Mungu na daima iliamini kwamba “Biblia ni maneno ya Mungu,” na “Biblia inamwakilisha Bwana.” Je, mawazo haya ni sahihi? Video hii itafichua majibu kwako!

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho.

3/01/2018

Umeme wa Mashariki | Ufalme wa Milenia Umewasili

Umeme wa Mashariki | Ufalme wa Milenia Umewasili

    Je, mmeona kazi ambayo Mungu ataikamilisha katika kundi hili la watu? Mungu alisema, hata katika Ufalme wa Milenia watu ni lazima waendelee kufuata matamshi Yake, na katika maisha ya baadaye, matamshi ya Mungu bado yatakuwa yanaongoza maisha ya mwanadamu moja kwa moja kwenda katika nchi ya Kanaani. Musa alipokuwa jangwani, Mungu alimwelekeza na kuzungumza naye moja kwa moja. Kutoka mbinguni Mungu alituma chakula, maji, na mana ili watu waweze kuvifurahia, na leo bado ni hivyo: Mungu mwenyewe ametuma vitu chini kwa ajili ya kula na kunywa ili watu wafurahi, na yeye mwenyewe ametuma laana ili kuwaadibu watu.

Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

(I) Mhutasari juu ya Mamlaka ya Mungu, Tabia ya Haki ya Mungu, na Utakatifu wa Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Mnapomaliza maombi yenu, je, mioyo yenu inahisi utulivu katika uwepo wa Mungu? (Ndiyo.) Ikiwa moyo wa mtu unaweza kutulizwa, ataweza kusikia na kuelewa neno la Mungu na ataweza kusikia na kuuelewa ukweli. Ikiwa moyo wako hauwezi kutulizwa, ikiwa moyo wako siku zote unayoyoma, au siku zote unafikiria juu ya mambo mengine, utaathiri kuja kwako pamoja kusikia neno la Mungu. Sasa, ni kitu gani cha msingi tunachokijadili wakati huu? Hebu sote turudi nyuma kidogo katika hoja kuu. Kuhusiana na kumjua Mungu Mwenyewe, yule wa kipekee, sehemu ya kwanza tuliyoijadili ni ipi? (Mamlaka ya Mungu.) Ya pili ilikuwa ni ipi? (Tabia ya haki ya Mungu.) Na ya tatu? (Utakatifu wa Mungu.)