Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Katika-Mwili. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Katika-Mwili. Onyesha machapisho yote

10/24/2018

Swahili Christian Sketch "Onyo Kutoka kwa Historia" (Kichekesho)


Miaka elfu mbili iliyopita, wakati Bwana Yesu alipotokea na kufanya kazi, Mafarisayo walikwamia sheria na kukashifu kazi Yake, wakisema kuwa kazi Yake ilienda zaidi ya Maandiko.Ili kulinda hali zao na maisha yao, walijitahidi kwa nguvu zao zote ili kuwazuia watu kutafuta kazi ya Bwana Yesu, na kujiunga na serikali ya Kirumi kumsulubisha msalabani.

9/24/2018

Je, Kuna Msingi Katika Biblia wa Kurudi kwa Bwana Kupitia Kupata Mwili?



πŸŒΊπŸŒΊπŸŒΊπŸŒΊπŸŒΊπŸŒΊπŸŒΊπŸŒΊπŸ’•πŸ’•πŸ’•πŸ’•πŸ’•πŸ’•πŸ’•πŸ’•πŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’ž

"Njia ya Kwenda katika Ufalme wa Mbinguni ni Yenye Hatari" (2) - Je, Kuna Msingi Katika Biblia wa Kurudi kwa Bwana Kupitia Kupata Mwili? 


Watu wengi katika kukaribisha kuja kwa mara ya pili kwa Bwana wanaweka umuhimu tu katika unabii ulio katika Maandiko kwamba Bwana atashuka kutoka mawinguni kuja tena huku wakipuuza unabii kwamba kuja kwa pili kwa Bwana ni kupitia kupata mwili. Wanatangaza kuwa ya uongo njia yoyote ambayo inashuhudia kuja kwa mara ya pili kwa Bwana kama Mungu kuwa mwili. Je, ufahamu wao na kutenda kwao kunapatana na Maandiko? Kuhusu kurudi kwa Bwana kupitia kupata mwili, je, kumetabiriwaje hasa katika Maandiko?

Sikiliza zaidi: Neno la Mwenyezi Mungu, Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

9/12/2018

Maana ya Mateso na ni Mateso ya Aina Gani Ambayo Waumini wa Mungu Lazima Wastahimili

Sura ya 7 Vipengele Vingine vya Ukweli Ambavyo Unafaa Kueleweka Katika Imani Yako kwa Mungu

6. Maana ya Mateso na ni Mateso ya Aina Gani Ambayo Waumini wa Mungu Lazima Wastahimili

Maneno Husika ya Mungu:
Leo, watu wengi sana hawana ufahamu huo. Wao huamini kwamba mateso hayana thamani, wao hukanwa na ulimwengu, maisha yao ya nyumbani yamesumbuliwa, wao si wapendwa wa Mungu, na matazamio yao ni matupu. Kuteseka kwa watu wengine hufikia kiwango fulani, na fikira zao hugeukia kifo. Huu si upendo wa kweli kwa Mungu; watu kama hao ni waoga, hawana ustahamilivu, wao ni wadhaifu na wasio na nguvu!

9/11/2018

Ee Mungu, Unajua Nakukosa Wewe

Moyo wangu unakupenda sana. Lakini nahisi kuwa sifai upendo Wako.
Mnyonge sana sifai kuwa katika uwepo Wako, nina hofu sana na wasiwasi!
Naweza tu kuamua; kutoa nafsi yangu yote Kwako.
Nitateseka kwa ajili Yako, nipipitie mateso yote, hadi pumzi ya mwisho ya maisha yangu.
Mungu! Unajua kuwa nasubiri, nasubiri Wewe urejee.

9/07/2018

Nyimbo ya Msifuni Mwenyezi Mungu | Katika Mapana na Marefu, Mwaminifu Hadi Kifo

Nyimbo ya Msifuni Mwenyezi Mungu | Katika Mapana na Marefu, Mwaminifu Hadi Kifo

Kutoka mbinguni hadi duniani, Akijificha katika mwili.
Akifanya kazi miongoni mwa wanadamu, katika upepo na mvua.
Ukachukua njia ngumu, ukafungua enzi mpya.
Kumkomboa mwanadamu, kutoa maisha Yako na kumwaga damu.
Upepo na mvua, miaka mingi sana. Kutelekezwa na kila mwanadamu.

7/28/2018

Mungu Kupata Mwili Ni Nini? Kiini cha Mungu Kupata Mwili Ni Nini?

Sura ya 5 Ukweli Kuhusu Mungu Kupata Mwili

1. Mungu Kupata Mwili Ni Nini? Kiini cha Mungu Kupata Mwili Ni Nini?

Maneno Husika ya Mungu:
Maana ya kupata mwili ni kwamba Mungu Anajionyesha katika mwili, na Anakuja kufanya kazi miongoni mwa wanadamu wa uumbaji Wake katika umbo la mwili. Hivyo, ili Mungu kuwa mwili, ni lazima kwanza Apate umbo la mwili, mwili wenye ubinadamu wa kawaida; hili ndilo hitaji la kimsingi zaidi. Kwa kweli, maana ya kupata mwili kwa Mungu ni kwamba Mungu Anaishi na kufanya kazi katika mwili, Mungu katika kiini Chake Anakuwa mwili, Anakuwa mwanadamu. Maisha Yake ya kimwili na kazi vinaweza kugawanywa katika hatua mbili. Kwanza ni maisha Anayoishi kabla ya kuanza kutekeleza huduma Yake.

7/19/2018

Umuhimu wa Kazi ya Mungu ya Maneno

Sura ya 4 Ukweli wa Kazi ya Mungu ya Siku za Mwisho

1. Umuhimu wa Kazi ya Mungu ya Maneno

Maneno Husika ya Mungu:
Katika Enzi ya Ufalme, Mungu anatumia neno ili kukaribisha enzi mpya, ili kubadilisha mbinu za kazi Yake, na kuweza kufanya kazi katika enzi nzima. Hii ndiyo kanuni ambayo kwayo Mungu hufanya kazi katika Enzi ya Neno. Alikuwa mwili ili kuweza kuzungumza kutoka mitazamo tofauti, kumwezesha binadamu kumwona Mungu kwa kweli, ambaye ni Neno linaloonekana katika mwili, na hekima Yake na maajabu. Kazi kama hiyo inafanywa ili kwa njia bora zaidi kutimiza shabaha za kumshinda binadamu, kumkamilisha binadamu, na kumwondoa binadamu.

7/15/2018

Mungu Mmoja Wa Kweli Ameonekana katika Mwili

Radi inanguruma, ikitingiza mbingu. Mungu mmoja wa kweli ameonekana!
Ni sauti ya Roho Mtakatifu mwenyewe na ushuhuda Wake,
kama sauti ya radi kutoka mbingu. Amina! Amina!
Tunathibitisha Mungu ameonekana katika mwili.
Mwokozi amerejea, juu ya wingu jeupe.

6/23/2018

Nyimbo ya Msifuni Mwenyezi Mungu | Maisha Yetu Sio Bure

Nyimbo ya Msifuni Mwenyezi Mungu  | Maisha Yetu Sio Bure

Maisha yetu sio bure.
Maisha yetu sio bure.

🎧🎧🎧🎧🎧🎧~~~~~🎼🎼🎼🎼🎼~~~~~~😍😍😍
I
Leo tunakutana na Mungu,
tunapitia kazi Yake.
Tumemjua Mungu katika mwili,
wa utendaji na wa hakika.

6/05/2018

Ee Mwenyezi Mungu, Mpendwa Wangu Mzuri

Mwenyezi Mungu, mpendwa wangu mzuri, Una moyo wangu.
Unapitia magumu, Unavumilia aibu, yote kwa ajili ya kutuokoa.
Unatoa maisha Yako kwangu, naona jinsi Ulivyo mzuri.
Unakuja duniani kutoka mbinguni, ukiwa mwenye mwili.
Uko hapa Ukiishi na sisi, lakini hakuna anayejua Wewe ni nani.
Sikuota kamwe kuwa Muumba Mwenyewe angekuja ulimwenguni.
Aa … mpendwa wangu! Aa … mpendwa wangu!

5/01/2018

Kuendeleza Ubora wa Tabia ni Kwa Ajili ya Kupokea Wokovu wa Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Kuendeleza ubora wa tabia ya watu kunahitaji kwamba muendeleze uwezo wenu wa kupokea. Hitaji la msingi kabisa kwenu ni kwamba myapokee waziwazi maneno yanayonenwa kwenu. Je, siyo imani iliyovurugika ikiwa unanifuata bila kufahamu kile Ninachosema? Ubora wenu wa tabia ni duni sana. Ni kwa sababu hammiliki uwezo wa kupokea kwamba hamna ufahamu hata mdogo wa kile kinachosemwa. Kwa hivyo, ni vigumu sana kutimiza matokeo yanayotamanika. Mambo mengi hayawezi kusemwa kwenu moja kwa moja na athari ya awali haiwezi kutimizwa. Kwa hiyo, kazi za ziada zinapaswa kuongezwa kwa kazi Yangu.

3/30/2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Sura ya 12

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Sura ya 12

    Mwenyezi Mungu alisema,Watu wote wanapotilia maanani, wakati vitu vyote vinafanywa upya na kuhuishwa, wakati kila mtu anamtii Mungu bila shaka, na yuko tayari kubeba jukumu zito la mzigo wa Mungu—hapa ndipo wakati umeme wa mashariki unatoka, ukiangaza yote kutoka Mashariki hadi Magharibi, ukiyatisha yote ya ulimwengu na ujaji wa mwanga huu; na wakati huu, Mungu tena huanza maisha Yake mapya. Ambayo ni kusema, wakati huu Mungu huanza kazi mpya duniani, akitangaza kwa watu wa ulimwengu wote kwamba “Wakati umeme unatoka Mashariki—ambapo pia ni wakati hasa Naanza kunena—wakati umeme unakuja, mbingu yote inaangaziwa, na nyota zote zinaanza kubadilika."

2/23/2018

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 6

 Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 6

Kwa masuala ya ndani ya roho, unapaswa kuwa makini kwa utaratibu; kwa maneno Yangu, unapaswa kuwa msikivu kwa makini. Unapaswa kulenga hali ambayo unaona Roho Yangu na nafsi Yangu ya mwili, maneno Yangu na nafsi Yangu ya mwili, kama kitu kimoja kizima kisichogawanyika, na kufanya kuwa binadamu wote wataweza kuniridhisha mbele Yangu. Nimetembea ulimwenguni kwa miguu Yangu, Nikinyoosha macho Yangu juu ya anga yake nzima, na Nimetembea miongoni mwa wanadamu wote, Nikionja ladha tamu, ya asidi, chungu, na kali za uzoefu wa binadamu, lakini mwanadamu hakuwahi kweli kunitambua, wala hakuniona Nikitembea ng’ambo.

12/21/2017

Yote Yanafanikishwa Kupitia kwa Neno la Mungu

neno la Mungu,siku za mwisho,
    Mwenyezi Mungu alisema, Mungu huzungumza maneno Yake na kufanya kazi Yake kulingana na enzi tofauti, na katika enzi tofauti, Anazungumza maneno tofauti. Mungu hafuati sheria, ama kurudia kazi ya awali, ama kuhisi hali ya kumbukumbu kwa vitu vilivyopita; ni Mungu ambaye ni mpya kila wakati na hazeeki, na kila siku anazungumza maneno mapya. Lazima uyafuate yale ambayo lazima yafuatwe leo; haya ni majukumu na kazi ya mwanadamu. Ni muhimu kwamba utendaji uwekwe katika nuru iliyopo na maneno ya Mungu. Mungu hafuati masharti, na Anaweza kuzungumza kutoka kwa mitazamo mingi tofauti ili kufanya wazi hekima Yake na uwezo.

11/18/2017

Tofauti Muhimu Kati ya Mungu Aliyepata Mwili na Wanadamu Wanaotumiwa na Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki


Kwa miaka mingi Roho wa Mungu Amekuwa Akifanya kazi kwa kutafuta duniani. Kwa enzi nyingi Mungu Ametumia wanadamu wengi kufanya kazi Yake. Hata hivyo Roho wa Mungu bado hana mahali pazuri pa kupumzika. Kwa hivyo Mungu hupitia wanadamu mbalimbali kufanya kazi Yake na kwa kiasi kikubwa hutumia wanadamu kufanya hivyo. Yaani, katika miaka hii yote mingi, kazi ya Mungu haijawahi kusimama. Inaendelezwa mbele kupitia mwanadamu, bila kikomo mpaka siku ya leo. Ingawa Mungu Amesema na Ametenda mengi, mwanadamu bado hamjui Mungu, hii ni kwa sababu Mungu hajawahi kuonekana na mwanadamu na Yeye Hana umbo.