8/13/2019

New Swahili Gospel Movie "Siri ya Utauwa" | Bwana Yesu Kristo Atarudi Vipi?



New Swahili Gospel Movie "Siri ya Utauwa" | Bwana Yesu Kristo Atarudi Vipi?


Lin Bo'en alikuwa mzee wa kanisa katika kanisa la nyumbani Uchina. Wakati wa miaka yake yote kama muumini, alihisi kwamba ameheshimiwa kuteseka kwa ajili ya Bwana, na alithamini kumfahamu na kumpata Bwana Yesu Kristo zaidi ya kitu kingine chochote duniani. Siku moja ya jaala, alienda nje kuhubiri na akasikia habari fulani za kushtua: Bwana Yesu amerudi katika mwili, na Yeye ni Kristo wa siku za mwisho—Mwenyezi Mungu! Lin Bo'en alikanganyikiwa. 

8/12/2019

“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Tunaweza Kupata Uzima kwa Kuamini Katika Biblia? | Swahili Gospel Movie Clip 6/6



“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Tunaweza Kupata Uzima kwa Kuamini Katika Biblia? | Swahili Gospel Movie Clip 6/6


Mara kwa mara wachungaji na wazee huwafundisha watu kuwa hawawezi kuitwa waumini wakiondoka kwenye Biblia, na kwamba kwa kushikilia Biblia pekee ndiyo wanaweza kupata uzima na kuingia katika ufalme wa mbinguni. Kwa hivyo, je, kweli hatuwezi kupata uzima tukiondoka kwenye Biblia? Je, ni Biblia ambayo inaweza kutupa uzima, au ni Mungu ambaye anaweza kutupa uzima? Bwana Yesu alisema, "Tafuta katika maandiko; kwa kuwa ndani yake mnadhani kuwa mna uzima wa milele: na hayo ndiyo yananishuhudia. Nanyi hamtakuja Kwangu, kwamba mpate uhai" (Yohana 5:38-40).  

8/11/2019

Matamshi ya Mungu | Sura ya 41

Kuhusu shida zinazoibuka kanisani, usiwe na mashaka mengi. Kanisa linapojengwa haiwezekani kuepuka makosa, lakini usiwe na wasiwasi unapokabiliwa na shida hizo; kuwa mtulivu na makini. Sijawaambia hivyo? Omba Kwangu mara nyingi, na Nitakuonyesha kwa wazi nia Zangu. Kanisa ni moyo Wangu na ni lengo Langu la msingi, Nawezaje kutolipenda? Usiogope, mambo kama haya yanapotendeka kanisani, yote yanaruhusiwa na Mimi. Simama na uwe sauti Yangu.

8/10/2019

Wimbo wa Maneno ya Mungu "Mamlaka na Nguvu Anayoonyesha Mungu Anapopata Mwili"



Wimbo wa Maneno ya Mungu "Mamlaka na Nguvu Anayoonyesha Mungu Anapopata Mwili"


I Mungu alikuja duniani hasa kutimiza ukweli wa "Neno kuwa mwili." (tofauti na Agano la Kale, katika siku za Musa, Mungu alizingumza moja kwa moja kutoka mbinguni). Kisha, yote yatatimizwa katika enzi ya Ufalme wa Milenia kuwa ukweli ambao watu wanaweza kuona, ili watu waweze kuona utimizaji hasa kwa macho yao wenyewe. Hii ni maana ya kina ya Mungu kuwa mwili. Yaani, kazi ya Roho imekamilika kupitia kwa mwili na neno. Hii ni maana ya kweli ya "Neno kuwa mwili, Neno kuonekana katika mwili."

8/09/2019

Matamshi ya Mungu | Sura ya 53

Mimi ndiye mwanzo, na Mimi ndiye mwisho. Mimi ndiye Mungu mmoja wa kweli aliyefufuka na kamili. Nasema maneno Yangu mbele yenu, na lazima muamini Ninachosema kwa thabiti. Mbingu na dunia zinaweza kupita lakini hakuna herufi moja au mstari mmoja wa kile Ninachosema kitawahi kupita. Kumbuka hili! Kumbuka hili! Punde ambapo Nimesema, hakuna neno hata moja limewahi kurudishwa na kila neno litatimizwa. Sasa wakati umewadia na lazima muingie katika uhalisi kwa haraka. Hakuna muda mwingi. 

8/08/2019

Neno la Mungu | Sura ya 57

Je, umechunguza kila fikira na mawazo yako, na kila tendo lako? Uko wazi kuhusu gani kati ya haya yanalingana na mapenzi Yangu na gani hayalingani? Huna uwezo wa kutambua haya! Mbona hujaja mbele Yangu? Je, ni kwa sababu Sitakuambia, au ni kwa ajili ya sababu nyingine? Unapaswa kujua hili! Kujua kwamba wale walio wazembe hawawezi kuyaelewa mapenzi Yangu kabisa au kupokea mwangaza na ufunuo mkuu.

8/07/2019

“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Ni Vipi Kuna Makosa Ndani ya Biblia? | Clip 5/6



“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Ni Vipi Kuna Makosa Ndani ya Biblia? | Swahili Gospel Movie Clip 5/6

Watu wengi wanaamini kwamba Biblia yote imetiwa msukumo na Mungu, kwamba imetoka kabisa kwa Roho Mtakatifu, na kwamba hakuna hata neno moja lililo na kosa. Je, mtazamo wa aina hii unawiana na ukweli? Biblia iliandikwa na waandishi zaidi ya 40, yaliyomo yaliandikwa na kupangwa na mwanadamu, na haikufunuliwa moja kwa moja na Roho Mtakatifu. Ilikuwa vigumu kuepuka kuingiza mawazo na makosa ya mwanadamu wakati ambapo ilikuwa ikiandikwa na kupangwa na mwanadamu.


8/06/2019

“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Je, Biblia Nzima Imetiwa Msukumo na Mungu Kweli? | Swahili Gospel Movie Clip 4/6



“Fichua Siri Kuhusu Biblia” – Je, Biblia Nzima Imetiwa Msukumo na Mungu Kweli? | Swahili Gospel Movie Clip 4/6


Watu wengi katika ulimwengu wa dini wanaamini kwamba "Kila andiko limetolewa kwa msukumo wa Mungu," yote katika Biblia ni neno la Mungu. Je, kauli ya aina hii inakubaliana na ukweli? Biblia ni ushahidi wa Mungu pekee, rekodi ya kazi ya Mungu tu, na haijaundwa kwa matamshi ya Mungu kikamilifu. Ndani ya Biblia, ni maneno yaliyonenwa na Yehova Mungu, maneno ya Bwana Yesu, unabii wa Ufunuo na maneno ya manabii yaliyotolewa kwa msukumo wa Mungu pekee, ndiyo neno la Mungu. Mbali na hayo, mengi ya yaliyosalia yanahusiana na rekodi za kihistoria na ushuhuda wa uzoefu wa mwanadamu. Ikiwa ungependa kujua undani wa Biblia, basi tafadhali angalia video hii!

Video Sawa: Filamu za Kikristo | "Toka Nje ya Biblia" | Is Believing in the Bible Believing in God?

8/05/2019

Neno la Mwenyezi Mungu | Sura ya 58

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Neno la Mwenyezi Mungu | Sura ya 58

Ukiielewa nia Yangu, utaweza kuufikiria mzigo Wangu na unaweza kupata mwanga na ufunuo, na kupata ufunguliwaji na uhuru, kuuridhisha moyo Wangu, kuyaruhusu mapenzi Yangu kwa ajili yako kutekelezwa, kuwaletea watakatifu wote ujenzi wa maadili, na kuufanya ufalme Wangu duniani kuwa imara na thabiti. Jambo la muhimu sasa ni kuelewa nia Yangu, hii ni njia mnayopaswa kuingia katika na hata zaidi ni wajibu wa kutimizwa na kila mtu.

8/04/2019

Matamshi ya Mungu | Utendaji (8)

Kuna mengi kupita kiasi juu ya watu ambayo yamekengeuka na yasiyo sahihi, hawawezi kamwe kujishughulikia wenyewe, na hivyo bado ni muhimu kuwaongoza katika kuingia kwenye njia sahihi; kwa maneno mengine, wana uwezo wa kudhibiti maisha yao ya kibinadamu na maisha ya kiroho, kuweka mambo yote mawili katika vitendo, na hakuna haja ya wao mara nyingi kusaidiwa na kuongozwa. Wakati huo tu ndipo watakuwa na kimo cha kweli. Hii itamaanisha kuwa, katika siku za baadaye, wakati ambapo hakuna mtu wa kukuongoza, utakuwa na uwezo wa kuwa na uzoefu mwenyewe.

8/03/2019

Neno la Mwenyezi Mungu | Sura ya 60

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Neno la Mwenyezi Mungu | Sura ya 60


Si jambo rahisi kwa maisha kukua; yanahitaji mchakato, na aidha, kwamba muweze kulipa gharama na kwamba mshirikiane na Mimi kwa uwiano, na hivyo mtapata sifa Yangu. Mbingu na dunia na vitu vyote vinaanzishwa na kufanywa kamili kupitia maneno ya kinywa Changu na chochote kinaweza kutimizwa nami. Matakwa Yangu ya pekee ni kwamba mkue haraka, mchukue mzigo kutoka kwa mabega Yangu na kuuweka kama wenu, mfanye kazi Zangu kwa niaba Yangu, na hilo litauridhisha moyo Wangu.

8/02/2019

Maigizo Yaliyosimuliwa ya Hadithi za Kweli "Upendo wa Kweli wa Mungu" (Swahili Subtitles)


Maigizo Yaliyosimuliwa ya Hadithi za Kweli "Upendo wa Kweli wa Mungu" (Swahili Subtitles)


Ili kujitengenezea nafasi yake mwenyewe duniani, mhusika mkuu alilazimika kufuata mwenendo wa duniani humu, akihangaika na kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya umaarufu na hadhi. Maisha yake yalilikuwa hasa matupu na yenye maumivu. Baada ya kumwamini Mwenyezi Mungu, alipata maana ya maisha ya binadamu ndani ya maneno ya Mwenyezi Mungu, na akiwa amejawa na furaha, akamfuata Mungu na kutimiza majukumu yake. Hata hivyo, kwa sababu moyo wake ulikuwa chini ya udhibiti wa umaarufu na hadhi, katika kutekeleza majukumu yake mara kwa mara alitenda kwa mujibu wa mawazo yake mwenyewe, na alikuwa dhalimu na mwenye udikteta.

8/01/2019

New Swahili Gospel Movie "Jina la Mungu Limebadilika?!" | Kufunua Siri ya Jina la Mungu



New Swahili Gospel Movie "Jina la Mungu Limebadilika?!" | Kufunua Siri ya Jina la Mungu


Jina lake ni Wang Hua, na ni mhubiri wa kanisa la nyumbani Kusini mwa Uchina. Baada ya kuanza kumwamini Bwana, alipata kwenye Biblia kuwa Mungu aliitwa Yehova katika Agano la Kale, na aliitwa Yesu katika Agano Jipya. Ni kwa nini Mungu ana majina tofauti? Wang Hua alishangazwa sana na hili. Alijaribu kutafuta jibu katika Biblia, lakini akakosa kuelewa fumbo hilo... Lakini alikuwa na imani thabiti kuwa hakuna jina lingine chini ya mbingu lililopewa wanadamu, hivyo Yesu pekee ndiye Mwokozi, na kuwa muradi tushikilie jina la Yesu, bila shaka tutanyakuliwa kuingia katika ufalme wa mbinguni.