12/20/2019

Matamshi ya Mungu | “Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake” (Sehemu ya Pili)



Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”.
Maudhui ya video hii:
Tembea katika Njia ya Mungu: Mche Mungu na Kuepuka Maovu
Mungu Hutumia Majaribio Tofauti ili Kupima Kama Watu Humcha Mungu na Kujiepusha na Maovu
Kutomcha Mungu na Kutojiepusha na Maovu ni Kumpinga Mungu

12/19/2019

Latest Swahili Praise and Worship Song | "Tuna Bahati Kukutana na Kuja kwa Mungu" | Tenzi ya Rohoni


Tuna bahati kukutana na kuja kwa mungu, twaisikia sauti Yake.

Tuna bahati kukutana na kuja kwa mungu, tunahudhuria sikukuu ya Mwanakondoo.

Tunamjua Mwenyezi Mungu mwenye mwili, tunaona matendo Yake ya ajabu.

Tunaelewa siri ya maisha ya mwanadamu, maneno ya Mwenyezi Mungu ni ya thamani zaidi.

Tunakula na kunywa maneno ya Mungu, na tunaishi mbele Yake,

tusitafute tena huku na kule.

Tunapopitia hukumu ya Mungu, ingawa tunaweza kuteseka, tunatakaswa.

Tunapata ukweli na njia ya uzima wa milele.

Tukitafuta kumpenda Mungu, hatutawahi kujuta.

12/18/2019

20. Asiyeamini ni nini?

Maneno Husika ya Mungu:
Kwa sababu unamwamini Mungu, basi lazima uweke imani ndani ya maneno yote ya Mungu na ndani ya kazi Yake yote. Hii ni kusema kwamba, kwa sababu unamwamini Mungu, ni lazima umtii. Kama huwezi kufanya hivi, basi haijalishi iwapo unamwamini Mungu. Kama umemwamini Mungu kwa miaka mingi, lakini hujawahi kumtii ama kuyakubali maneno Yake, na badala yake umemwuliza Mungu anyenyekee kwako na kufuata dhana zako, basi wewe ni mtu mwasi zaidi ya wote, na wewe si muumini. Mtu kama huyu anawezaje kutii kazi na maneno ya Mungu ambayo hayafuati fikira za mwanadamu?
kutoka katika “Wale Wanaomtii Mungu kwa Moyo wa Kweli Hakika Watapatwa na Mungu” katika Neno Laonekana katika Mwili

12/17/2019

Latest Swahili Worship Song 2019 | "Kwa Kuwa Mungu Anamwokoa Mwanadamu, Atamwokoa Kabisa"


I

Kwa kuwa Mungu alimuumba mwanadamu, Atamwongoza;

kwa kuwa Anamwokoa mwanadamu, Atamwokoa na kumpata kabisa;

kwa kuwa anamwongoza mwanadamu, Atamfikisha katika hatima sahihi.

Kwa kuwa Alimuumba mwanadamu na Anamsimamia,

ni lazima awajibikie matarajio na jalaa ya mwanadamu.

Ni hii ndiyo kazi inayofanywa na Muumba.

Ingawa kazi ya ushindi inafanikishwa ikiondoa matarajio ya jamii ya wanadamu,

mwishowe, mwanadamu bado ataletwa katika hatima sahihi ambayo Mungu amemwandalia.

12/16/2019

Wimbo wa Kwaya ya Injili | "Wimbo wa Ufalme: Ufalme Washuka Duniani" Mambo Muhimu 3: Mbingu na Dunia Mpya Baada ya Maafa | Wimbo wa Kuabudu



Wimbo wa kusisimua wa ufalme umevuma, ukitangazia ulimwengu wote kuwasili kwa Mungu kati ya mwanadamu! Ufalme wa Mungu umefika! Watu wote washangilia, vitu vyote vyafurahi! Kila kitu mbinguni kote kina furaha tele. Mandhari haya yanayopendeza mno ya shangwe ni yapi?

Miongoni mwa wanadamu, ni nani aishiye katika uchungu na ambaye amevumilia maelfu ya miaka ya upotovu wa Shetani, ambaye hatamani—hana hamu—ya kuwasili kwa Mungu? Je, ni waumini na wafuasi wangapi wa Mungu katika enzi zote, ambao chini ya ushawishi wa Shetani, wamevumilia taabu na dhiki, mateso na kutengwa? Ni nani asiyetumaini kuwa ufalme wa Mungu utakuja hivi karibuni? Baada ya kuonja furaha na masikitiko ya binadamu, ni nani kati ya wanadamu asiyetamani ukweli na haki vimiliki kati ya wanadamu?

12/15/2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Wote Wasiomjua Mungu Ndio Wanaompinga Mungu"

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Wote Wasiomjua Mungu Ndio Wanaompinga Mungu"


Mwenyezi Mungu anasema, "Wale Ninaosema wanampinga Mungu ni wale wasiomjua Mungu, wale wanaokiri Mungu na maneno matupu ilhali hawamjui, wale wanaomfuata Mungu lakini hawamtii, na wale wanaofurahia neema ya Mungu lakini hawawezi kumshuhudia. Bila ufahamu wa madhumuni ya kazi ya Mungu na kazi ya Mungu kwa mwanadamu, mwanadamu hawezi kuwa katika ulinganifu na moyo wa Mungu, na hawezi kumshuhudia Mungu. Sababu kwamba mwanadamu humpinga Mungu inatoka, kwa upande mmoja, katika tabia potovu ya mwanadamu, na kwa upande mwingine, kutokana na kutomfahamu Mungu na kutoelewa kanuni za kazi ya Mungu na mapenzi Yake kwa mwanadamu. Vipengele hivi viwili vinaunganishwa katika historia ya upinzani wa mwanadamu kwa Mungu."

12/14/2019

Unafiki ni nini?

Maneno Husika ya Mungu:
Ufafanuzi wa neno “Mfarisayo” ni upi? Ni mtu ambaye ni mnafiki, ambaye ni bandia na anajifanya katika kila kitu anachofanya, akijifanya kuwa mwema, mwenye fadhila, na mzuri. Je, hivyo ndivyo alivyo kwa kweli? Yeye ni mnafiki, na hivyo kila kitu kinachodhihirika na kufichuliwa ndani yake ni cha uongo, yote ni kujifanya—sio hali yake ya kweli. Hali yake ya kweli imefichwa ndani ya moyo wake; haionekani. Watu wasipofuatilia ukweli, kama hawaelewi ukweli, basi maarifa yao ya kidini na nadharia ambazo wamepata zinakuwa nini? Je, zinakuwa maneno ya mafundisho ambayo watu huzungumzia mara nyingi? Watu hutumia haya yanayodaiwa kuwa mafundisho sahihi kujifanya na kujionyesha kuwa wazuri. Popote waendapo, mambo wanayozungumzia, mambo wanayoyasema, na tabia yao ya nje huonekana kuwa sawa na nzuri kwa wengine. Yote yanalingana na fikira na mapendeleo ya mwanadamu. Machoni pa wengine, wao ni wenye kumcha Mungu na wanyenyekevu. Wao ni wavumilivu, wastahimilivu, na wenye upendo kwa wengine. Kwa kweli, yote ni bandia—yote ni kujifanya. Kwa nje, wao ni waaminifu kwa Mungu, lakini kisirisiri, kila kitu wanachofanya ni cha uzembe. Kwa juujuu, wameacha familia zao na kazi zao, wanajitahidi kwa bidii na hujitumia—lakini kwa kweli wanafaidika kisirisiri kutoka kwa kanisa na kuiba sadaka! Kila kitu wanachofichua kwa nje, tabia yao yote ni bandia! Hii ndiyo maana ya Mfarisayo mnafiki. “Mafarisayo”—watu hawa hutoka wapi? Je, wanajitokeza kati ya wasioamini? Wote hujitokeza kati ya wasioamini. Kwa nini waumini hawa hugeuka kuwa hivyo? Inaweza kuwa kwamba maneno ya Mungu yaliwafanya wawe namna hiyo? Sababu ya wao kuwa namna hiyo ni hasa kwamba waliichukua njia mbaya. Wanayachukulia maneno ya Mungu kama chombo cha kujihami nacho; wanajihami na maneno haya na kuyachukulia kama mtaji wa kupata riziki, kupata kitu bila kutoa chochote. Hawafanyi chochote ila kuhubiri mafundisho ya kidini, na hawajawahi kufuata njia ya Mungu. Tabia yao inayokisiwa kuwa nzuri na mwenendo mzuri, hicho kidogo ambacho wameacha na kutumia kimelazimishwa kabisa, yote ni uigizaji tu wanaofanya. Yote ni bandia kabisa; yote ni kujifanya. Katika mioyo ya watu hawa hakuna uchaji kwa Mungu hata kidogo, na hawana hata imani yoyote ya kweli kwa Mungu. Zaidi ya hayo, wao ni wa wasioamini. Watu wasipofuatilia ukweli, watatembea njia ya aina hii, na watakuwa Mafarisayo. Je, hili silo jambo la kuhofisha?

12/13/2019

Kiongozi wa uongo au mchungaji wa uongo ni nini? Je, kiongozi wa uongo au mchungaji wa uwongo anaweza kutambuliwaje?

Maneno Husika ya Mungu:
Wale ambao wanaweza kufuata kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu, na ambao wanaweza kuzifuata nyayo za Mungu, kiasi kwamba wamfuate Mungu popote Awaongozapo—hawa ni watu ambao wamebarikiwa na Mungu. Wale wasiofuata kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu hawajaingia katika kazi ya maneno ya Mungu, na haijalishi wanafanya kazi kiasi gani, au mateso yao ni makubwa vipi, au wanakimbia hapa na pale kiasi gani, hakuna linalomaanisha chochote kwa Mungu kati ya hayo, na Yeye hatawasifu. Leo, wale wote ambao hufuata maneno halisi ya Mungu wako ndani ya mkondo wa Roho Mtakatifu; wale ambao ni wageni kwa maneno halisi ya Mungu wako nje ya mkondo wa Roho Mtakatifu, na watu hao hawasifiwi na Mungu. Huduma ambayo imetenganishwa na matamshi halisi ya Roho Mtakatifu ni huduma ambayo ni ya mwili, na ya dhana, na haiwezi kuwa kwa mujibu wa mapenzi ya Mungu. Kama watu huishi miongoni mwa dhana za kidini, basi hawawezi kufanya lolote lenye kustahili kwa mapenzi ya Mungu, na hata ingawa wao humhudumia Mungu, wao huhudumu katikati ya mawazo na dhana zao, na hawawezi kabisa kuhudumu kwa mujibu wa mapenzi ya Mungu. Wale ambao hawawezi kuifuata kazi ya Roho Mtakatifu hawaelewi mapenzi ya Mungu, na wale ambao hawaelewi mapenzi ya Mungu hawawezi kumhudumia Mungu. Mungu hutaka huduma inayoupendeza moyo Wake mwenyewe; Hataki huduma ambayo ni ya dhana na mwili. Kama watu hawawezi kuzifuata hatua za kazi ya Roho Mtakatifu, basi wao huishi katikati ya dhana, na huduma ya watu hao hukatiza na huvuruga. Huduma hiyo huenda kinyume na Mungu, na hivyo wale ambao hawawezi kuzifuata nyayo za Mungu hawawezi kumhudumia Mungu; wale ambao hawawezi kuzifuata nyayo za Mungu humpinga Mungu bila shaka, na ni wasioweza kulingana na Mungu.

12/12/2019

Kristo wa uongo ni nini? Kristo wa uongo anaweza kutambuliwaje?

Maneno Husika ya Mungu:
Ikiwa mwanadamu atajiita Mungu lakini hawezi kuonyesha uungu na kufanya kazi ya Mungu Mwenyewe, au amwakilishe Mungu, bila shaka si Mungu kwani hana sifa za Mungu, na kile ambacho Mungu Anaweza kukitimiza hakimo ndani yake.
kutoka katika “Tofauti Kati ya Huduma ya Mungu Mwenye Mwili na Wajibu wa Mwanadamu” katika Neno Laonekana katika Mwili
Yeye Aliye mwili wa Mungu Atakuwa na dutu ya Mungu, na Yule Aliye Mungu katika mwili Atakuwa na maonyesho ya Mungu. Kwa maana Mungu Hupata mwili, Ataleta mbele kazi Anayopaswa kufanya, na kwa maana Mungu Amepata mwili, Ataonyesha kile Alicho na Ataweza kuuleta ukweli kwa mwanadamu, kumpa mwanadamu uhai, na Amwonyeshe mwanadamu njia. Mwili usio na dutu ya Mungu kwa kweli sio Mungu mwenye mwili; kwa hili hakuna tashwishi. Kupeleleza kama kweli ni mwili wa Mungu mwenye Mwili, mwanadamu lazima aamue haya kutoka kwa tabia Yeye huonyesha na maneno Yeye hunena. Ambayo ni kusema, kama ni mwili wa Mungu mwenye mwili au la, na kama ni njia ya kweli au la, lazima iamuliwe kutokana na dutu Yake. Hivyo, katika kudadisi[a] iwapo ni mwili wa Mungu mwenye mwili, cha msingi ni kuwa makini kuhusu dutu Yake (Kazi Yake, maneno Yake, tabia Yake, na mengine mengi), bali sio hali ya sura Yake ya nje.

12/11/2019

Mpinga Kristo ni nini? Mpinga Kristo anaweza kutambuliwaje?

Maneno Husika ya Mungu:
Kwa wakati ambao Mungu bado hakuwa amegeuka mwili, kipimo cha iwapo mwanadamu alimpinga Mungu kilitegemea iwapo mwanadamu alimwabudu na kumheshimu Mungu aliye mbinguni asiyeonekana. Ufafanuzi wa upinzani kwa Mungu wakati huo haukuwa halisi, kwani mwanadamu wakati huo hangemwona Mungu wala kujua mfano wa Mungu ama jinsi Alivyofanya kazi na kuongea. Mwanadamu hakuwa na dhana za Mungu na alimwamini Mungu kwa njia isiyo dhahiri, kwani Hakuwa amejitokeza kwa mwanadamu. Kwa hivyo, vile mwanadamu alivyomwamini Mungu katika mawazo yake, Mungu hakumlaumu mwanadamu ama kuulizia mengi kutoka kwa mwanadamu, kwani mwanadamu hangemwona Mungu hata kidogo. Mungu anapopata mwili na kuja kufanya kazi miongoni mwa wanadamu, wote wanamtazama Mungu na kusikia maneno Yake, na wote wanaona vitendo vya Mungu katika mwili. Wakati huo, dhana zote za mwanadamu zinafutwa na kubaki povu tu. Kwa wale wanaomwona Mungu anayejitokeza katika mwili, wote walio na utiifu ndani ya mioyo yao hawalaaniwi, ilhali wanaosimama dhidi Yake kimakusudi watachukuliwa kuwa wapinzani wa Mungu. Wanadamu kama hao ni maadui wa Kristo na ni maadui wanaosimama dhidi ya Mungu kimakusudi.

12/10/2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima Tamko La Nane"

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima Tamko La Nane"


Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

12/09/2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima Tamko la Kumi na Sita"

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima Tamko la Kumi na Sita"


Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

12/08/2019

Matamshi ya Mungu | "Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IV Utakatifu wa Mungu (I)" (Sehemu ya Kwanza)

Matamshi ya Mungu | "Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IV Utakatifu wa Mungu (I)" (Sehemu ya Kwanza)



Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu "Neno Laonekana katika Mwili".

Maudhui ya video hii:
Amri ya Yehova Mungu kwa Mwanadamu
Nyoka Anamshawishi Mwanamke

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.