5/31/2019

Wimbo wa Maneno ya Mungu | "Kusudi la Kazi ya Mungu la Usimamizi" | The True Love of God for Man

Wimbo wa Kuabudu | "Kusudi la Kazi ya Mungu la Usimamizi" | The True Love of God for Man

I
Mungu ana mpango wa usimamizi wa miaka 6,000, uliyogawanywa katika hatua tatu, kila moja inaitwa enzi. Kwanza ni Enzi ya Sheria, kisha Enzi ya Neema, na Enzi ya Ufalme ni awamu ya mwisho. Ingawa kazi ya Mungu ni tofauti katika kila moja, yote inalingana na kile ambacho binadamu wanahitaji, ama hasa inalingana na ujanja ambao Shetani anatumia, anapopigana na Yeye. Kusudi la Kazi ya Mungu ni kumshinda Shetani, kufunua hekima ya Mungu na ukuu, na kufichua ujanja wote wa Shetani, hivyo kumwokoa mwanadamu kutoka kwa utawala wake, hivyo kumwokoa mwanadamu kutoka kwa utawala wake.

5/30/2019

Wimbo wa Injili "Kiini cha Kristo Ni Mungu" | Differences Between the True Christ and False Christs



Wimbo wa Injili "Kiini cha Kristo Ni Mungu" | Differences Between the True Christ and False Christs


Mungu anayekuwa mwili anaitwa Kristo,
na hivyo Kristo anayeweza kuwapa watu ukweli anaitwa Mungu.
Si kupita kiasi kusema hivyo,
kwani Ana kiini cha Mungu, Ana tabia ya Mungu na hekima katika kazi Yake,
ambayo haifikiwi na mwanadamu.
Wale wanaojiita Kristo wenyewe ilhali hawawezi kufanya kazi ya Mungu ni wadanganyifu.
Wanaojifanya kuwa Kristo hatimaye wataanguka,
ingawaje wanadai kuwa Kristo,
hawana kiini chochote cha Kristo.

5/29/2019

“Wakati Wa Mabadiliko” – Njia ya Pekee ya Kuinuliwa Kwenda Katika Ufalme wa Mbinguni | Clip 2/2


“Wakati Wa Mabadiliko” – Njia ya Pekee ya Kuinuliwa Kwenda Katika Ufalme wa Mbinguni | Swahili Gospel Movie Clip 2/2


Watu wengine huamini, kwa kuwa Mungu aliweza kuumba mbingu na dunia na vitu vyote kwa neno moja, kuweza kuwafufua wafu kwa neno moja, Mungu pia Ataweza kubadili taswira zetu mara moja, kutufanya watakatifu, kutuinua hewani kukutana na Bwana wakati Atakaporudi katika siku za mwisho. Je, kweli ni ili kuinuliwa kwenda katika ufalme wa mbinguni? Je, kazi ya kurudi kwa Mungu katika siku za mwisho rahisi hivyo jinsi tunavyofikiri? Mungu husema, "Lazima ufahamu wala usirahisishe mambo zaidi. Kazi ya Mungu ni tofauti na kazi nyingine ya kawaida. Uzuri wake hauwezi kutambuliwa na akili za mwanadamu wala hekima yake kupatikana vile.

5/28/2019

“Ndoto Yangu ya Ufalme wa Kibinguni” | Swahili Gospel Movie Clip 5/5


“Ndoto Yangu ya Ufalme wa Kibinguni” – Ushuhuda wa Kupitia Hukumu Mbele ya Kiti cha Kristo na Kupokea Uzima | Swahili Gospel Movie Clip 5/5


Mwenyezi Mungu ameanzisha kazi ya hukumu akianza na nyumba ya Mungu kwa kuonyesha ukweli. Utangulizi wa hukumu kabla ya ufalme mkuu mweupe kuanza. Tunapitia hukumu ya Mungu na kuadibiwa na Mungu vipi? Je, ni aina gani ya utakaso na mabadiliko yanaweza kupatikana baada ya kupitia hukumu na adabu ya Mungu? Ni maarifa gani ya kweli ya Mungu yanaweza kuarifiwa?

Mwenyezi Mungu anasema, “Leo, mazungumzo juu ya kufanywa mkamilifu ni hali moja tu. Haijalishi kinachofanyika, lazima muwe na hatua hii ya ushuhuda kwa kufaa.

5/27/2019

“Ndoto Yangu ya Ufalme wa Kibinguni” | Swahili Gospel Movie Clip 4/5


“Ndoto Yangu ya Ufalme wa Kibinguni” – Ni nini Tofauti Kati ya Kazi ya Mungu ya Hukumu katika Siku za Mwisho na Kazi ya Bwana Yesu? | Swahili Gospel Movie Clip 4/5


Baadhi ya watu huamini kwamba baada ya Bwana Yesu kufufuka na kupaa mbinguni, Roho Mtakatifu alishuka kufanya kazi kwa mtu katika siku ya Pentekoste. Yeye aliishutumu dunia ya dhambi, na ya haki, na ya hukumu. Tunapopokea kazi ya Roho Mtakatifu na kutubu kwa Bwana kwa ajili ya dhambi zetu, tunapitia hukumu ya Bwana. Kazi inayofanywa na Roho Mtakatifu katika siku ya Pentekoste inapaswa kuwa kazi ya hukumu ya Mungu katika siku za mwisho. Je, tu sahihi katika njia tunayoipokea? Je, kuna tofauti gani kati ya kazi ya Bwana Yesu na kazi ya hukumu ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho?

5/26/2019

“Ndoto Yangu ya Ufalme wa Kibinguni” | Swahili Gospel Movie Clip 3/5


“Ndoto Yangu ya Ufalme wa Kibinguni” – Ufalme wa Mbinguni u Wapi Hasa? | Swahili Gospel Movie Clip 3/5


Matamanio yetu makuu sisi tunaoamini katika Bwana ni kukaribisha kurudi kwa Bwana, kuletwa katika ufalme wa mbinguni, na kupokea ahadi na baraka za Mungu. Watu wengi wanaamini kwamba Bwana atakaporudi, tutainuliwa hewani kukutana na Bwana. Lakini katika Biblia, inasemekana kwamba Yerusalemu mpya itashuka kutoka mbinguni. "maskani ya Mungu yako pamoja na wanadamu," "falme za dunia zimekuwa falme za Bwana wetu, na za Kristo wake." Je, ufalme wa mbinguni uko angani au duniani? Bwana atawapelekaje watakatifu katika ufalme wa mbinguni atakaporudi?

Sikiliza zaidi: Kurudi kwa Bwana Yesu

5/25/2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa Makanisa | Sura ya 16

Baada ya ushuhudiaji wa Mwana wa Adamu, Mwenyezi Mungu alijifichua kwetu hadharani kama Jua la haki. Haya ndiyo mabadiliko mlimani! Sasa inakuwa halisi zaidi na zaidi, na zaidi kuwa jambo la uhalisi. Tumeona utaratibu wa kazi ya Roho Mtakatifu, Mungu Mwenyewe ameibuka kutoka kwa mwili wa damu. Yeye hayuko chini ya udhibiti wa mwanadamu, wala anga, wala jiografia; Yeye huvuka mipaka ya nchi na bahari, Yeye hufika miisho halisi ya ulimwengu, na mataifa yote na watu wa jumuia zote wanasikiliza sauti Yake kwa utulivu.

5/24/2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa Makanisa | Sura ya 8

Kwa kuwa Mwenyezi Mungu—Mfalme wa ufalme—ameshuhudiwa, mawanda ya usimamizi wa Mungu yamejitokeza kabisa katika ulimwengu wote. Sio tu kwamba kuonekana kwa Mungu kumeshuhudiwa nchini China, lakini jina la Mwenyezi Mungu limeshuhudiwa katika mataifa yote na nchi zote. Wote wanaliita jina hili takatifu, wakitafuta kufanya ushirika na Mungu kwa njia yoyote iwezekanayo, wakiyafumbata mapenzi ya Mwenyezi Mungu na kuhudumu kwa uratibu katika kanisa. Roho Mtakatifu hufanya kazi kwa njia hii ya ajabu.

5/23/2019

Umeme wa Mashariki | “Ndoto Yangu ya Ufalme wa Kibinguni” | Swahili Gospel Movie Clip 2/5

“Ndoto Yangu ya Ufalme wa Kibinguni” – Jinsi ya Kufuatilia Ili Kuingia katika Ufalme wa Mbinguni (2) | Swahili Gospel Movie Clip 2/5


Waumini wengi wa Bwana wanahisi kwamba almradi tukiyafuata maneno ya Bwana, tukitenda unyenyekevu na uvumilivu, na kufuata mfano wa Paulo kwa kujitolea, kutumia rasilmali na kufanya kazi kwa ajili ya Bwana, tutayaridhisha mapenzi ya Mungu. Na tutaletwa katika ufalme wa mbinguni Bwana atakaporudi. Hata hivyo, je, tumewahi kufikiria iwapo jitihada kama hizi kweli zitastahili sifa za Bwana na ruhusa ya kuingia katika ufalme wa mbinguni? Kama sivyo, tunapaswa kufuatilia kupata sifa ya Bwana na kuletwa katika ufalme wa mbinguni vipi?

5/22/2019

“Ndoto Yangu ya Ufalme wa Kibinguni” | Swahili Gospel Movie Clip 1/5


“Ndoto Yangu ya Ufalme wa Kibinguni” – Jinsi ya Kufuatilia Ili Kuingia katika Ufalme wa Mbinguni (1) | Swahili Gospel Movie Clip 1/5


        Waumini wengi wa Bwana wanahisi kwamba almradi tukiyafuata maneno ya Bwana, tukitenda unyenyekevu na uvumilivu, na kufuata mfano wa Paulo kwa kujitolea, kutumia rasilmali na kufanya kazi kwa ajili ya Bwana, tutayaridhisha mapenzi ya Mungu. Na tutaletwa katika ufalme wa mbinguni Bwana atakaporudi. Hata hivyo, je, tumewahi kufikiria iwapo jitihada kama hizi kweli zitastahili sifa za Bwana na ruhusa ya kuingia katika ufalme wa mbinguni? Kama sivyo, tunapaswa kufuatilia kupata sifa ya Bwana na kuletwa katika ufalme wa mbinguni vipi?

Mwenyezi Mungu anasema, “  Kazi inapozungumziwa, mwanadamu anaamini kwamba kazi ni kusafiri kwenda huku na huko kwa ajili ya Mungu, akihubiri kila sehemu, na kugharimia rasilmali kwa ajili ya Mungu.

5/21/2019

2018 Gospel Music "Mungu Kuutawala Ulimwengu" (Swahili Subtitles)


2018 Gospel Music "Mungu Kuutawala Ulimwengu" (Swahili Subtitles)


Ulimwengu ni mkubwa sana na usio na kikomo, na una nyota nyingi mno zisizohesabika katika mzunguko sahihi…. Unatamani kujua aliyeziumba sayari za juu za ulimwengu, na yule ambaye huamuru tao la mtupo angani? Dondoo ya kustaajabisha ya filamu ya Kikristo ya Mungu Kuutawala Ulimwengu itakuonyesha nguvu yenye uwezo ya Muumba.

Kujua zaidi: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu.

Sikiliza zaidi: 2018 Gospel Music "Mungu Kuutawala Mwanzo na Mustakabali wa Wanadamu" (Swahili Subtitles)

5/20/2019

Swahili Christian Skit | "Polisi Waenda kwa Ziara ya Mwaka Mpya" (Kichekesho)


Zheng Xinming, mwanamume mzee wa karibu miaka sabini, ni Mkristo wa dhati. Kwa sababu ya imani yake katika Bwana, aliwekwa kizuizini na kufungwa gerezani, na kuhukumiwa miaka nane. Alipoachiliwa, bado alikuwa ameorodheshwa na Polisi wa Kikomunisti wa China kama mlengwa wa ufuatiliaji wa kuzingatiwa. Hasa, baada ya mzee huyo kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, polisi walikuja karibu kila siku kumtisha, kumuogofya na kumsumbua. Hakukuwa na njia ya Zheng Xinming kusoma neno la Mungu nyumbani kwa kawaida, na hata familia yake ilishiriki hali yake ya wasiwasi.

5/19/2019

Neno la Mungu "Jinsi ya Kuujua Uhalisi"


Mwenyezi Mungu anasema, "Mungu ni Mungu wa uhalisi: kazi Zake zote ni halisi, maneno yote Anayoyanena ni halisi, na ukweli wote Anaouonyesha ni halisi. Kila kisicho maneno Yake ni kitupu, kisichokuwepo, na kisicho timamu. Leo, Roho Mtakatifu yupo kwa ajili ya kuwaongoza watu katika maneno ya Mungu. Ikiwa watu wanatafuta kuingia katika uhalisi, basi ni lazima wauandame uhalisi, na waujue uhalisi, baadaye ni lazima wapitie uhalisi, na kuishi kwa kudhihirisha uhalisi. Kadiri watu wanavyoujua uhalisi zaidi, kadiri wanavyoweza kugundua ikiwa maneno ya wengine ni halisi;