Mwenyezi Mungu alisema, Watu wote wamepitia usafishaji kwa sababu ya maneno ya Mungu. Kama sio Mungu mwenye mwili wanadamu bila shaka hawangebarikiwa kuteseka hivyo. Inaweza pia kusemwa hivi—wale wanaoweza kukubali majaribio ya maneno ya Mungu ni watu waliobarikiwa. Kulingana na ubora wa akili wa watu wa asili, mwenendo wao, mitazamo yao kwa Mungu, hawastahili kupokea aina hii ya usafishaji. Ni kwa sababu wameinuliwa na Mungu ndio wamefurahia baraka hii. Watu walikuwa wakisema kwamba hawakustahili kuuona uso wa Mungu au kusikia maneno Yake. Leo ni kwa sababu tu ya kutiwa moyo na Mungu na fadhili Zake ndio watu wamepokea usafishaji wa maneno Yake.
"Mungu anatekeleza hatua ya kazi kubwa kila wakati yeye hujifunua. Kazi hii ni tofauti na ile ya enzi mwingine yoyote. Haiwezi kufikiriwa na mtu, na haijawahi kujifunza na mwanadamu. Ni kazi ambayo huanza enzi mpya na huhitimisha enzi, na ni aina mpya ya kazi kwa ajili ya wokovu wa wanadamu; Zaidi ya hayo, ni kazi ya kuwaleta wanadamu katika wakati mpya. Hiyo ni umuhimu wa kuonekana kwa Mungu. kutoka kwa Neno Laonekana Katika Mwili"
4/13/2018
4/12/2018
Maneno ya Yesu kwa Wanafunzi Wake Baada ya Kufufuka Kwake | Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III
12. Maneno ya Yesu kwa Wanafunzi Wake Baada ya Kufufuka Kwake
(Yohana 20:26-29) Na baada ya siku nane wanafunzi wake walikuwa ndani tena, na Tomaso pamoja nao: Kisha akaja Yesu, na milango imefungwa, na akasimama katikati, kisha akasema, Amani iwe kwenu. Kisha akamwambia Tomaso, Weka hapa kidole chako, na utazame mikono yangu; na ulete mkono wako uuweke ubavuni mwangu, na usiwe asiyeamini, bali uwe aaminiye. Naye Tomaso akajibu akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu! Yesu akamwambia, Tomaso, kwa kuwa umeniona, umeamini; heri wanayo wale ambao hawajaona, ilhali wameamini.

(Yohana 21:16-17) Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yona, je, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana; wewe unajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha kondoo wangu. Akamwambia mara ya tatu, Simoni, mwana wa Yona, je, unanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, je, unanipenda? Na akamwambia, Bwana, wewe unajua mambo yote; wewe unajua ya kwamba nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.
Mungu Kuja Duniani na Kuwa Sadaka ya Dhambi

~~~~~~~~~~~~~~ ~~~~~~~~~~~~~~
×××××××××××××××××××
👇👇🌺🌺🌺👇👇🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺🌺👇👇🌺🌺🌺👇👇🌺🌺🌺
Mwenyezi Mungu alisema, Ndani ya upana wa kazi ambayo Bwana Yesu alikamilisha katika Enzi ya Neema, unaweza kuona kipengele kingine cha kile Alicho nacho Mungu na kile Alicho. Kilielezewa kupitia kwa mwili Wake, na kikawezeshwa kwa watu kuiona na kufahamu zaidi kupitia kwa ubinadamu Wake.
4/11/2018
Uchaguzi Kutoka katika Mafungu Kumi ya Neno la Mungu juu ya “Kazi na Kuingia”
1. Tangu watu waanze kukanyaga njia sahihi ya maisha, kumekuwa na mambo mengi ambayo bado hayajaeleweka vizuri. Bado wapo kwenye mkanganyiko kabisa kuhusu kazi ya Mungu, na kuhusu kiasi gani cha kazi wanapaswa kufanya. Hii, kwa upande mmoja, ni kwa sababu ya kuwa na uelekeo tofauti wa uzoefu wao na mipaka katika uwezo wao wa kupokea; kwa upande mwingine, ni kwa sababu kazi ya Mungu bado haijawaleta watu katika hatua hii. Kwa hiyo, kila mtu anapata utata kuhusu masuala mengi ya kiroho. Sio tu kwamba hamna uhakika kuhusu kile ambacho mnapaswa kuingia kwacho; bali pia ni wajinga kuhusu kazi ya Mungu.
Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VI

Neno la Mwenyezi Mungu | Utakatifu wa Mungu (III)
Mnahisi vipi baada ya kusema sala zenu? (Tunafurahia na kuguswa sana.) Wacha tuanze ushirika wetu. Tulishiriki mada ipi wakati uliopita? (Utakatifu wa Mungu.) Na ni kipengele kipi cha Mungu Mwenyewe kinahusisha utakatifu wa Mungu? Je, kinahusisha kiini cha Mungu? (Ndiyo.) Kwa hivyo ni nini hasa mada inayohusiana na kiini cha Mungu? Je, ni utakatifu wa Mungu? (Ndiyo.) Utakatifu wa Mungu: hiki ni kiini cha kipekee cha Mungu. Ni nini ilikuwa dhamira kuu tuliyoshiriki wakati uliopita? (Kutambua uovu wa Shetani.) Na ni yapi tuliyoyashiriki wakati uliopita kuhusu uovu wa Shetani? Mnaweza kukumbuka? (Jinsi Shetani anampotosha mwanadamu. Anatumia maarifa, sayansi, desturi ya kitamaduni, ushirikina, na mienendo ya kijamii kutupotosha.) Sahihi, hii ndiyo ilikuwa mada kuu tuliyojadili wakati uliopita.4/10/2018
Matamshi ya Mwenyezi Mungu | (III) Aina Tano za Watu
Matamshi ya Mwenyezi Mungu | (III) Aina Tano za Watu
Kwa sasa, Nitaacha ushirika wetu kuhusu tabia ya haki ya Mungu umalizikie hapo. Kinachofuata Nitaainisha wafuasi wa Mungu katika kategoria mbalimbali, kulingana na ufahamu wao wa Mungu na ufahamu wao na kile wamepitia kuhusiana na tabia ya haki Yake, ili muweze kujua awamu ambayo kwa sasa mnapatikana ndani pamoja na kimo chenu cha sasa. Kuhusiana na maarifa yao ya Mungu na ufahamu wao wa tabia Yake ya haki, awamu na kimo tofauti ambavyo watu huwa navyo vinaweza kugawanywa katika aina tano. Mada hii imeelezewa kwa msingi wa kumjua Mungu wa kipekee na tabia Yake ya haki; kwa hivyo, unaposoma maudhui yafuatayo, unafaa kujaribu kwa makini kuchambua ni kiwango kipi haswa cha ufahamu na maarifa ulichonacho kuhusiana na upekee wa Mungu na tabia Yake ya haki, na kisha utumie hayo kujua ni awamu gani ambayo kwa kweli unapatikana ndani, kimo chako ni kikubwa vipi kwa kweli, na wewe ni aina gani ya mtu kwa kweli.11. Kupitia Utunzaji wa Uangalifu wa Mungu wa Wokovu wa Mwanadamu katika Maafa⭐❤️

➛➛➛➛➝➝➝➝➜➜➜➜➞➞➞➞➟➟➟➟➠➠➠➠➡➡➡➡➢➢➢➢➤➤➤➤➤
*****************⭐*****************💓💓💓*****************⭐*****************
~~~~~~~~👇~~~~~~~~~~~~~~~👇~~~~~~~~
Muling , Beijing
Agosti 16, Mwaka wa 2012
*****************⭐*****************💓💓💓*****************⭐*****************
~~~~~~~~👇~~~~~~~~~~~~~~~👇~~~~~~~~
Muling , Beijing
Agosti 16, Mwaka wa 2012
Mnamo Julai 21, mwaka wa 2012, Beijing ilipata mvua kubwa zaidi katika miaka sitini. Katika mvua hiyo kubwa niliona matendo ya Mungu na kuona jinsi Yeye huwaokoa mwanadamu.
Siku hiyo adhuhuri, dada zangu watatu na mimi tulikuwa tumekutana. Nje mvua ilikuwa ikiendelea kunyesha. Saa kumi u nusu jioni mume wangu, ambaye hakuwa muumini, alirudi akitwambia kwamba kulikuwa na maji mengi kwa mzunguko kiasi kwamba watu hawakuweza kupitia. Hata hivyo, saa kumi na moja jioni aliondoka kwa haraka sana kwenda kwa zamu yake ya usiku kazini.
4/09/2018
Maono ya Kazi ya Mungu (3)

Mwenyezi Mungu alisema, Mara ya kwanza Mungu alipopata mwili ilikuwa kupitia kutungwa mimba kwa Roho Mtakatifu, na ilihusiana na kazi Aliyokusudia kufanya. Jina la Yesu liliashiria mwanzo wa Enzi ya Neema. Wakati Yesu Alianza kufanya huduma Yake, Roho Mtakatifu Alianza kutoa ushuhuda kwa jina la Yesu, na jina la Yehova halikuzungumziwa tena, na badala yake Roho Mtakatifu Alianza kazi mpya hasa kwa jina la Yesu. Ushuhuda wa wale waliomwamini Yeye ulitolewa kwa ajili ya Yesu Kristo, na kazi waliyoifanya walifanya pia kwa ajili ya Yesu Kristo. Hitimisho Enzi ya Sheria ya Agano la Kale lilimaanisha kuwa kazi iliyofanywa hasa kutumia jina la Yehova ilikuwa imefikia kikomo. Baada ya hii, jina la Mungu halikuwa Yehova tena;
Kanisa la Mwenyezi Mungu | Mjadala Kati ya Njia Mbili za Maisha na Kifo🎬🔔
Chama cha Kikomunisti cha China kinakandamiza kwa hasira na kushambulia imani ya kidini. Wanawafunga jela na kuwatesa kikatili Wakristo bila kujizuilia. Wanawaruhusu watu tu kufuata Chama cha Kikomunisti. Hawawaruhusu watu kumwamini Mungu na kumfuata Mungu wanapotembea njia sahihi ya maisha. Matokeo ya mwisho ya Chama cha Kikomunisti cha China yatakuwa nini? Chini ya ukandamizaji, ukamataji na utesaji wa hasira wa Chama cha Kikomunisti cha China, Wakristo kwa thabiti wanaendelea kumfuata Mungu, wakieneza injili na kuwa na ushuhuda kwa Mungu. Sababu ya hili ni nini? Katika Video hii, mjadala mzuri kati ya Mkristo na maafisa wa Chama cha Kikomunisti cha China utafichua njia hizi mbili tofauti ambazo zinaelekea kwa miisho miwili tofauti katika maisha yetu.
4/08/2018
Kifo: Awamu ya Sita | Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kifo: Awamu ya Sita
Baada ya mahangaiko mengi na masikitiko mengi, na kuvunjwa moyo kwingi, baada ya furaha nyingi na huzuni nyingi na baada ya misukosuko ya maisha, baada ya miaka mingi sana isiyosahaulika, baada ya kutazama misimu ikipita na kujirudia, mtu hupita kwenye kiungo muhimu sana cha maisha bila ya arifa, na kwa ghafla tu mtu anajipata kwenye miaka yake ya kufifia. Alama za muda zimejichora kotekote kwenye mwili wa mtu: Mtu hawezi tena kusimama wima, kichwa cha nywele nyeusi kinageuka na kuwa cha nywele nyeupe, macho maangavu na mazuri yanabadilika na kuanza kufifiliza na kuwa na wingu mbele yao, nayo ngozi laini, yenye unyumbufu inageuka na kuwa na makunyanzi na madoadoa.Sura ya 46. Ni Kwa Kuujua Uweza wa Mungu Pekee Ndipo Unaweza Kuwa na Imani ya Kweli
Mwenyezi Mungu alisema, Wengi wa watu hawaelewi kazi ya Mungu na si rahisi kuelewa kipengele hiki. Kitu cha kwanza ambacho lazima ujue ni kwamba kunawakati ulioteuliwa wa kazi yote ya Mungu na bila shaka si kama ilivyodhaniwa na watu. Mwanadamu hawezi kamwe kuelewa kazi ambayo Mungu ataifanya ama wakati Ataifanya. Anafanya sasa kile kinachostahili kufanywa sasa na hiki ni kitu ambacho hakuna anayeweza kukiharibu; Anafanya baadaye kile kinachostahili kufanywa baadaye, na hachelewi hata kwa sekunde moja, na hakuna anayeweza kuharibu jambo hilo pia. Kanuni ya kazi Yake ni kwamba inafanywa kulingana na mipango Yake, wakati huo pia ikifanywa kulingana na mapenzi Yake.
Uhuru: Awamu ya Tatu | Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III

Neno la Mwenyezi Mungu | Uhuru: Awamu ya Tatu
Baada ya mtu kupita utoto na wakati wake wa kubaleghe na kwa utaratibu bila kuzuilika kufikia ukomavu, hatua inayofuata ni kwake yeye kuuaga kabisa ule ujana wake, kuwaaga wazazi wake, na kukabiliana na barabara iliyo mbele yake akiwa mtu mzima huru. Wakati huo[c] lazima wakabiliane na watu, matukio na mambo yote ambayo mtu mzima lazima apitie, na kukabiliana na viungo mbalimbali katika msururu wa hatima yake. Hii ndiyo awamu ya tatu ambayo lazima mtu apitie.1. Baada ya Kuwa Huru, Mtu Huanza Kupitia Ukuu wa Muumba
Kama kuzaliwa kwa mtu na kulelewa kwake ni “kipindi cha matayarisho” katika safari ya mtu maishani, kuweka lile jiwe la msingi katika hatima ya mtu, basi uhuru wa mtu ndio mazungumzo nafsi ya kufungua hatima ya maisha ya mtu.4/07/2018
Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III

Neno la Mwenyezi Mungu | Mamlaka ya Mungu (II)
Leo tutaendelea na ushirika wetu kuhusu mada ya “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee.” Tayari tumekuwa na ushirika mara mbili katika mada hii, wa kwanza kuhusiana na mamlaka ya Mungu na wa pili kuhusiana na tabia ya haki ya Mungu. Baada ya kusikiliza ushirika huu mara mbili, je, umepata ufahamu mpya wa utambulisho wa Mungu, hadhi, na hali halisi? Je, maono haya yamekusaidia kufikia maarifa mazito zaidi na uhakika wa ukweli kuuhusu uwepo wa Mungu? Leo Ninapanga kufafanua mada hii ya “Mamlaka ya Mungu.”Kuelewa Mamlaka ya Mungu Kutoka kwa Mitazamo Mikubwa na Midogo
Mamlaka ya Mungu ni ya kipekee. Ndiyo maonyesho ya sifa ya, na hali halisi maalum ya, utambulisho wa Mungu Mwenyewe. Hakuna kiumbe ambacho kiliumbwa wala kile ambacho hakikuumbwa kinachomiliki maonyesho ya sifa kama hizi na hali halisi maalum;
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)